Sports
Mchezaji Tenesi Alcaraz Bingwa Tena
Mchezaji Tenesi anayeorodheshwa wa Pili duniani kwa sasa Carlos Alcaraz raia wa Uhispania ameweza kuandikisha rekodi mpya baada ya kushinda taji la pili kombe la Queens Cup Title baada ya kumlaza Jiri Licheka raia wa Czech kwa seti za 7-5, 6-7 (5/7), 6-2 kabila ya finali ya Wimblendon.
Nyota huyo raia wa Uhispania alimzidi mwenzake kwenye fainali baada ya kuonyesha makali tokea mwanzo huku mchezaji huyo anayeorodheshwa wa 30 akikubali kichapo hicho kwa muda lisali 2 na dakika 10.
Mwanatenesi huyo tayari ana mataji matano baada ya kuzishinda fainali za French Open,Rome Open,Monte Carlo na Rotherdam mwaka huu wa 2025.
Mwamba huyo hajapoteza katika mashindano fainali 18 mpaka sasa tangu fainali za Barcelona Open April 20.