Connect with us

International News

Rais Samia aitisha mazungumzo na upinzani

Published

on

Rais wa Tanzania Samia Suluhu sasa ametaka mazungumzo na upinzani wa taifa hilo baada ya uchaguzi uliokumbwa na utata na ghasia.

Wito huu ukitolewa siku moja baada ya kukamatwa kwa katibu mkuu wa chama cha upinzani cha CHADEMA Amani Golugwa kwenye msako wa kuwatafuta washukiwa wa ghasia za baada ya uchaguzi.

Emmanuel Nchimbi ambaye ni makamu wa rais wa Tanzania alisema hatua hiyo ni kutoa fursa kwa wapinzani kusikizwa na kuhakikisha Tanzania inasalia yenye amani.

Nchimbi alisema rais Samia Suluhu Hassan anania ya kuweka udhabiti wa taifa hilo sawa na kuweka mazingira bora kwa wawekezaji.

Rais Samia amekosolewa pakubwa kutokana na uchaguzi huo ulioshuhudia kuzimwa kwa mitindao pamoja na kukandamizwa kwa vyombo vya habari.

Waangazili wa mashirika kama vile umoja wa afrika, na hata muungano wa mataifa ya kusini mwa afrika SADC yalisema uchaguzi huo haukuwa huru na haki.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

International News

Vita vya Iran vyasambaratisha biashara za kimataifa.

Published

on

By

Vita vya Iran vinaweza kuisha hivi karibuni au kuendelea kwa miezi kadhaa licha ya tamko la rais wa Marekani Donald Trump kuhusu mpango ya kumaliza vita hivyo.

Iwapo vita hivyo vitakomeshwa basi Hormuz itakapofunguliwa tena ilhali mtihani halisi utakuwa ni vipi minyororo ya usambazaji wa nishati, mbolea na bidhaa nyingine itaweza kurejea haraka.

Wakati wale wenye matumaini wakianza kuhisi kwamba vita kati ya Marekani na Israel dhidi ya Iran vilikuwa karibu kumalizika, mgogoro huo wa mwezi mzima unachukua mwelekeo mwingine tena.

Rais wa Marekani Donald Trump alionya Tehran kwamba hakutakuwa na kurudi nyuma kuhusu mashambulizi yaliyoongozwa ya Marekani, kinyume na kauli yake kwamba hivi karibuni Marekani itaondoka Iran na hatua za kijeshi za nchi hiyo zitakomeshwa ndani ya wiki mbili au tatu zijazo.

Iran, kwa upande wake, inaruhusu idadi ndogo ya meli kupita katika Mlango wa Hormuz, huku ikikanusha kuwa mazungumzo yoyote ya kusitisha vita yanaendelea.

Wataalamu wengi wanakubaliana juu ya jambo moja muhimu: kadiri mzozo huu unavyoendelea kwa muda mrefu, ndivyo athari zake zitakavyokuwa mbaya zaidi kwa usambazaji wa nishati duniani, mfumuko wa bei na uthabiti wa uchumi.

Benki ya hifadhi ya Shirikisho ya Dallas, ambayo ni sehemu ya mfumo wa benki kuu ya Marekani, ilitabiri mapema mwezi huu kwamba kufungwa kwa mlango huo kwa miezi mitatu au zaidi kungesababisha ukuaji wa pato la taifa la dunia kupungua kwa asilimia 2.9 kwa mwaka katika robo ya pili ya mwaka.

Continue Reading

International News

Trump asema Marekani itasitisha vita dhidi ya Iran

Published

on

By

Rais Donald Trump amesema kwamba Marekani itaondoka Iran hivi karibuni na hatua za kijeshi za nchi hiyo zitakomeshwa ndani ya wiki mbili au tatu zijazo.

Rais Trump alisema Marekani imefikia malengo iliyojiwekea kabla ya kuanza kwa mashambulizi ya anga dhidi ya Iran mwezi uliyopita kwa ushirikiano na Israel.

Aidha aliongeza kuwa lengo la kuizuia Iran kuwa na uwezo wa kuunda silaha za nyuklia limefikiwa na sasa Marekani inamaliza kazi.

Trump pia aliema Marekani sasa inatawala anga za Iran na pia imepata mabadiliko ya utawala kufuatia mauaji ya viongozi wakuu wa kisiasa na kijeshi.

Aliwataja viongozi hao wapya mjini Tehran kama walio na misimamo mikali na waadilifu zaidi, ikilinganishwa na watangulizi wao.

Trump pia alisema viongozi wa Iran wanaomba kufanya makubaliano na Marekani ili kumaliza vita, madai ambayo hapo awali yalipingwa na Iran na kuongeza kwamba vita vinaweza kumalizika bila makubaliano kati ya pande hizo mbili.

Kuhusu athari za vita hasa kupanda kwa bei ya mafuta, rais Trump alisema bei itashuka mara tu Marekani itakapomaliza hatua zake za kijeshi.

Continue Reading

Trending