Connect with us

News

Mwaura: Hakuna Mswada wa Fedha wa Mwaka 2025 uliyowasilishwa Bungeni

Published

on

Serikali imejitokeza na kupinga taarifa zinazoendelea katika mitandao ya kijamii kwamba inalenga kuwasilisha mswada wa fedha wa mwaka wa 2025 bungeni ambao unalenga kuongeza ushuru kwa wakenya.

Msemaji wa Serikali Isaac Mwaura amesema taarifa hizo ni propaganda zisizo na ukweli wowote na ambazo zinalenga kuwagonganisha wakenya kama ilivyoshuhudiwa mwezi Juni mwaka wa 2024 wakati wananchi walipozua vurugu kupinga mswada wa fedha.

Katika kikao na Wanahabari katika jumba la mikutano la KICC jijini Nairobi, Mwaura amesema japo serikali iko na mipango ya kutengeneza bajeti ya mwaka wa kifedha wa 2025/2026, ni lazima wananchi wahusishwe kikamilifu katika vikao vya kutoa maoni ya umma.

Msemaji huyo wa serikali amebainisha kwamba serikali itahakikisha inawashikiza wakenya wanaokwepa kulipa ushuru kuwajibika huku akisema wakenya zaidi ya milioni 8.5 wamenufaika na bima ya Afya ya Taifa Care.

Wakati huo huo ameelezea hatua zilizopigwa na serikali za kimaendeleo katika kipindi cha zaidi ya miaka miwili sasa, akisisitiza haja ya wakenya kuunga mkono serikali kufanikisha ajenda yake ya maendeleo kwa wananchi wote.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Polisi wanachunguza tukio la wizi dhidi ya raia wa kigeni

Published

on

By

Maafisa wa Polisi kaunti ya Mombasa wanachunguza tukio la wizi dhidi ya mtalii wa kigeni lililotokea katika eneo la Nyali

Kulingana na ripoti ya maafisa wa polisi, mtalii huyo mwenye umri wa miaka 51 ambaye ni raia wa Marekani, anadai kulaghaiwa na kisha kushambuliwa na kundi la wanaume aliyokutana nao muda mfupi kabla ya tukio.

Ripoti hiyo imeeleza kwamba mnamo mwezi Aprili 9 mwaka huu, raia huyo wa kigeni akiwa katika mkahawa mmoja eneo la Nyali jijini Mombasa, alikutana na mwanaume aliyejitambulisha kama Alex, ambaye alimshawishi kuelekea katika nyumba ya Airbnb iliyoko karibu na mkahawa huo.

Taarifa hiyo ilifafanua zaidi kwamba alipofika katika chumba hicho, alikumbana na wanaume wengine watano waliokuwa wakimsubiri ambapo mlango ulifungwa na kisha akashambuliwa na kulazimishwa kutoa pesa na vitu vya thamani.

Wahalifu hao walitoroka na mali mbalimbali ikiwemo simu ya rununu, kompyuta mpakato (laptop), fedha taslimu pamoja na fedha za kigeni na pia walifanikiwa kutoa pesa kutoka kwenye kadi zake za benki kwa njia ya udanganyifu.

Maafisa wa polisi kutoka Bamburi kwa kushirikiana na maafisa wa upelelezi wa DCI Nyali walifika eneo la tukio na kuanza uchunguzi, ingawa hadi sasa hakuna mtu aliyekamatwa wala mali iliyopatikana.

Kesi hiyo imewekwa chini ya uchunguzi zaidi huku juhudi zikiendelea kuwabaini na kuwakamata wahusika wa tukio hilo.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

News

Polisi eneo la Likoni-Mombasa inachunguza kifo cha mwanamke

Published

on

By

Idara ya usalama eneo la Likoni kaunti ya Mombasa imesema inachunguza kifo cha mwanamke mmoja aliyefariki katika mtaa wa senti kumi.

Mkuu wa polisi wa Likoni Joseph Mutungi alisema mwanamke huyo anadaiwa kupoteza maisha wakati wakiwa nyumbani kwa mwanamme anayesemekana kuwa mchumba wake.

Taarifa za awali ziliarifu kuwa marehemu alikuwa mgonjwa na anadaiwa alifika hospitalini kusaka matibabu japo hakupata huduma na kurejea nyumbani bila kutibiwa.

Inasemekana baadaye mchumba wake alioondoka kwenda kazini na kumwacha chini ya uangalizi wa mwanamke mwengine katika ploti hiyo.

Hali yake inadaiwa kuzorota na hatimaye kuaga dunia.

Maafisa wa usalama walisema wanaendelea na uchunguzi kubaini chanzo cha kifo hicho.

Mwili wa marehemu unahifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti katika hospitali ya Coast general kwa uchunguzi zaidi.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Trending