Business
Biashara ya Viazi Vitamu Yaendelea Kunga’ara Mjini Kilifi Licha ya Changamoto za Usafiri
Kilifi, Kenya – Wachuuzi wa viazi vitamu katika barabara ya mjini Kilifi wameripoti kuimarika kwa biashara hiyo ikilinganishwa na vipindi vya nyuma, wakisema hali hiyo imesababishwa na upatikanaji wa bidhaa hiyo kwa wingi kutoka mashambani.
Akizungumza na wanahabari, Joyce Kemboi, ambaye ni mmoja wa wachuuzi wa viazi vitamu katika eneo hilo, amesema kuwa kwa sasa wakulima wanavuna kwa wingi kutokana na hali nzuri ya mvua ambayo imeimarisha uzalishaji mashambani.
“Kwa sasa viazi vitamu vinapatikana kwa wingi sana, na hii imetuwezesha kufanya biashara nzuri. Wateja pia wameongezeka kwa sababu bidhaa ni safi na za bei nafuu,” amesema Kemboi.
Hata hivyo, licha ya mafanikio hayo, wachuuzi hao wanakabiliwa na changamoto ya gharama ya juu ya usafiri, hali inayochangiwa na kuharibika kwa barabara nyingi kufuatia mvua kubwa inayoendelea kunyesha katika maeneo mengi ya nchi.
Kemboi anasema kuwa usafirishaji wa viazi kutoka mashambani hadi sokoni umekuwa ghali mno, jambo ambalo linaathiri faida ya wachuuzi wa kiwango cha chini.
“Gharama ya kusafirisha gunia moja imepanda. Barabara nyingi zimeharibika, magari hayafiki kwa urahisi, na tunalazimika kutumia njia mbadala ambazo ni ghali,” ameongeza.
Kwa sasa, gunia la kilo 90 la viazi vitamu linauzwa kwa shilingi elfu 10, bei ambayo ni ya juu ikilinganishwa na msimu wa kiangazi ambapo gunia hilo hilo lingeuzwa kwa kati ya shilingi elfu 6 hadi 7.
Licha ya bei hiyo kupanda, wachuuzi wana matumaini kuwa soko litaendelea kuboreka hasa kwa kuwa bidhaa hiyo ina uhitaji mkubwa kwa wateja wa kila tabaka.
Business
Wafanyibiashara wa mitumba eneo la Diani wafunga biashara zao
Wafanyibiashara wa mitumba katika soko la Diani, kaunti ya Kwale, wamelazimika kufunga biashara zao kutokana na kudorora kwa shughuli za kibiashara katika kipindi hiki cha msimu wa watalii wachache na mvua zinazoendelea kushuhudiwa katika eneo hilo.
Wafanyabiashara hao wanasema idadi ya wanunuzi imepungua kwa kiasi kikubwa, hali iliyosababisha nguo nyingi kukosa soko.
Kulingana na wafanyibiashara hao wanategemea zaidi watalii wa ndani na nje na kutokana na msimu huu kuwa uko uko chini wateja wamepungua hali inayofanya maisha kuwa mgumu.
Wanasema wamelazimika kutupa baadhi ya nguo kwani zimesalia sokoni kwa muda mrefu hadi zingingine kuharibika, jambo ambalo limepelekea kupata hasara kubwa.
Aidha, wameongeza kuwa bei ya nguo za mitumba imeendelea kupanda ambapo wananunua ngunia moja kwa shilingi elfu 40 huku mauzo yakizidi kushuka.
“ Biashara imedorora sai kwani hakuna wateja ikizingatiwa kuwa tunategemea sana watalii na sasa hakuna wageni hata imetulazimu kutupa nguo kwani ngigi zimeharibika baada ya kukaa kwa mda mrefu bila kununuliwa”.
Taarifa ya Pauline Mwango
Business
Mamlaka ya AFA yahimiza upanzi wa mkorosho
Mamlaka ya Kilimo na Chakula nchini AFA, imekuwa mstari wa mbele kuhakikisha taifa linaboresha mazao yake na kuchangia uzalishaji wa chakula nchini.
Hatua hii imechangia zaidi na mikakati endelevu ya kuwawezesha wakulima kufahamu mipango endelevu ya uimarishaji wa Kilimo cha sasa na kwa kuzingatia utumiaji wa mifumo bora ya kilimo.
Mamlaka hiyo ambapo inaendeleza kampeni ya kuhamisha wakulima kuhusu umuhimu wa kilimo cha Korosho imesisitiza haja ya ujumuishaji wa wakulima, wawekezaji na wadau mbalimbali ili kupiga jeki sekta ya Kilimo huku ikiahidi kuendeleza hamasa kwa jamii za kaunti za Pwani kuhusu kilimo cha korosho na utafutaji wa soko huru.
Katika Kongamano la kitaifa lililoandaliwa katika kaunti ya Kwale, Mamlaka hiyo iliwapa wakulima kutoka kaunti sita za Pwani miche ya mikorosho elfu mia moja katika juhudi za kukuza kilimo cha zao hilo nchini.
Katibu katika Idara ya Kilimo nchini Paul Kiprono, alisema mpango huo unalenga kuwawezesha wakulima kuongeza uzalishaji wa korosho na kuchangia ukuaji wa uchumi wa taifa.
Akizungumza wakati wa ufunguzi wa kongamano hilo, Kiprono alitoa wito kwa serikali za kaunti pamoja na wadau wa sekta ya kilimo kushirikiana kwa karibu ili kuboresha kilimo cha korosho.
“Kenya ilikuwa ikiongoza katika zao la mkorosho katika miaka ya 1990 lakini kutokana na changamoto za kibiashara zao hilo lilishuka katika masoko ya kimataifa kutokana na ukosefu wa kuwekezaji kwa wakulima lakini sasa tumeanza kupiga hatua kwani tunazalisha zaidi ya tan elfu 9 za korosho”, alisema Rono.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa AFA, Cornelly Serem, alisema mamlaka hiyo imejizatiti kuboresha kilimo cha korosho kupitia utoaji wa miche bora na mafunzo kwa wakulima ili kuongeza tija.
Taarifa ya Mwanahabari wetu

