Connect with us

Sports

Kikosi Cha Voliboli Malkia Strikers Kina Mortisha Kuelekea Mechi Ya Pili Dhidi ya Poland

Published

on

Kocha wa timu ya taifa ya mpira wa voliboli ya akina dada, Malkia Strikers, Geoffrey Omondi, ana matumaini makubwa kuelekea mechi yao ya pili ya Kundi “G” dhidi ya Poland katika Mashindano ya Dunia ya FIVB yanayoendelea Phuket, Thailand, leo jioni.

Kenya siku ya Jumamosi ilipoteza kwa seti za moja kwa moja (22-25, 08-25, 20-25) dhidi ya Ujerumani katika mechi ya ufunguzi wa makundi.

Akizungumza baada ya mazoezi ya Jumapili, Omondi alisema iwapo wachezaji wake wataendelea kutoka pale walipoishia Jumamosi, wanaweza kushangaza Poland, ambayo inashikilia nafasi ya tatu kwenye viwango vya dunia vya FIVB.

“Wachezaji walifanya kazi nzuri sana walipocheza na Ujerumani, na tunatumaini watakuwa na ari ileile watakapomenyana na Poland. Tumefanya mazoezi mazuri na kurekebisha maeneo tuliyolegea dhidi ya Ujerumani. Ninaamini tunaweza kusababisha mshangao dhidi ya Poland. Wachezaji wako na morali ya juu baada ya baadhi yao kulipwa posho zao, na sasa umakini uko kwenye mechi zilizobaki,” alisema Omondi, ambaye pia ni kocha wa Kenya Pipeline, mabingwa wa Ligi ya Taifa ya Shirikisho la Mpira wa Wavu Kenya (KVF).

“Iwapo tunaweza kushinda seti moja au mbili au hata kushinda mechi kabisa, basi hiyo itakuwa hatua kubwa. Timu hii ina uwezo wa kushindana katika kiwango cha juu iwapo watapata mechi nyingi za kirafiki za kimataifa kama tulizocheza kabla ya mashindano. Hii yote inalenga maandalizi ya Michezo ya Olimpiki ya 2028,” aliongeza.

Kenya wiki iliyopita ilicheza mechi za kirafiki dhidi ya Uhispania na wenyeji Vietnam na kupoteza zote. Mabingwa wa Afrika hao watakamilisha michezo ya makundi Jumatano kwa kukutana na Vietnam.

Timu mbili za juu mwishoni mwa michezo ya awali zitafuzu kuingia raundi ya pili.

Nahodha wa Malkia Strikers, Meldina Sande, alithibitisha kuwa baadhi ya wachezaji wamelipwa posho zao baada ya timu kulalamika awali kuwa serikali haijawalipa kwa wakati.

“Tunashukuru Wizara ya Michezo, Kamati ya Olimpiki ya Taifa la Kenya (NOC-K) kwa msaada wake. Sasa tuko tayari kushindana na kupata matokeo mazuri. Tunawashukuru Wakenya walioko nyumbani kwa sapoti yao, na tunawaombea tuwape furaha,” alisema Sande, ambaye anachezea Rwanda Police.

Kenya itacheza mechi ya mwisho Jumatano dhidi ya Vietnam.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting

Published

on

By

Mshambuliaji Kai Havertz aliifungia Arsenal F.C. bao la ushindi katika dakika za mwisho kabisa, na kuisaidia timu hiyo kuibuka na ushindi mwembamba wa 1-0 dhidi ya Sporting CP katika mechi ya mkondo wa kwanza wa robo fainali ya UEFA Champions League iliyochezwa Jana usiku.

Kikosi cha kocha Mikel Arteta kilifika katika Uwanja wa Estadio Jose Alvalade kikiwa kimeathiriwa na vipigo viwili mfululizo dhidi ya Manchester City F.C. kwenye fainali ya Kombe la Ligi na Southampton F.C. katika robo fainali ya Kombe la FA.

Kwa mara nyingine, Arsenal haikucheza kwa kiwango chake bora, lakini ilifanikiwa kupata ushindi kutokana na uokoaji mzuri wa kipa David Raya pamoja na umakini wa Havertz aliyefunga bao la ushindi katika muda wa nyongeza.

Arsenal sasa ina nafasi kubwa ya kufuzu nusu fainali kabla ya mechi ya marudiano itakayochezwa kaskazini mwa London tarehe 15 Aprili, ingawa italazimika kuboresha kiwango chake ikiwa inataka kushinda taji hilo kwa mara ya kwanza.

Vipigo dhidi ya City na Southampton vilikuwa mara ya kwanza msimu huu kwa Arsenal kupoteza mechi mbili mfululizo, huku kipigo cha Kombe la FA kikiwa cha tano kwao msimu huu.

Athari za matokeo hayo bado zilionekana Lisbon, ambapo Arsenal ilipata ugumu wa kucheza kwa mwendelezo mzuri, lakini kama ilivyokuwa mara kadhaa msimu huu, walipata njia ya kushinda licha ya kutocheza vizuri.

katika mechi nyingine hatua ya robo fainali ni kwamba Bayern Munich waliondoka na ushindi wa magoli 2-1 mikononi mwa Real Madrid katika uwanja wao wa nyumbani Estadio Santiago Bernabeu.

Magoli ya Bayern yakitiwa kimyani na mshmabulizi Luis kipindi cha kwanza naye Erling Haaland kipindi cha pili.

Mechi ya marudiano itachezwa juma lijalo April 15.

Continue Reading

Sports

Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)

Published

on

By

Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.

Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.

SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

Continue Reading

Trending