Sports
Mujinga Kutoshiriki Mashindano ya Kipkeino Classic
Mwanariadha nyota kutoka Uswisi, Mujinga Kambundji, hatashiriki katika mashindano ya Kipkeino Classic yanayotarajiwa kufanyika Jumamosi, Mei 31 katika uwanja wa michezo wa Ulinzi, jijini Nairobi.
Kupitia ujumbe alioweka kwenye ukurasa wake wa Instagram Ijumaa iliyopita, Kambundji amethibitisha kuwa hatashiriki tena katika mashindano ya msimu huu wa riadha. Ameeleza kuwa sababu ya kusitisha msimu wake ni ujauzito, na ameahidi kurejea tena uwanjani mwaka ujao.
Kwenye taarifa yake Mujinga alisema, “Msimu umeisha, kwa sababu nzuri zaidi. Nina furaha sana kuwajulisha kuwa muujiza wetu mdogo uko njiani.” Kauli hiyo iliambatana na picha yake akionyesha matokeo ya uchunguzi wa ultrasound, ambao hutumika kuangazia maendeleo ya fetusi na tathmini ya ujauzito.
View this post on Instagram
Kambundji, mwenye umri wa miaka 32, ni mshindi wa medali za dunia mara kadhaa, ikiwa ni pamoja na medali ya shaba katika mashindano ya dunia ya riadha pamoja na mafanikio kwenye mashindano ya ndani ya baridi. Ametangaza kuwa anatarajia kurejea tena kwenye mashindano mwaka wa 2026.
Awali, mashindano ya Kipkeino Classic yalipangwa kufanyika katika uwanja wa Nyayo, lakini kutokana na ukarabati unaoendelea, yamehamishiwa katika uwanja wa Ulinzi Sports Complex
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

