International News
Rais Samia Suluhu wa CCM, aidhinishwa kugombea Urais Tanzania, Wapinzani Wakizuiliwa
Tume ya uchaguzi nchini Tanzania, INEC imemuidhinisha rasmi Rais Samia Suluhu Hassan wa Tanzania, na mgombea mwenza Emmanuel Nchimbi kuwa wagombea wa Urais kwa chama cha Mapinduzi CCM nchini humo.
Hatua hii imewekwa wazi kwamba Rais Samia huenda hatakuwa na upinzani mkubwa wakati wa uchaguzi mkuu utakapoandaliwa nchini humo baadaye Oktoba 29 mwaka huu baada ya tume hiyo kuwazuia wagombea wa vyama vikuu vya upinzani kushiriki uchaguzi huo.
Rais Samia Suluhu na mgembea mwenza Emmanuel Nchimba, sasa watakabiliana na wagombea wa vyama vidogo vidogo baada ya chama kikubwa cha upinzani CHADEMA, kinachooongozwa na Tundu Lisu, kuondolewa kwenye kinyang’anyiro hicho mnamo April 2025 kwa madai ya kukiuka na kukataa kutia saini makubaliano ya utaratibu na sheria za Uchaguzi.
Chama kingine cha upinzani kuondolewa hivi punde ni kile cha Alliance for Change and Transparency ACT- Wazalemdo kinachoongozwa na Luhaga Mpina.
Luhaga amekatazwa kushiriki uchaguzi huo na tume hiyo ya Uchaguzi, INEC.

Kinara wa cha chama cha ACT – Wazalendo, Luhaga Mpina.
Mwenyekiti wa chama cha CHADEMA Tundu Lissu, amekuwa kizuizini kwa zaidi ya miezi mine sasa baada ya kushtakiwa kwa kosa la Uhaini mwezi April mwaka huu.
Hata hivyo Tundu amekanusha madai hayo akisema kuwa ni njama ya CCM kuhujumu Upinzani katika ushirikishwaji wa uchaguzi mwaka huu.
Kukamatwa kwa Lissu na pamoja na kuongezeka kwa visa vya utekaji nyara wa wanaharakati wa haki za bimadamu nchini Tanzani, kumeipa doa serikali ya Samia Suluhu Hassan katika kujitolea kwake kudumisha haki na usawa, licha ya rais huyo kusisitizia Ulimwengu kwamba amejitolea kudumisha haki za binadamu.
Miongoni mwa visa vya utekaji nyara hivi majuzi ni Wakenya waliokuwa wamesafuiri nchini humo kufuatilia kesi ya Tundu Lisu, wakiongozwa na Martha Karua, Jaji mkuu mstaafu Willy Muntunga na mwanaharakati Boniface Mwangi.
Rais Suluhu aliingia mamlakani kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais wa Nchi hiyo John Pombe Magufuli kufariki 2021
International News
Vita vya Iran vyasambaratisha biashara za kimataifa.
Vita vya Iran vinaweza kuisha hivi karibuni au kuendelea kwa miezi kadhaa licha ya tamko la rais wa Marekani Donald Trump kuhusu mpango ya kumaliza vita hivyo.
Iwapo vita hivyo vitakomeshwa basi Hormuz itakapofunguliwa tena ilhali mtihani halisi utakuwa ni vipi minyororo ya usambazaji wa nishati, mbolea na bidhaa nyingine itaweza kurejea haraka.
Wakati wale wenye matumaini wakianza kuhisi kwamba vita kati ya Marekani na Israel dhidi ya Iran vilikuwa karibu kumalizika, mgogoro huo wa mwezi mzima unachukua mwelekeo mwingine tena.
Rais wa Marekani Donald Trump alionya Tehran kwamba hakutakuwa na kurudi nyuma kuhusu mashambulizi yaliyoongozwa ya Marekani, kinyume na kauli yake kwamba hivi karibuni Marekani itaondoka Iran na hatua za kijeshi za nchi hiyo zitakomeshwa ndani ya wiki mbili au tatu zijazo.
Iran, kwa upande wake, inaruhusu idadi ndogo ya meli kupita katika Mlango wa Hormuz, huku ikikanusha kuwa mazungumzo yoyote ya kusitisha vita yanaendelea.
Wataalamu wengi wanakubaliana juu ya jambo moja muhimu: kadiri mzozo huu unavyoendelea kwa muda mrefu, ndivyo athari zake zitakavyokuwa mbaya zaidi kwa usambazaji wa nishati duniani, mfumuko wa bei na uthabiti wa uchumi.
Benki ya hifadhi ya Shirikisho ya Dallas, ambayo ni sehemu ya mfumo wa benki kuu ya Marekani, ilitabiri mapema mwezi huu kwamba kufungwa kwa mlango huo kwa miezi mitatu au zaidi kungesababisha ukuaji wa pato la taifa la dunia kupungua kwa asilimia 2.9 kwa mwaka katika robo ya pili ya mwaka.
International News
Trump asema Marekani itasitisha vita dhidi ya Iran
Rais Donald Trump amesema kwamba Marekani itaondoka Iran hivi karibuni na hatua za kijeshi za nchi hiyo zitakomeshwa ndani ya wiki mbili au tatu zijazo.
Rais Trump alisema Marekani imefikia malengo iliyojiwekea kabla ya kuanza kwa mashambulizi ya anga dhidi ya Iran mwezi uliyopita kwa ushirikiano na Israel.
Aidha aliongeza kuwa lengo la kuizuia Iran kuwa na uwezo wa kuunda silaha za nyuklia limefikiwa na sasa Marekani inamaliza kazi.
Trump pia aliema Marekani sasa inatawala anga za Iran na pia imepata mabadiliko ya utawala kufuatia mauaji ya viongozi wakuu wa kisiasa na kijeshi.
Aliwataja viongozi hao wapya mjini Tehran kama walio na misimamo mikali na waadilifu zaidi, ikilinganishwa na watangulizi wao.
Trump pia alisema viongozi wa Iran wanaomba kufanya makubaliano na Marekani ili kumaliza vita, madai ambayo hapo awali yalipingwa na Iran na kuongeza kwamba vita vinaweza kumalizika bila makubaliano kati ya pande hizo mbili.
Kuhusu athari za vita hasa kupanda kwa bei ya mafuta, rais Trump alisema bei itashuka mara tu Marekani itakapomaliza hatua zake za kijeshi.

