News
Soma la Hisababiti ni Lazima, Asema Migos
Waziri wa Elimu nchini Julius Migos ametangaza kwamba Somo la Hisabati litakuwa la lazima katika shule za upili na kubatilisha tamko la awali la serikali la kulifanya somo hilo liwe la hiari.
Akizungumza wakati wa mtakano wa kitaifa kuhusu uboreshaji wa mtaala wa elimu nchini CBC, Waziri Migos amesema uamuzi huo ulifanywa baada ya wadau mbalimbali kujadili masuala ya CBC kutaka somo la Hisabati kuwa la lazima katika shule za upili.
Waziri Migos amesema wanafunzi ambao watachagua fani ya STEM ikiwemo ni somo la Sayansi, Teknlojia, Uhandisi na Hisabati watasomo Hisabati ya hali ya juu na wanafunzi watakaochagua njia nyingine mbili watasomo Hisabati iliyorahisishwa.
Katika mfumo huo mpya, wanafunzi watachukua masomo manne ya lazima, ambayo ni Lugha ya Ishara ya Kiingereza, Kiswahili, Elimu ya Kimwili, mafunzo ya huduma za jamii na masomo mengine matatu kutoka kwa kundi la chaguzi 38.
Uamuzi huo umejiri baada ya kupata pingamizi hapo awali kutoka kwa Chama cha walimu wa shule za upili na vyuo vya kadri nchini KUPPET wakiongozwa na Katibu wao mkuu Moses Nthurima kuhusu kulifanya somo la Hisabati kuwa la hiari
News
Polisi wanachunguza tukio la wizi dhidi ya raia wa kigeni
Maafisa wa Polisi kaunti ya Mombasa wanachunguza tukio la wizi dhidi ya mtalii wa kigeni lililotokea katika eneo la Nyali
Kulingana na ripoti ya maafisa wa polisi, mtalii huyo mwenye umri wa miaka 51 ambaye ni raia wa Marekani, anadai kulaghaiwa na kisha kushambuliwa na kundi la wanaume aliyokutana nao muda mfupi kabla ya tukio.
Ripoti hiyo imeeleza kwamba mnamo mwezi Aprili 9 mwaka huu, raia huyo wa kigeni akiwa katika mkahawa mmoja eneo la Nyali jijini Mombasa, alikutana na mwanaume aliyejitambulisha kama Alex, ambaye alimshawishi kuelekea katika nyumba ya Airbnb iliyoko karibu na mkahawa huo.
Taarifa hiyo ilifafanua zaidi kwamba alipofika katika chumba hicho, alikumbana na wanaume wengine watano waliokuwa wakimsubiri ambapo mlango ulifungwa na kisha akashambuliwa na kulazimishwa kutoa pesa na vitu vya thamani.
Wahalifu hao walitoroka na mali mbalimbali ikiwemo simu ya rununu, kompyuta mpakato (laptop), fedha taslimu pamoja na fedha za kigeni na pia walifanikiwa kutoa pesa kutoka kwenye kadi zake za benki kwa njia ya udanganyifu.
Maafisa wa polisi kutoka Bamburi kwa kushirikiana na maafisa wa upelelezi wa DCI Nyali walifika eneo la tukio na kuanza uchunguzi, ingawa hadi sasa hakuna mtu aliyekamatwa wala mali iliyopatikana.
Kesi hiyo imewekwa chini ya uchunguzi zaidi huku juhudi zikiendelea kuwabaini na kuwakamata wahusika wa tukio hilo.
Taarifa ya Mwanahabari wetu
News
Polisi eneo la Likoni-Mombasa inachunguza kifo cha mwanamke
Idara ya usalama eneo la Likoni kaunti ya Mombasa imesema inachunguza kifo cha mwanamke mmoja aliyefariki katika mtaa wa senti kumi.
Mkuu wa polisi wa Likoni Joseph Mutungi alisema mwanamke huyo anadaiwa kupoteza maisha wakati wakiwa nyumbani kwa mwanamme anayesemekana kuwa mchumba wake.
Taarifa za awali ziliarifu kuwa marehemu alikuwa mgonjwa na anadaiwa alifika hospitalini kusaka matibabu japo hakupata huduma na kurejea nyumbani bila kutibiwa.
Inasemekana baadaye mchumba wake alioondoka kwenda kazini na kumwacha chini ya uangalizi wa mwanamke mwengine katika ploti hiyo.
Hali yake inadaiwa kuzorota na hatimaye kuaga dunia.
Maafisa wa usalama walisema wanaendelea na uchunguzi kubaini chanzo cha kifo hicho.
Mwili wa marehemu unahifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti katika hospitali ya Coast general kwa uchunguzi zaidi.
Taarifa ya Mwanahabari wetu

