Business
Mataifa yanayoshuhudia ghasia yaibua wasiwasi wa usafiri wa ndege
Kenya inapolenga kuongeza ushuru unaokusanywa katika sekta ya uchukuzi wa angani, suala la usalama wa ndege zinazosafiri kupitia mataifa yanayoshuhudia ghasia limeibua wasiwasi.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya safari za ndege nchini Mary Keter alisema mabadiliko ya sera yanahitajika ili kupatia kipaumbele suala la ukaguzi na utathmini wa hatari zilizopo ili kuhakikisha ustawi hauathiri usalama au uendeshaji wa biashara.
Ikumbukwe kwamba shughuli za uchukuzi wa abiria humu nchini ziliongezeka kwa asilimia 38.5 mwaka uliopita huku wasafiri zaidi ya milioni 10 wakitumia uwanja wa kimataifa wa ndege wa Jomo Kenyatta.
Haya yanajiri huku mikakati zaidi ikiendelezwa naMamlaka hiyo kuhakikisha uchukuzi wa angani unaimarika kwa asilimia kubwa licha ya changamoto za kiuchumi zinazolikumba taifa hili.
Taarifa ya Pauline Mwango
Business
Biashara ya Mananasi yakabiliwa na changamoto Kilifi
Wafanyibiashara kuuza matunda aina ya Nanasi kaunti ya Kilifi wanasema biashara ya matunda hayo inazidi kudorora msimu huu ikilinganishwa na msimu uliopita.
Kulingana na wafanyibiashara hao, matunda ya Mananasi hayapatikana kwa urahisi sokoni kutokana na mabadiliko ya hali ya angani licha ya biashara ya matunda hayo kuwa na thamani kubwa katika soko la Pwani na taifa.
Wakiongozwa na Japhet Khambi, wafanyibiashara hao walisema kwa sasa wanategemea matunda hayo kutoka nje ya nchi hasa taifa la Uganda ambapo uagizaji wa matunda hayo umekuwa ghali mno.
Katika suala la usafirishaji wa bidhaa hiyo katika soko la kaunti ya Kilifi kutoka taifa hilo jirani la Afrika Mashariki, wafanyibiashara hao walisema ghamara ya usafiri uko juu mno hali ilichangia bei ya bidhaa hizo kuongezeka mara dufu.
“Hii mambo ya gharama ya usafirishaji na uhaba wa matunda hayo bei ya bidhaa hiyo imepanda kwa kiwango kikubwa, alieleza Khambi.
Wafanyibiashara wa matunda ya Mananasi walisema Nanasi ambalo lilikuwa Linanunuliwa kwa shilingi 100 sasa tunda hilo limepanda bei na kuuzwa kwa shilingi 250.
“ Tulikuwa tunanunua Mananasi kutoka eneo la Chakama katika eneo bunge la Magarini kaunti ya Kilifi kwa bei nafuu lakini kwa sasa hayapatikani na kutulazimu kuangiza matunda kutoka Uganda.”, alisema Khambi.
Taarifa ya Pauline Mwango
Business
Bei za mafuta kuongezeka katikati ya mwezi aprili
Kenya sasa inakabiliwa na hatari ya kupanda kwa bei za mafuta, huku mgogoro unaoendelea mashariki ya Kati ukianza kuathiri bei nchini.
Serikali sasa imeonya kuwa kufikia katikati ya mwezi Aprili, bei za mafuta huenda zikapanda ikionya kuwa ongezeko la bei ya mafuta kwa sasa haliwezi kuepukika kufuatia kupanda kwa bei za mafuta kimataifa.
Waziri wa hazina kuu ya kitaifa John Mbadi aliwahakikishia wakenya kuwa hakuna cha kuhofia kwani wameweka mikakati kupunguza athari zake.
Ili kupunguza athari za bei za mafuta kuongezeka, serikali ilisema itatumia shilingi bilioni 17 kutoka mfuko wa ada ya uwekezaji wa mafuta kusaidia kudhibiti bei kwa mda wa miezi 3 ijayo.
Kwa sasa serikali inasema kuna akiba ya kutosha ya mafuta na shehena zaidi zinatarajiwa nchini hivi karibuni.
Taarifa ya Joseph Jira

