Connect with us

Sports

Nyota wa U20 Lawrence Ouma Okoth na Austine Odhiambo Waitwa Harambee Stars Kwa Mara ya Kwanza

Published

on

Mshambuliaji chipukizi wa Kenya U-20 Lawrence Ouma Okoth amepokea wito wake wa kwanza katika kikosi cha timu ya taifa ya wakubwa baada ya kocha mkuu Benni McCarthy kutangaza kikosi cha Harambee Stars kitakachocheza mechi za mwisho za kufuzu Kombe la Dunia la FIFA dhidi ya Burundi na Ivory Coast.

Okoth, mshambuliaji anayechezea klabu ya ngazi ya juu nchini Finland SJK Seinäjoki, ni mmoja wa nyota waliyojumuishwa. Fowadi huyo mwenye umri wa miaka 19 anatoka katika Michael Olunga Football Academy (MOFA) na aliweka historia mapema mwaka huu kwa kuwa Mkenya wa kwanza kufunga bao kwenye AFCON U-20, akifunga kichwa cha kukumbukwa dhidi ya Morocco.

Kikosi pia kinashuhudia kurejea kwa Austin Odhiambo na Daniel Sakari, waliokosa mechi za kufuzu zilizopita dhidi ya Gambia na Shelisheli. Beki anayesakata soka Uingereza Vincent Harper pia ameitwa tena, akitafuta kucheza mechi yake ya kwanza ya kimataifa baada ya kuwa kwenye kikosi kilichocheza kirafiki dhidi ya Urusi mwaka 2023.

Orodha ya wachezaji 25 ya McCarthy imechanganya vipaji vipya na wale wazoefu waliowawezesha Kenya kufika robo fainali ya CHAN 2024, akiwemo kipa Byrne Omondi, kiungo Alpha Onyango, na mabeki Sylvester Owino na Alphonce Omija.

Kenya itasafiri kwanza kwenda Bujumbura kuvaana na Burundi mnamo Oktoba 9 katika Uwanja wa Intwari, kisha kuhitimisha kampeni yao dhidi ya Ivory Coast mnamo Oktoba 14 katika Uwanja wa Alassane Ouattara, Abidjan.

Kwa sasa Stars wako nafasi ya tano kwenye kundi lao wakiwa na pointi tisa na hawawezi tena kufuzu kwa Kombe la Dunia 2026, lakini watahitaji kuhitimisha kampeni kwa heshima. Kikosi kinatarajiwa kuingia kambini mapema Oktoba, huku safari za mwisho zikitegemea tathmini za kiafya na mazoezi ya utimamu wa mwili.

Wito kwa Okoth na Harper unaonyesha dhamira ya Benni McCarthy ya kuunganisha vipaji vya vijana na wale wa nje ya nchi katika kikosi cha wakubwa, ishara ya mwelekeo wa kujenga timu thabiti kwa mashindano ya bara na dunia yajayo.

Kikosi cha Harambee Stars

Makipa:
Faruk Shikhalo, Byrne Omondi, Brian Bwire

Mabeki:
Manzur Suleiman, Vincent Harper, Sylvester Owino, Alphonce Omija, Collins Sichenje, Michael Kibwage, Ronney Onyango, Abud Omar, Daniel Sakari

Viungo:
Alpha Onyango, Duke Abuya, Timothy Ouma, Ben Stanley, Marvin Nabwire, Austin Odhiambo

Viungo wa pembeni (Wingers):
William Lenkupae, Job Ochieng, Boniface Muchiri

Washambuliaji:
Michael Olunga, Ryan Ogam, Lawrence Okoth

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting

Published

on

By

Mshambuliaji Kai Havertz aliifungia Arsenal F.C. bao la ushindi katika dakika za mwisho kabisa, na kuisaidia timu hiyo kuibuka na ushindi mwembamba wa 1-0 dhidi ya Sporting CP katika mechi ya mkondo wa kwanza wa robo fainali ya UEFA Champions League iliyochezwa Jana usiku.

Kikosi cha kocha Mikel Arteta kilifika katika Uwanja wa Estadio Jose Alvalade kikiwa kimeathiriwa na vipigo viwili mfululizo dhidi ya Manchester City F.C. kwenye fainali ya Kombe la Ligi na Southampton F.C. katika robo fainali ya Kombe la FA.

Kwa mara nyingine, Arsenal haikucheza kwa kiwango chake bora, lakini ilifanikiwa kupata ushindi kutokana na uokoaji mzuri wa kipa David Raya pamoja na umakini wa Havertz aliyefunga bao la ushindi katika muda wa nyongeza.

Arsenal sasa ina nafasi kubwa ya kufuzu nusu fainali kabla ya mechi ya marudiano itakayochezwa kaskazini mwa London tarehe 15 Aprili, ingawa italazimika kuboresha kiwango chake ikiwa inataka kushinda taji hilo kwa mara ya kwanza.

Vipigo dhidi ya City na Southampton vilikuwa mara ya kwanza msimu huu kwa Arsenal kupoteza mechi mbili mfululizo, huku kipigo cha Kombe la FA kikiwa cha tano kwao msimu huu.

Athari za matokeo hayo bado zilionekana Lisbon, ambapo Arsenal ilipata ugumu wa kucheza kwa mwendelezo mzuri, lakini kama ilivyokuwa mara kadhaa msimu huu, walipata njia ya kushinda licha ya kutocheza vizuri.

katika mechi nyingine hatua ya robo fainali ni kwamba Bayern Munich waliondoka na ushindi wa magoli 2-1 mikononi mwa Real Madrid katika uwanja wao wa nyumbani Estadio Santiago Bernabeu.

Magoli ya Bayern yakitiwa kimyani na mshmabulizi Luis kipindi cha kwanza naye Erling Haaland kipindi cha pili.

Mechi ya marudiano itachezwa juma lijalo April 15.

Continue Reading

Sports

Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)

Published

on

By

Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.

Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.

SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

Continue Reading

Trending