Sports
Jose Mourinho ‘akubali mkataba wa miaka miwili’ kujiunga na Benfica kama kocha mkuu
Mkufunzi mreno Jose Mourinho ameripotiwa kukubali kandarasi ya miaka miwili kuwa kocha mkuu wa Benfica, miaka 25 tangu alipohudumu kwa mara ya kwanza katika klabu hiyo.
Mourinho, mwenye umri wa miaka 62, amekuwa huru tangu alipofutwa kazi na Fenerbahce mwezi uliopita baada ya kushindwa kufuzu kwa Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Upatikanaji wa Mreno huyo uliibua uvumi mkubwa kuhusu hatima yake, lakini ripoti mapema wiki hii zilimhusisha kwa karibu na Benfica baada ya klabu hiyo kumtimua aliyekuwa kocha wa Wolves, Bruno Lage.
Hali hiyo imeharakishwa ndani ya saa 24 zilizopita, na Mourinho alionekana akiwasili nchini Ureno Jumatano usiku akitokea Barcelona, akiweka wazi hatua ya kuelekea klabuni hapo. Na, kwa mujibu wa Sky Sports, Mourinho sasa amekubali kurejea katika timu iliyompa kazi yake ya kwanza ya ukocha mwaka 2000 – ambapo atasaini mkataba wa miaka miwili.
Mwaka 2000, Mourinho alisimamia mechi 10 pekee, lakini mabadiliko ya uongozi wa juu wa klabu yalisababisha yeye kuwasilisha barua ya kujiuzulu – kabla ya kuchukua nafasi ya muda wote katika klabu ya Uniao de Leiria.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

