Connect with us

Sports

Kenya Harlequins Tayari Kwa Msururu wa Chistie 7s Nairobi

Published

on

Kocha Mkuu wa kilabu ya Kenya Harlequins na mchezaji wa zamani wa Shujaa, Samuel Odongo, ameonya kuwa wako tayari kwa vita wakati wa toleo la 59 la Christie 7s litakaloanza hii leo, Agosti hadi 17 katika uwanja wa RFUEA.

Baada ya msururu wa Prinsloo Sevens,kikosi hicho kimepangwa Kundi A wakiwa pamoja na mabingwa wa Prinsloo mara mbili mfululizo, Strathmore Leos, Zetech Oaks na MSC Rugby.

Harlequins, ambao kwa sasa wanashikilia nafasi ya saba kwenye msururu wa National Sevens wakiwa na pointi 24, wameweza kumaliza katika nafasi ya sita kwenye Driftwood na Prinsloo Sevens. Odongo, anayelenga kutetea taji la jumla la Quins, alibainisha kuwa ushindani utakuwa mkali, hasa ikizingatiwa kwamba migawo miwili ya mwanzo tayari imetoa mabingwa tofauti na pia kuongezwa kwa kikosi maalum cha Uganda, Ruga Ruga.

“Mashindano haya yatakuwa magumu. Migawo miwili iliyopita imeshuhudia mabingwa wawili tofauti, na pia kuwa na Ruga Ruga kunaleta upekee wa aina yake. Itakuwa wikendi yenye msisimko wa kupanda na kushuka, hasa kwa timu kubwa kushangazwa, na tunatumai hatutajikuta kwenye kapu hilo,” alisema Odongo.

Kauli yake iliungwa mkono na nahodha wa Quins na nyota wa zamani wa U-20, Richel Wangila, ambaye alionyesha kujiamini licha ya mwanzo wa msimu usio wa kuridhisha.

“Tumeendelea kujijenga na kuwa wavumilivu. Hata baada ya matokeo yasiyoridhisha kwenye misururu miwili ya mwanzo, tuko tayari kuwapatie mashabiki burudani ya kuvutia. Tunakazana kushinda mchezo wa kwanza, kisha kuchukua kila mechi inavyokuja, huku lengo kuu likiwa ni kufika fainali na kulinyakua kombe,” alisema Wangila.

Mashindano hayo ya siku tatu yanaanza leo kwa michuano ya vijana asubuhi, ikifuatiwa na mashindano ya wastaafu jioni. Hatua kuu ya Christie Sevens inaanza kesho, ambapo inatarajiwa kushuhudiwa mchezo wa kasi wa raga huku timu zikipambana kwa alama muhimu za msururu.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Entertainment

Arsenal Ikishinda Kombe Nitampa Main Man Rio Gari na Dadangu – Shuga Boy

Published

on

Mjadala mkali umeibuka katika kipindi cha COCO Asubuhi baada ya Shuga Boy, shabiki wa Manchester United, kuweka dau zito na la kushangaza dhidi ya Main Man Rio ambaye ni shabiki wa Arsenal.

Akizungumza kwenye kipindi cha COCO Asubuhi, kinachoendeshwa na Tatu Sure—inayojumuisha Shuga Boy mwenyewe, Main Man Rio na Solomon Zully—Shuga Boy alifunguka, akidai kuwa Arsenal hawana uwezo wa kubeba hata kombe moja msimu huu licha ya matarajio makubwa kutoka kwa mashabiki wao.

Kwa mujibu wa Shuga Boy, mashabiki wa Arsenal wamekuwa wakijipa matumaini makubwa ya kutwaa hadi vikombe vinne, lakini hali halisi uwanjani haioneshi dalili hizo. Alienda mbali zaidi na kuweka dau la kipekee kwa Main Man Rio, ambaye ni shabiki mkubwa wa Arsenal.

“Nilimwambia Main Man Rio, wakibeba kombe nitampa gari yangu. Sasa naongeza dau—wakishinda kikombe msimu huu, nitampa gari yangu pamoja na dadangu,” alisema Shuga Boy kwa msisitizo, kauli iliyozua kicheko na mjadala mkali studio.

Kauli hiyo imekuja katika kipindi ambacho Arsenal wamekuwa wakionyesha ushindani mkubwa chini ya kocha Mikel Arteta, wakijijenga kama moja ya timu zinazowania ubingwa wa Premier League. Licha ya maendeleo hayo, ukosefu wa vikombe katika misimu mingi bado unawapa wapinzani wao nafasi ya kuwabeza.

Kwa upande mwingine, Manchester United nao wanapitia kipindi cha mabadiliko, wakijaribu kurejea kwenye ubora wao wa zamani waliouonyesha enzi za Sir Alex Ferguson. Licha ya changamoto, bado wana historia nzito ya mafanikio, jambo linalowapa mashabiki wao kujiamini wanapojadili soka la Uingereza.

Usiku wa leo, macho ya mashabiki yataelekezwa kwenye mchezo wa ligi kati ya Manchester United dhidi ya Leeds United—mchezo unaotarajiwa kuwa na ushindani mkali, huku Shuga Boy akitumaini timu yake itapata ushindi na kuendeleza presha kwa wapinzani wao.

Wakati mabishano yakiendelea mitandaoni na kwenye studio za redio, swali kubwa linabaki: Je, Arsenal wataweza kuwanyamazisha wakosoaji wao kwa kubeba angalau kombe moja msimu huu, au kauli ya Shuga Boy itageuka kuwa unabii?

Continue Reading

Sports

Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting

Published

on

By

Mshambuliaji Kai Havertz aliifungia Arsenal F.C. bao la ushindi katika dakika za mwisho kabisa, na kuisaidia timu hiyo kuibuka na ushindi mwembamba wa 1-0 dhidi ya Sporting CP katika mechi ya mkondo wa kwanza wa robo fainali ya UEFA Champions League iliyochezwa Jana usiku.

Kikosi cha kocha Mikel Arteta kilifika katika Uwanja wa Estadio Jose Alvalade kikiwa kimeathiriwa na vipigo viwili mfululizo dhidi ya Manchester City F.C. kwenye fainali ya Kombe la Ligi na Southampton F.C. katika robo fainali ya Kombe la FA.

Kwa mara nyingine, Arsenal haikucheza kwa kiwango chake bora, lakini ilifanikiwa kupata ushindi kutokana na uokoaji mzuri wa kipa David Raya pamoja na umakini wa Havertz aliyefunga bao la ushindi katika muda wa nyongeza.

Arsenal sasa ina nafasi kubwa ya kufuzu nusu fainali kabla ya mechi ya marudiano itakayochezwa kaskazini mwa London tarehe 15 Aprili, ingawa italazimika kuboresha kiwango chake ikiwa inataka kushinda taji hilo kwa mara ya kwanza.

Vipigo dhidi ya City na Southampton vilikuwa mara ya kwanza msimu huu kwa Arsenal kupoteza mechi mbili mfululizo, huku kipigo cha Kombe la FA kikiwa cha tano kwao msimu huu.

Athari za matokeo hayo bado zilionekana Lisbon, ambapo Arsenal ilipata ugumu wa kucheza kwa mwendelezo mzuri, lakini kama ilivyokuwa mara kadhaa msimu huu, walipata njia ya kushinda licha ya kutocheza vizuri.

katika mechi nyingine hatua ya robo fainali ni kwamba Bayern Munich waliondoka na ushindi wa magoli 2-1 mikononi mwa Real Madrid katika uwanja wao wa nyumbani Estadio Santiago Bernabeu.

Magoli ya Bayern yakitiwa kimyani na mshmabulizi Luis kipindi cha kwanza naye Erling Haaland kipindi cha pili.

Mechi ya marudiano itachezwa juma lijalo April 15.

Continue Reading

Trending