News
Mpango wa matumizi ya kawi safi Kilifi kukabili mabadiliko ya hali ya anga
Kongamano la siku tatu kuhusu wiki ya upishi kutumia kawi safi limezinduliwa rasmi mjini Kilifi katika kaunti ya Kilifi huku serikali kuu ikimesema inaendelea kujumuisha kila eneo katika miradi mbali mbali ya maendeleo.
Waziri wa Kawi nchini Opiyo Wandayi alisema serikali kuu inashirikisha serikali za kaunti kwenye mipango ya kawi safi ili kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi.
Akizungumza katika kongamano hilo, waziri Wandayi alisema Kenya inaendelea kutekeleza matumizi ya kawi safi ili kuepuka athari za kiafya kwa watumizi pamoja uharibifu wa Mazingira.
Waziri Wandayi alisistiza kuwa kwa sasa serikali inauia kuafikia utekelezaji wa sheria na mipango ya kawi safi kwa kushirikiana na wadau tofauti kwa manufaa ya jamii.
Vile vile alidokeza kuwa serikali imeitegengea kaunti ya Kilifi zaidi ya shilingi bilioni 2 zitakazotumika kuunganisha nyumba elfu 21 za ziada na nguvu za umeme.
Kwa upande wake mkewe rais Bi Rachel Ruto alisema mpango huo wa upishi safi utakomoa familia nyingi mashinani kiuchumi, kuimarisha mazingira ya elimu kwa wanafunzi majumbani vile vile kuondoa kero la wanawake katika matumizi ya mbinu za kale za upishi.
Naye gavana wa kaunti ya Kilifi Gedion Mung’aro alisema mabadiliko ya tabia nchi yamekuwa na athari kubwa kwa wakaazi hasa maeno ya Ganze na Magarini, akisistiza kuwa kawi safi pekee itaokoa maisha ya wakaazi wengi.

Mama wa taifa Bi Rachel Ruto pamoja na Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro na Waziri wa Kawi nchini Opiyo Wandayi
Ubalozi wa Uingereza na Ujerumani hapa nchini ulishinikiza serikali kukumbatia kikamilifi matumizi ya kawi safi kwa kuafikia maendeleo endelevu sawa na kubuni nafasi zaidi za ajira, kwa kushirikiana na serikali za kaunti.
Kongamano hilo linatarajiwa kukamilika alhamisi Agost 28, 2025, kauli mbiu ikiwa ni kutekeleza mikakati na mipango ya upishi safi, mabadiliko, ushirikishwaji na uwezeshaji.
Taarifa ya Joseph Jira
News
Ethekon: Uchaguzi mkuu utakuwa huru, haki na uwazi
Tume huru ya uchaguzi na mipaka nchini IEBC imeanza rasmi zoezi la kuwasajili wapiga kura wapya kote nchini, huku ikilenga kuwasajili wapiga kura milioni 6.2, kabla ya uchaguzi mkuu ujao.
Mwenyekiti wa Tume hiyo Erastus Ethekon aliwahakikishia wakenya kwamba makamishna wa tume hiyo watahakikisha uchuguzi mkuu ujao unakuwa huru, haki na uwazi.
Akizungumza katika kaunti ya Kwale wakati wa kuzindua wa zoezi la usajili wa wakipiga kura kote nchini, Ethekon alisema serikali imewekeza raslimali za kutosha za kufanikisha zoezi hilo.
“Nataka kuwahakikishia wakenya kwamba tumejipanga kama IEBC na tuko na raslimali za kutosha kuhakikisha zoezi la usajili wa wapiga kura linaendeshwa vyema na uchaguzi mkuu utakuwa huru, haki na wazi ili kuhakikisha wakenya wanatekeleza jukumu lao la kidemokrasia na hatua hiyo tutafikia idadi ya wapiga kura zaidi ya milioni 27”, alisema Ethekon.
Naye Naibu Mwenyekiti wa IEBC Fahima Araphat alisema tayari maafisa wapya wa IEBC elfu 12 wameajiriwa kuhakikisha zoezi hilo liendeshwa vyema ili kusajili idadi kubwa ya wapiga kura
“Sisi tunafanya kazi yetu bila kuegemea upande wowote wa kisiasa na tuko tayari kuhakikisha anashinda uchaguzi anatangazwa mshindi kwa haki, na kama tuko na makarani elfu 12 na wote wasajili wapiga kura wapya elfu 10 kila moja tutakuwa na idadi kubwa ya wapiga kura, sasa hiyo ndio tunalenga kupata”, alisema Fahima.
Kwa upande wake Gavana wa kaunti ya Kwale Fatuma Achani, aliipongeza tume hiyo kwa zoezi hilo endelevu la wapiga kura, akisema ni hatua ya kipekee kwa jamii ambazo zimekosa fursa ya kujisajili kama wapiga kura.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi
News
IEBC yasema idadi ya wanaojisajili ni ndogo mno
Zoezi endelevu la usajili wa wapiga kura kote nchini limeng’oa nanga huku maafisa wa Tume huru ya uchaguzi na mipaka nchini IEBC wakilenga idadi kubwa ya vijana katika zoezi hilo.
Katika kaunti ya Kilifi eneo bunge la Kilifi Kazkazini, zoezi hilo limefanyika katika vituo vinne tofauti huku idadi ndogo ya wapiga kura ikishuhudiwa licha ya vuguvugu la TUKO KADI kuanzishwa na vijana ili kuwajisajili wapiga kura.
Akizungumza na Wanahabari wakati wa zoezi hilo, Naibu Afisa wa usajili wa wapiga kura katika eneo bunge la Kilifi Kazkazini Abdul Mohammed aliwarai vijana kujitokeza kwa wingi na kujisajili.
Mohammed pia aliwarai vijana kukoma kutumiwa vibaya na wanasiasa kwa manufaa yao binafsi, akipongeza vuguvugu lilionzishwa na vijana la TUKO KADI kama njia moja ya kuwahamasisha vijana kujisajili kama wapiga kura.
“Tumeanza zoezi hili na tunawahimiza vijana wajitokeze kwa wingi na kujisajili kama wapiga kura ili kutumia nafasi hiyo kuchagua viongozi wanawataka na wala wasikubali kutumiwa vibaya na wanasiasa”, alisema Mohammed.
Kwa upande wao baadhi ya vijana waliojisajili waliwarai vijana wenzao kujitokeza kwa wingi na kushiriki zoezi hilo ili kuchagua viongozi wanaohisi wataleta maendeleo sawa na kubuni nafasi za ajira.
Taarifa ya Elizabeth Mwende

