Connect with us

Sports

Winga Wa Arsenal Bukayo Saka Kuwa Nje Wiki Nne Kutokana na Jeraha

Published

on

Kilabu ya Arsenal yapata pigo, hii ni baada ya winga Bukayo Saka kutarajiwa kukosa mechi ya Arsenal dhidi ya Liverpool Jumapili pamoja na mechi za kufuzu Kombe la Dunia za England dhidi ya Andorra na Serbia mwezi ujao kutokana na jeraha.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 23 aliumia msuli wa paja katika ushindi wa nyumbani wa Jumamosi dhidi ya Leeds United, na inakadiriwa atakuwa nje kwa muda wa hadi wiki nne.

Nahodha wa Arsenal, Martin Odegaard, pia yuko kwenye shaka ya kucheza mechi ya Anfield kutokana na jeraha la bega alilopata katika ushindi huo dhidi ya Leeds.

Odegaard alionekana kuumwa sana wakati alibadilishwa katika kipindi cha kwanza cha ushindi wa mabao 5-0, na inaelezwa aliondoka Uwanja wa Emirates akiwa na mkono katika kiwiko cha kushikilia bega.

Hata hivyo, mchezaji huyo wa Norway hajathibitishwa kukosa kabisa mechi dhidi ya mabingwa wa Ligi Kuu, na kuna matumaini ndani ya Arsenal kwamba Odegaard mwenye umri wa miaka 26 na Saka hawatakuwa majeruhi wa muda mrefu.

Kuna afueni kubwa zaidi kuhusu Saka, ambaye alikosa miezi mitatu ya msimu uliopita kwa jeraha la msuli wa paja.

Arsenal msimu huu wana kikosi kipana zaidi cha washambuliaji baada ya kumsajili Viktor Gyokeres, Noni Madueke na Eberechi Eze majira ya kiangazi.

Kocha wa Arsenal, Mikel Arteta, pia ana Gabriel Martinelli, Leandro Trossard, Ethan Nwaneri na Max Dowman ili kuziba mapengo ya Saka na Odegaard.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting

Published

on

By

Mshambuliaji Kai Havertz aliifungia Arsenal F.C. bao la ushindi katika dakika za mwisho kabisa, na kuisaidia timu hiyo kuibuka na ushindi mwembamba wa 1-0 dhidi ya Sporting CP katika mechi ya mkondo wa kwanza wa robo fainali ya UEFA Champions League iliyochezwa Jana usiku.

Kikosi cha kocha Mikel Arteta kilifika katika Uwanja wa Estadio Jose Alvalade kikiwa kimeathiriwa na vipigo viwili mfululizo dhidi ya Manchester City F.C. kwenye fainali ya Kombe la Ligi na Southampton F.C. katika robo fainali ya Kombe la FA.

Kwa mara nyingine, Arsenal haikucheza kwa kiwango chake bora, lakini ilifanikiwa kupata ushindi kutokana na uokoaji mzuri wa kipa David Raya pamoja na umakini wa Havertz aliyefunga bao la ushindi katika muda wa nyongeza.

Arsenal sasa ina nafasi kubwa ya kufuzu nusu fainali kabla ya mechi ya marudiano itakayochezwa kaskazini mwa London tarehe 15 Aprili, ingawa italazimika kuboresha kiwango chake ikiwa inataka kushinda taji hilo kwa mara ya kwanza.

Vipigo dhidi ya City na Southampton vilikuwa mara ya kwanza msimu huu kwa Arsenal kupoteza mechi mbili mfululizo, huku kipigo cha Kombe la FA kikiwa cha tano kwao msimu huu.

Athari za matokeo hayo bado zilionekana Lisbon, ambapo Arsenal ilipata ugumu wa kucheza kwa mwendelezo mzuri, lakini kama ilivyokuwa mara kadhaa msimu huu, walipata njia ya kushinda licha ya kutocheza vizuri.

katika mechi nyingine hatua ya robo fainali ni kwamba Bayern Munich waliondoka na ushindi wa magoli 2-1 mikononi mwa Real Madrid katika uwanja wao wa nyumbani Estadio Santiago Bernabeu.

Magoli ya Bayern yakitiwa kimyani na mshmabulizi Luis kipindi cha kwanza naye Erling Haaland kipindi cha pili.

Mechi ya marudiano itachezwa juma lijalo April 15.

Continue Reading

Sports

Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)

Published

on

By

Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.

Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.

SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

Continue Reading

Trending