International News
Kampeni za uchaguzi mkuu za shika kasi Tanzania
Mgombea wa wadhfa wa Rais wa Jamhurui ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa chama cha Mapinzudi CCM taifa Dkt Samia Suluhu Hasssan anaendeleza kampeni za uchaguzi mkuu kwa chama hicho.
Rais Samia Suluhu, na mgombea mwenza Emmanuel Nchimbi kutoka chama tawala CCM, wamo katika harakati za kuwashawishi wapiga kura ili kuwachagua kuliongoza taifa hilo kwa awamu nyingine ya miaka mitano ijayo.
Siku ya Alhamis tarehe 11 Septemba 2025, Rais Samia Suluhu alifanya mkutano mkubwa wa siasa katika eneo la Urambo mkoani Tabora, ambako alizungumzia zaidi ufanisi wa maendeleo akisema umetokana na utawala bora wa chama cha Mapinduzi (CCM).
Miongoni mwa hayo ni kuboreshwa kwa muundo misingi ya barabara, afya na ustawi wa uchumi na biashara, na kutaja kimakusudi zao la Tumbaku linalokuzwa kwa wingi mkoani Tabora.
Rais Samia alisema kuwa kunaongezeko kubwa la pato linalotokana na zao la Tumbaku ambapo sasa linauzwa kwa dola 2.5 kutoka bei ya zamani ya dola 1 kwa tani moja.

Kampeni za uchaguzi mkuu nchini Tanzania katika mji wa Urambo mkoa wa Tabora {picha kwa hisani}
Kwa upande wake, Mgombea mwenza Emmanuel Nchimbi alikuwa katika mkoa wa Katavi, kusasambua yale serikali ya Mama Samia Suluhu imepanga kuyatimiza punde tu itakapochaguliwa kuwaongoza Watanzania.
Tanzania inaingia kwenye kampeni za uchaguzi mkuu uliopangwa kufanyika Oktoba, 29 2025.
Mpinzani wake mkuu Tundu Lissu anaendelea kuzuiwa jela, kwa tuhma za uchochezi na uhaini.
Taarifa ya Eric Ponda
International News
Kumbukumbu za muaji ya kimbari Rwanda
Ni miaka 32 tangu kutokea kwa mauaji ya kimbari nchini Rwanda.
Leo, tarehe saba Aprili, raia wa Rwanda pamoja na dunia kwa ujumla wanaungana kukumbuka kuanza kwa mauaji ya kimbari ya mwaka 1994, ambapo zaidi ya watu laki nane, wengi wao wakiwa jamii ya Watutsi, waliuawa ndani ya kipindi cha siku mia moja.
Tarehe hii ni ya kihistoria kwa taifa hilo ambalo miaka 32 iliyopita lilikumbwa na moja ya matukio ya kikatili zaidi katika historia ya mwanadamu.
Mauaji hayo yalichochewa na kuuawa kwa aliyekuwa rais wa Rwanda Juvenal Habyarimana, tukio lililosababisha kuzuka kwa vurugu kote nchini.
Kilichofuatia ni mashambulizi ya kimbari kati ya Wahutu na Watutsi, ambapo zaidi ya watu milioni moja wanaripotiwa kupoteza maisha katika muda wa siku mia moja.
Wanawake, wanaume na watoto walilengwa katika mashambulizi hayo yaliyopangwa, jamii zikivunjika na dunia ikishuhudia tukio hilo kwa muda bila kuchukua hatua za haraka kuzuia maafa hayo.
Katika kuadhimisha siku hii, inayojulikana kama KWIBUKA, yenye maana ya “tunakumbuka,” bendera nchini Rwanda zinapepea nusu mlingoti, huku Rais Paul Kagame akitarajiwa kuwasha mwenge wa kumbukumbu katika makavazi ya Kigali.
Hata hivyo, licha ya historia hiyo ya maumivu, Rwanda imepiga hatua kubwa katika kipindi cha miongo mitatu iliyopita, ikijijenga upya kutoka jamii iliyogawanyika hadi kuwa taifa lenye umoja, likishuhudia maendeleo ya kijamii na kiuchumi pamoja na juhudi za maridhiano na haki kwa wahanga.
Leo hii, Rwanda inasimama kama mfano kwa mataifa mengine aduniani, huku wito wa kuhakikisha mauaji ya kimbari hayajirudii tena ukiendelea kusisitizwa.
Taarifa ya Hamis Kombe
International News
Rais wa Cameroon amteua mwanawe kuwa makamu wa rais
Taifa la Cameroon limeidhinisha mabadiliko ya kisheria kuhusu wadhfa wa makamu wa rais na kumpa mamlaka zaidi rais wa taifa hilo kufanya uteuzi upya.
Sheria hiyo mpya, inampa uwezi makamu wa rais kuchukua nafasi ya rais moja kwa moja iwapo rais wa taifa hilo amefariki ama amekubwa na ugonjwa na kushindwa kuendelelea na majukumu yake kama rais kabla ya uchaguzi kuandaliwa.
Bunge la taifa hilo siku ya Jumamosi liliidhinisha mabadiliko hayo ya kisheria na kutoa nafasi ya kuteuliwa kwa makamu wa rais ili kuhakikisha shughuli za kiserikali zinaendeshwa vyema baada ya bunge la kitaifa na seneti kupiga kura na kufanya mabadiliko hayo ya kisheria katika taifa hilo la Cameroon.
Wabunge wa bunge la kitaifa na Seneti nchini Cameroon walipiga kura 200 huku wengine 18 wakipinga na wengine 4 wakikwepa kikao hicho cha bunge, hatua iliyopelekea mswada huo kupitishwa.
Hatua hiyo sasa imefanya Rais wa Cameroon Paul Biya mwenye umri wa miaka 93 kumteua mwanawe Franck Emmanuel Biya kuwa makamu wa kwanza wa rais katika taifa hilo.

Rais wa Cameroon Paul Biya mwenye umri wa miaka 93 na mwanawe Franck Emmanuel aliyemteua kuwa makamu wa rais wa taifa hilo.
Ni hatua ambayo imeibua mjadala mkali nchini Cameroon na bara Afrika kwa jumla baada ya uteuzi huo kutangazwa rasmi Aprili 4, 2026.
Sheria hiyo pia imepiga marufuku wananchi wa taifa hilo kujadili kuhusu hali ya afya ya rais Biya, kukosoa utendakazi wake pamoja na maamuzi yanayofanywa na Ikulu ya rais.
Emmanuel amehudumu katika wadhfa wa mkuu wa majeshi mbali na kushikilia cheo kikuu katika wizara ya ulinzi nchini humo.
Rais Biya amekuwa mamlakani tangu 1982 na alishinda muhula wa nane kwenye uchaguzi mkuu mwaka uliopita.
Kuidhinishwa kwa mabadiliko haya ya kisheria nchini Cameroon kunatambulika kama tukio la kihistoria tangu mwaka 2008 ambapo taifa hilo lilishuhudia pingamizi za kisheria kutoka kwa wananchi baada ya bunge la kitaifa kuongeza hatamu ya uongozi wa rais na kusababisha maandamano makubwa.
Taarifa ya Hamis Kombe

