Connect with us

Sports

Matayarisho yamekamilika kwa Fainali ya Kusisimua ya Misruru ya Raga ya Wachezaji Saba kila Upande Jijini Kisumu

Published

on

Shughuli zote ziko tayari kwa ajili ya fainali ya kusisimua ya Raga ya Taifa ya Mizunguko ya Saba mwaka 2025, itakayofanyika jijini Kisumu marufu kama Dala Sevens katika Uwanja wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta, Mamboleo, kuanzia Septemba 13–14.

Kwa sasa, KCB RFC na Strathmore Leos wako kwenye pambano kali la kuwania ubingwa wa jumla, na macho yote yataelekezwa Kisumu ambapo mzunguko huu wa mwisho unatarajiwa kutoa burudani kubwa la raga na shangwe za mashabiki.

Dala Sevens imekua na kuwa moja ya mashindano yenye ushindani mkubwa na yenye hisia nyingi nchini, na mwaka huu hautakuwa tofauti. Tupo tayari kukaribisha familia ya raga Kisumu kwa wikendi kubwa,” alisema Mwenyekiti wa Kisumu RFC, Gabriel Ouma, wakati jiji la kando ya Ziwa likijiandaa kwa fainali hiyo kubwa.

Akizungumzia maandalizi, Ouma alionyesha kujiamini katika kutoa uzoefu wa kipekee ndani na nje ya uwanja.
“Dala Sevens imekua kuwa moja wa mashindano makali na yenye mvuto mkubwa, na mwaka huu pia itakuwa hivyo. Tupo tayari kuwapokea mashabiki wa raga Kisumu kwa wikendi ya kukumbukwa.

“Ufadhili wa Tusker umechangia sana kuinua ubora wa mashindano haya, na tunatarajia mashabiki kujitokeza kwa wingi kufurahia raga ya kiwango cha juu na mazingira ya kipekee ya Dala Sevens.”

Mashindano ya mwaka huu yamepata msukumo baada ya Tusker kuthibitisha ufadhili wa Ksh milioni 3 kwa ajili ya kuunga mkono Dala Sevens.

Ushirikiano huu unaendeleza dhamira ya muda mrefu ya Tusker katika kudhamini raga ya Kenya na kusherehekea shauku na uvumilivu wa wanariadha wa nyumbani.

“Raga ina nafasi ya kipekee katika mioyo ya Wakenya, na Dala Sevens kila mara imekuwa tukio kubwa la msimu,” alisema Keza Mpyisi, Meneja wa Michezo wa Tusker Brand.
“Tunajivunia kusimama na Kisumu RFC na familia pana ya raga tunapokaribia tamati ya mzunguko huu. Kwa Tusker, si suala la kudhamini tu, bali ni kuwaleta mashabiki pamoja kusherehekea ubora, kipaji na roho ya michezo ya Kenya.”

Kwa sasa, KCB Rugby wanaongoza mzunguko kwa alama 104 na wanahitaji tu kufika nusu fainali ili kutwaa ubingwa, huku Strathmore Leos wenye alama 95 wakihitaji safari kamili ya ushindi Kisumu ili kuendeleza matumaini yao.

Makundi ya Dala Sevens:

  • Kundi A: Kabras Sugar, CUEA Monks, MMUST, Nakuru RFC

  • Kundi B: Daystar Falcons, MSC Rugby, Kenya Harlequin, Nondescripts

  • Kundi C: KCB Rugby, Mwamba RFC, Homeboyz RFC, Embu RFC

  • Kundi D: Strathmore Leos, Menengai Oilers, Impala RFC, Kisumu RFC

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting

Published

on

By

Mshambuliaji Kai Havertz aliifungia Arsenal F.C. bao la ushindi katika dakika za mwisho kabisa, na kuisaidia timu hiyo kuibuka na ushindi mwembamba wa 1-0 dhidi ya Sporting CP katika mechi ya mkondo wa kwanza wa robo fainali ya UEFA Champions League iliyochezwa Jana usiku.

Kikosi cha kocha Mikel Arteta kilifika katika Uwanja wa Estadio Jose Alvalade kikiwa kimeathiriwa na vipigo viwili mfululizo dhidi ya Manchester City F.C. kwenye fainali ya Kombe la Ligi na Southampton F.C. katika robo fainali ya Kombe la FA.

Kwa mara nyingine, Arsenal haikucheza kwa kiwango chake bora, lakini ilifanikiwa kupata ushindi kutokana na uokoaji mzuri wa kipa David Raya pamoja na umakini wa Havertz aliyefunga bao la ushindi katika muda wa nyongeza.

Arsenal sasa ina nafasi kubwa ya kufuzu nusu fainali kabla ya mechi ya marudiano itakayochezwa kaskazini mwa London tarehe 15 Aprili, ingawa italazimika kuboresha kiwango chake ikiwa inataka kushinda taji hilo kwa mara ya kwanza.

Vipigo dhidi ya City na Southampton vilikuwa mara ya kwanza msimu huu kwa Arsenal kupoteza mechi mbili mfululizo, huku kipigo cha Kombe la FA kikiwa cha tano kwao msimu huu.

Athari za matokeo hayo bado zilionekana Lisbon, ambapo Arsenal ilipata ugumu wa kucheza kwa mwendelezo mzuri, lakini kama ilivyokuwa mara kadhaa msimu huu, walipata njia ya kushinda licha ya kutocheza vizuri.

katika mechi nyingine hatua ya robo fainali ni kwamba Bayern Munich waliondoka na ushindi wa magoli 2-1 mikononi mwa Real Madrid katika uwanja wao wa nyumbani Estadio Santiago Bernabeu.

Magoli ya Bayern yakitiwa kimyani na mshmabulizi Luis kipindi cha kwanza naye Erling Haaland kipindi cha pili.

Mechi ya marudiano itachezwa juma lijalo April 15.

Continue Reading

Sports

Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)

Published

on

By

Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.

Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.

SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

Continue Reading

Trending