Connect with us

Entertainment

#UlijanjarukaVipi! Safari ya Mpishi Nguli, Don Moses: Kutoka Kukosa Karo Hadi Kuwa Head Chef

Published

on

Katika dunia ya leo ambapo changamoto za kiuchumi zimewaacha vijana wengi wakihangaika, simulizi ya Don Moses ni mwanga wa matumaini kwa wengi.

Akiwa mgeni katika kipindi cha Janjaruka 254, kinachorushwa kila siku ya wiki kuanzia Jumatatu hadi Ijumaa, Moses alisimulia safari yake ya ajabu kutoka kwa kijana aliyezuiwa na karo ya shule hadi kuwa mpishi mashuhuri hadi kuwa Head Chef aliyesimamia wapishi waliosomea fani hiyo chuoni.

Baada ya kuhitimu kidato cha nne, Moses alikuwa ameweka ndoto ya kujiunga na chuo lakini maisha yalikuwa na mpango tofauti. Mama yake alipata ajali mbaya, hali iliyolazimu familia kuhamishia raslimali kwenye matibabu badala ya karo yake ya chuo.

“Nilijua wazi kuwa singeweza kulazimisha familia ichague kati ya maisha ya mama na elimu yangu. Ilibidi nitafute njia mbadala,” anasema Moses.

Jiko la YouTube: Darasa la Ukombozi

Akiwa hana karo, lakini akiwa na shauku, Moses alianza kujifunza sanaa ya upishi kupitia video za YouTube. Binamu yake, Moses Gambo, ndiye aliyemfungulia mlango wa maarifa kwa kumtambulisha kwenye tutorials mbalimbali mtandaoni.

Ni ujuzi huo wa mtandaoni uliomfungulia milango ya ajira katika hoteli za kifahari, ambapo aliweza kupanda ngazi hadi kuwa mpishi mkuu (Head Chef) — akiongoza wapishi waliopitia vyuo vya kitaaluma. Ni mafanikio ambayo wengi hawakuyatarajia kutoka kwa kijana ambaye hakuingia darasa la kawaida, bali alikaa mbele ya skrini.

“Najua kwenye upishi kuna kupika mashendea ama kupika chakula kibaya ila sijawahi kufeli. Siku zote mimi ni makini na ratio ya viungo. Ndiyo silaha yangu,” anasema kwa kujiamini.

Mwaka wa Mageuzi: 2020

Kama ilivyokuwa kwa wengi, mwaka wa janga la COVID-19 – 2020 – ndiyo ulikuwa mwaka wa mabadiliko makubwa kwa Moses. Akiwa na muda mwingi na motisha mpya, alianza kupika kibiashara, akihudumia watu waliokuwa majumbani.

“Kabula ya hapo, nilikuwa napika kwa kujifurahisha tu. Lakini corona ilinifungua macho. Nikaanza kuona kuwa mapishi ni biashara yenye nguvu,” anasema Moses.

Karo Iliyogeuka Mtaji

Kipindi fulani baadaye, Moses alipata nafasi ya kujiunga na chuo hatimaye. Lakini kwa mshangao wa wengi, alikataa ofa hiyo kwa hiari na kuomba fedha hizo zitumike kupanua biashara yake ya upishi.

“Nitamudu gharama ya chuo siku moja. Kwa sasa, najenga misingi. Muda wa kusoma utafika,” anasema.

💡 Ushauri kwa Vijana: Anza na Kile Kilicho Mkono Wako

Don Moses sasa ni sauti ya matumaini kwa vijana wengi wanaohisi kuwa elimu ya juu au mtaji mkubwa ndio tiketi pekee ya mafanikio. Anasisitiza umuhimu wa kuanza na huduma, si lazima mtaji.

“Kama huna kazi wala mtaji, toa huduma kwanza. Ukiwa na bidii na ubunifu, malipo yatafuata,” anashauri.

Leo hii, sehemu kubwa ya mapato ya Moses huingia moja kwa moja kwenye ununuzi wa vifaa bora vya upishi, huku akiendeleza ndoto yake ya kuwa mmoja wa wapishi wakubwa zaidi nchini Kenya.

Continue Reading
1 Comment

1 Comment

  1. Austine oscar

    June 6, 2025 at 10:12 pm

    Tumeona kazi zako Boss kupitia mm mkufunzi wako heko na kupa cha zaidi nakuombea heri na mafanikio mema na uishi maisha marefu ju isingekuwa ww singekuwa mahali nilipo nashkuru Mungu Sana kwa umbali umenitoa ningetamani pia mm nifike mahali upo na Niko na Imani kubwa Sana hata ww mwenyewe walijuwa hilo ila IPO siku 🧨🙏

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Entertainment

Mimi Ndo Msanii Nimebaki Wengine ni Content Creators! – Hubby Africana

Published

on

Msanii wa nyimbo za kizazi kipya, Hubby Africana, ameibua mjadala mpana mitandaoni baada ya kauli yake ya hivi karibuni aliyochapisha kupitia ukurasa wake wa Facebook.

Kupitia ujumbe huo, Hubby Africana alijinasibu kuwa yeye ndiye msanii halisi aliyebaki katika tasnia, akiwatuhumu wengine kwa kugeukia zaidi uundaji wa maudhui badala ya muziki.

Aliandika kwa kujiamini: “Mimi ndo msanii nimebaki🤔 hao wengine wamekua content creator😂😂 very soon mtanielewa #mnyama is coming stay tuned 🔥💯.”

Hubby Africana si jina geni kabisa pwani. Msanii huyo alishiriki kwenye makala ya kwanza ya Kilifi All Stars 2025, ambapo aliweza kumaliza katika nafasi ya saba kwa kupata kura 258. Ushiriki wake kwenye shindano hilo ulimuweka karibu zaidi na mashabiki na kumpa jukwaa la kuonesha kipaji chake.

Katika shindano hilo, aliingia na wimbo wake unaojulikana kama “Ndakukunda”, ambao ulimtambulisha rasmi kwa hadhira pana zaidi. Wimbo huo ulionyesha uwezo wake katika kuunganisha ladha ya muziki wa mapenzi na vionjo vya kisasa vinavyovutia kizazi cha sasa.

Kauli yake ya hivi karibuni inaonekana pia kuwa sehemu ya mkakati wa kujitangaza, hasa kwa kuzingatia alivyotumia kauli “#mnyama is coming.”

Je, Hubby analenga kujitofautisha na wengine na kujiweka katika daraja la kipekee? Swali kubwa linalobaki ni kama ataweza kusimama imara na kuthibitisha madai yake kupitia ubora wa kazi zake zijazo. Katika ulimwengu wa muziki, ushindani ni mkali—na mwisho wa yote, muziki mzuri ndio unaozungumza zaidi kuliko maneno. Tusubiri.

Continue Reading

Entertainment

Live Yageuka Vita: Beka Ruga Amvaa Madundo Bila Huruma

Published

on

Mtengeneza maudhui maarufu Beka Ruga amezua mjadala mkali mitandaoni baada ya kumkosoa vikali mchekeshaji Madundo wakati wa “live” aliyofanya pamoja na Bujra saa chache zilizopita.

Akijibu swali la kwa nini hajawahi kushirikiana na Madundo, Ruga hakuficha hisia zake. Alisema wazi kuwa haoni aina ya content ambayo wanaweza kufanya pamoja, akimtaja Madundo kama mtu anayependelea kuvaa nguo chafu na kukimbia mitaani kama sehemu ya burudani yake.

Kauli hiyo haikuishia hapo. Ruga aliendelea kusema kuwa kama angepewa nafasi ya kumbadilisha Madundo, angeanza kwa kumshauri aache kujipaka makaa na aanze kuzingatia usafi wake binafsi. Kwa mujibu wa Ruga, kujipaka makaa kunaweza kuwa na madhara kiafya, akihusisha hata hatari ya saratani.

Aidha, alimkosoa pia kwa kile alichokiita “kujidhalilisha” alipokuwa Tanzania, akidai kuwa Madundo alipiga picha na Gigy Money akiwa amevaa mavazi yasiyofaa hadharani.

Hata hivyo, licha ya ukosoaji huo mkali, Ruga alikanusha kuwa na bifu na Madundo. Alisema wote wanatoka eneo moja (Mkwale) na wana uwezo wa kufanya kazi nzuri pamoja—lakini akasisitiza kuwa Madundo anahitaji kubadilika ili kueleweka zaidi kwenye tasnia.

Sasa swali linabaki: je, huu ni ushauri wa kujenga au ni mashambulizi yaliyovuka mipaka?

Kwa upande mmoja, baadhi ya watu wanaona Ruga kama mtu anayesema ukweli ambao wengi wanaogopa kuusema. Kwa mwingine, wapo wanaoamini kuwa kila msanii ana mtindo wake wa kipekee, na kile kinachoonekana “cha ajabu” kwa mmoja, ndicho kinachomtofautisha na kumuinua mwingine.

Katika ulimwengu wa uundaji maudhui creation, utofauti ndio nguvu. Lakini pia, taswira na namna mtu anavyojiwasilisha vinaweza kuathiri namna anavyopokelewa na fursa anazopata.

Wewe unaonaje—Beka Ruga yuko sahihi au amevuka mipaka?

Continue Reading

Trending