Sports
Mahakama Kuu ya Kakamega yatupilia mbali ombi la Patrick Matasi, FKF yapewa ruhusa kuendelea na nidhamu dhidi yake
Mahakama Kuu mjini Kakamega imetupilia mbali ombi lililowasilishwa na mlinda lango wa zamani wa Harambee Stars, Patrick Matasi, hatua ambayo imeiruhusu rasmi Shirikisho la Soka la Kenya (FKF) kuendelea na hatua za kinidhamu dhidi yake kuhusiana na madai ya upangaji wa matokeo ya mechi (match-fixing).
Uamuzi huo ni ushindi mkubwa kwa FKF katika vita vyake dhidi ya udanganyifu kwenye soka, baada ya mahakama kuthibitisha kuwa shirikisho hilo lilitenda ndani ya mamlaka yake chini ya Kanuni za FKF za Kupambana na Upangaji wa Mechi.
Matasi alikuwa amewasilisha kesi mwezi Aprili 2025, na kupata amri za muda (conservatory orders) zilizozuia kwa muda FKF kutekeleza adhabu yake ya kusimamishwa kwa siku 90.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

