Connect with us

News

Murkomen Amshambulia Muturi kwa Kushikilia Nyaraka za Siri za Serikali

Published

on

Waziri wa usalama wa ndani Kipchumba Murkomen amemkashifu aliyekuwa Waziri la utumishi wa umma Justin Muturi kwa madai ya kushikilia nyaraka muhimu za siri za serikali

Waziri Murkomen amesema hatua kama hiyo inaweza kuchangia athari za kisheria.

Akizungumza na Wanahabari, Waziri Murkomen ameeleza kwamba Muturi alipokuwa Mwanasheria mkuu nchini aliapa kutunza siri alipokuwa akishughulikia stakabadhi za serikali na kudai kushangazwa na Muturi.

Waziri Murkomen amedai kwamba anashuku Muturi ana nia mbaya ya kunyima stakabadhi za serikali, akidai kwamba katika mataifa mengine mtu kama huyo angeweza kufungwa jela.

Waziri huyo pia alirejelea kesi ya 2016 iliyomhusisha aliyekuwa Waziri wa Mambo ya nje wa Marekani Hillary Clinton ambaye alishtakiwa kwa kutumia barua pepe ya kibinafsi kushughulikia maswala yanayohusiana na kazi, ambapo alitishia usalama wa taifa.

Murkomen hata hivyo imeitaka idara ya upelelezi wa jinai nchini DCI, ile ya ujasusi nchini NIS pamoja na Ofisi ya mkurugenzi wa mashtaka ya umma nchini ODPP kumkamata Muturi na kumfungulia mashtaka.

Itakumbukwa kwamba Muturi alitimuliwa kazini na Rais William Ruto kutokana na msimamo wake wa kuikosoa serikali kufuatia visa vya utekaji nyara na mauaji ya kiholela, ufisadi ndani ya serikali pamoja na kudhalilishwa kwa mawaziri nchini.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Polisi wanachunguza tukio la wizi dhidi ya raia wa kigeni

Published

on

By

Maafisa wa Polisi kaunti ya Mombasa wanachunguza tukio la wizi dhidi ya mtalii wa kigeni lililotokea katika eneo la Nyali

Kulingana na ripoti ya maafisa wa polisi, mtalii huyo mwenye umri wa miaka 51 ambaye ni raia wa Marekani, anadai kulaghaiwa na kisha kushambuliwa na kundi la wanaume aliyokutana nao muda mfupi kabla ya tukio.

Ripoti hiyo imeeleza kwamba mnamo mwezi Aprili 9 mwaka huu, raia huyo wa kigeni akiwa katika mkahawa mmoja eneo la Nyali jijini Mombasa, alikutana na mwanaume aliyejitambulisha kama Alex, ambaye alimshawishi kuelekea katika nyumba ya Airbnb iliyoko karibu na mkahawa huo.

Taarifa hiyo ilifafanua zaidi kwamba alipofika katika chumba hicho, alikumbana na wanaume wengine watano waliokuwa wakimsubiri ambapo mlango ulifungwa na kisha akashambuliwa na kulazimishwa kutoa pesa na vitu vya thamani.

Wahalifu hao walitoroka na mali mbalimbali ikiwemo simu ya rununu, kompyuta mpakato (laptop), fedha taslimu pamoja na fedha za kigeni na pia walifanikiwa kutoa pesa kutoka kwenye kadi zake za benki kwa njia ya udanganyifu.

Maafisa wa polisi kutoka Bamburi kwa kushirikiana na maafisa wa upelelezi wa DCI Nyali walifika eneo la tukio na kuanza uchunguzi, ingawa hadi sasa hakuna mtu aliyekamatwa wala mali iliyopatikana.

Kesi hiyo imewekwa chini ya uchunguzi zaidi huku juhudi zikiendelea kuwabaini na kuwakamata wahusika wa tukio hilo.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

News

Polisi eneo la Likoni-Mombasa inachunguza kifo cha mwanamke

Published

on

By

Idara ya usalama eneo la Likoni kaunti ya Mombasa imesema inachunguza kifo cha mwanamke mmoja aliyefariki katika mtaa wa senti kumi.

Mkuu wa polisi wa Likoni Joseph Mutungi alisema mwanamke huyo anadaiwa kupoteza maisha wakati wakiwa nyumbani kwa mwanamme anayesemekana kuwa mchumba wake.

Taarifa za awali ziliarifu kuwa marehemu alikuwa mgonjwa na anadaiwa alifika hospitalini kusaka matibabu japo hakupata huduma na kurejea nyumbani bila kutibiwa.

Inasemekana baadaye mchumba wake alioondoka kwenda kazini na kumwacha chini ya uangalizi wa mwanamke mwengine katika ploti hiyo.

Hali yake inadaiwa kuzorota na hatimaye kuaga dunia.

Maafisa wa usalama walisema wanaendelea na uchunguzi kubaini chanzo cha kifo hicho.

Mwili wa marehemu unahifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti katika hospitali ya Coast general kwa uchunguzi zaidi.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Trending