Connect with us

Business

Wawekezaji wakuu nchini waingia katika mkataba wa kiuchumi

Published

on

Benki ya KCB kwa ushirikiano na bebki ya Afrexim zimeingia kwenye mkataba wa maelewano unaolenga kutoa usaidizi wa kuwezesha kifedha na kibiashara kwa wawekezaji wanaoendesha shughuli zao katika eneo la kiuchumi la Vipingo kaunti ya Kilifi.

Chini ya makubaliano hayo benki hizo mbili zitatoa ufadhili wa dola milioni 500 na 300 za marekani mtawalia kwenye mradi huo.

Tangazo hilo lilitolewa wakati wa mkutano uliowaleta pamoja viongozi wa kibiashara mbalimbali na wawekezaji  kujadili jinsi ya kuiweka kenya katika nafasi ya kuwa kivutio kikubwa cha uwekezaji.

Akizungumza katika eneo la Vipingo kaunti ya Kilifi, Mkurungezi wa benki ya KCB Paul Russo alisema kuwa mkataba huo unaashiria hatua muhimu wa ukuaji endelevu wa viwanda nchini kenya na kukuza ufikiaji wa masoko ya kimataifa.

Kulingana na wadau wa sekta ya maswala ya uchumi hatua hiyo itawanufaisha wawekezaji kutokana na shindani ili kuanzisha shughuli zao katika eneo hilo kwa kuzingatia viwanda, mazao kutoka kilimo na biashara za kuongeza thamani.

Taarifa ya Pauline Mwango

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Business

KPA yaimarisha usafirishaji wa makasha na kampeni za kimataifa

Published

on

By

Halmashauri ya bandari nchini (KPA), imeimarisha ushirikiano wake na kampuni ya kimataifa ya usafirishaji kwa njia ya bahari, Maersk, katika juhudi za kuboresha huduma na kuongeza ufanisi wa usafirishaji wa mizigo katika eneo la Afrika Mashariki.

Makubaliano hayo yameafikiwa katika mkutano uliofanyika katika makao makuu ya KPA jijini Mombasa ambapo Mkurugenzi wa Maersk Kanda ya Afrika Mashariki, Tito Okuku, alieleza kuwa kampuni hiyo ina nia ya kupanua shughuli zake zaidi nchini na katika eneo la Afrika Mashariki kwa ujumla.

Moja ya maeneo yatakayopata kipaumbele ni kuimarisha matumizi ya Kituo cha Makontena cha ndani cha Naivasha kinachotazamwa kama kitovu muhimu katika kushughulikia usafirishaji wa mazao ya kilimo kutoka Kenya kwenda masoko ya kimataifa, huku kikitoa njia ya haraka na ya kuaminika kwa wauzaji kufikia masoko ya kimataifa.

Mkurugenzi Mkuu wa KPA, Nahodha William Ruto, alieleza kukubaliana na hatua hiyo akisema ni wakati mwafaka kwa pande zote mbili kuimarisha ushirikiano huo.

Aidha alibainisha kuwa Bandari ya Mombasa pamoja na vituo vyake vya ndani vinaendelea kushuhudia ongezeko la shehena, na akahakikishia kuwa KPA iko tayari kushughulikia mahitaji yanayoongezeka kupitia maboresho ya miundombinu na huduma.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Business

Wakulima wa Mananasi Magarini walilia soko

Published

on

By

Wakulima wa matunda aina ya nanasi katika eneo bunge la Magarini kaunti ya Kilifi wanaitaka serikali kuwatafutia soko ili kuuza bidhaa zao ambazo zinaendelea kuharibika msimu huu.

Kulingana na wakulima hao hakuna soko ambapo wanaweza kuuza bidhaa hizo kwa bei nzuri hali inayofanya wakulima wengi kuuza kwa bei ya chini ili kuepuka kuharibika kwa katunda hayo.

Wakizunumza na cocofm wakulima hao walisema kuwa kwa sasa wanakadiria hasara kwani matunda ni mengi.

Wakati huo huo wakulima hao wameitaka serikali ya kaunti kujenga viwanda.

Ni kauli ambayo imeongwa mkono na wafanyibiashara wa matunda mjini Kilifi kaunti ya Kilifi ambao walisema kuwa matunda mengi msimu huu huharibika kutokana na idadi ndogo ya wateja.

“Serikali itutafutie soko pamoja na kujenga viwanda ili kusaidia wakulima na wafanyibiashara wa matunda aina ya mamanasi, kuuza matunda yao ili kuawaepushia hasara hasa wakati huu ambapo matunda ni mengi.”

Taarifa ya Pauline Mwango

Continue Reading

Trending