Connect with us

Sports

Mshambulizi wa PSG Ousmane Dembele ndiye Mchezaji bora tuzo ya Ballon d’Or ya wanaume katika sherehe iliyofanyika jijini Paris Jumatatu

Published

on

Mshambuliaji wa Ufaransa, Ousmane Dembele, ameshinda tuzo ya Ballon d’Or ya wanaume katika sherehe iliyofanyika jijini Paris Jumatatu, tuzo kubwa zaidi ya heshima binafsi katika soka, akitunukiwa kwa mchango wake mkubwa katika kikosi cha Paris Saint-Germain kilichotwaa ubingwa wa Ligi ya Mabingwa msimu uliopita.

Dembele, mwenye umri wa miaka 28, amemshinda nyota chipukizi wa Barcelona na Uhispania, Lamine Yamal, katika kinyang’anyiro hicho na kumrithi kiungo wa Manchester City na Uhispania, Rodri, aliyeshinda tuzo hiyo mwaka 2024.

Dembele, akiwa na hisia kali, alishindwa kuzuia machozi mara tatu wakati wa hotuba yake kabla ya mama yake kujiunga naye jukwaani.

  • Mshambulizi wa Arsenal, Viktor Gyokeres, alishinda tuzo ya Mshambuliaji Bora kutokana na ubora wake akiwa Sporting Lisbon ya Ureno msimu uliopita.

  • Gianluigi Donnarumma alitwaa tuzo ya Kipa Bora,

  • huku Kocha wa PSG, Luis Enrique, akitunukiwa tuzo ya Kocha Bora.

Dembele, aliyewahi kuchezea Borussia Dortmund na Barcelona, na aliyekuwa sehemu ya kikosi cha Ufaransa kilichotwaa Kombe la Dunia mwaka 2018, alifunga mabao 35 katika mashindano yote. PSG walitwaa Ligi ya Ufaransa, Kombe la Ufaransa, na kwa mara ya kwanza katika historia yao, Ligi ya Mabingwa Ulaya.

“Sina maneno ya kueleza… ulikuwa msimu wa kipekee na PSG,” alisema Dembele kwa hisia, akimuelezea kocha wake Luis Enrique kama “kama baba.”

“Hii ni tuzo ya mchezaji mmoja, lakini ukweli ni kwamba ilikuwa juhudi ya pamoja,” aliongeza Dembele, mmoja kati ya wachezaji tisa wa PSG walioteuliwa kwa tuzo hiyo.

“Ballon d’Or haikuwa lengo kubwa katika maisha yangu ya soka, lakini nilifanya kazi kwa bidii ili timu ishinde Ligi ya Mabingwa.”

Kwa upande mwingine, Lamine Yamal mwenye umri wa miaka 18, ambaye alikuwa mchezaji mwenza wa Dembele Barcelona alipoibuka mwaka 2023, alishinda tena Kopa Trophy kwa mchezaji bora mwenye umri chini ya miaka 21 — ikiwa ni mara ya pili mfululizo kutwaa heshima hiyo.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting

Published

on

By

Mshambuliaji Kai Havertz aliifungia Arsenal F.C. bao la ushindi katika dakika za mwisho kabisa, na kuisaidia timu hiyo kuibuka na ushindi mwembamba wa 1-0 dhidi ya Sporting CP katika mechi ya mkondo wa kwanza wa robo fainali ya UEFA Champions League iliyochezwa Jana usiku.

Kikosi cha kocha Mikel Arteta kilifika katika Uwanja wa Estadio Jose Alvalade kikiwa kimeathiriwa na vipigo viwili mfululizo dhidi ya Manchester City F.C. kwenye fainali ya Kombe la Ligi na Southampton F.C. katika robo fainali ya Kombe la FA.

Kwa mara nyingine, Arsenal haikucheza kwa kiwango chake bora, lakini ilifanikiwa kupata ushindi kutokana na uokoaji mzuri wa kipa David Raya pamoja na umakini wa Havertz aliyefunga bao la ushindi katika muda wa nyongeza.

Arsenal sasa ina nafasi kubwa ya kufuzu nusu fainali kabla ya mechi ya marudiano itakayochezwa kaskazini mwa London tarehe 15 Aprili, ingawa italazimika kuboresha kiwango chake ikiwa inataka kushinda taji hilo kwa mara ya kwanza.

Vipigo dhidi ya City na Southampton vilikuwa mara ya kwanza msimu huu kwa Arsenal kupoteza mechi mbili mfululizo, huku kipigo cha Kombe la FA kikiwa cha tano kwao msimu huu.

Athari za matokeo hayo bado zilionekana Lisbon, ambapo Arsenal ilipata ugumu wa kucheza kwa mwendelezo mzuri, lakini kama ilivyokuwa mara kadhaa msimu huu, walipata njia ya kushinda licha ya kutocheza vizuri.

katika mechi nyingine hatua ya robo fainali ni kwamba Bayern Munich waliondoka na ushindi wa magoli 2-1 mikononi mwa Real Madrid katika uwanja wao wa nyumbani Estadio Santiago Bernabeu.

Magoli ya Bayern yakitiwa kimyani na mshmabulizi Luis kipindi cha kwanza naye Erling Haaland kipindi cha pili.

Mechi ya marudiano itachezwa juma lijalo April 15.

Continue Reading

Sports

Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)

Published

on

By

Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.

Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.

SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

Continue Reading

Trending