Sports
Novak Djokovic Kusaka Taji La 25 La Wimbledone Hii Leo
Nyota wa mchezo wa Tenesi Ulimwenguni Novak Djokovic raia wa Serbia anaingia leo ulingoni kusaka taji la 25 la Wimbledon.
Hata hivyo mchezaji huyo anatarajiwa upinzani mkubwa kutoka kwa Carlos Alcaraz raia wa Uhispania ambaye anaorodheshwa wa pili kote ulimwenguni na Jennik Sinner anayeorodheshwa wa kwanza kote ulimwenguni.
Bingwa huyo ambaye ana mataji 24 kwa sasa akiwa kwenye kiwango kimoja na Magret Court anamini kwamba anauza kuwa Mwanatenesi wa kwanza kushinda taji la 25 na kuingia kwenye daftari za kumbukumbu kabla ya kustaafu.
Mshindi huyo mara nane wa tuzo hilo la Wimbledon amepoteza fainali mbili mfululizo kwa nyota wa Uhispania Carlos Alcaraz.
Djokovic anatarajiwa kufungua kampeini yake dhidi ya Alexandre Muller raia wa Ufaransa Leo Usiku.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

