Connect with us

News

Erastus Edung Ethekon Aapishwa Kuwa Mwenyekiti Mpya wa Tume Ya IEBC

Published

on

Wenyekiti mpya wa Tume ya uchaguzi na mipaka Erastus Ethekon pamoja na makamishena wengine sita wa Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC), wameapishwa leo Ijumaa Julai 11 katika jengo la Mahakama ya upeo.

Mwenyekiti huyo sasa atawaongoza makamishena wengine, Ann Nderitu, Moses Mukhwana, Mary Sorobit, Hassan Noor, Francis Adoul, na Fahima Abdallah kuhudumu katika time hiyo.

Awali zoezi la kuwapishwa makamishena hao, lilikuwa limesimamishwa kufuatia agizo la Mahakama kuu, iliyotaja ukiukwaji mkubwa wakati wa mchakato wa kuwateua makamishena hao.

Hata hivyo agizo hilo sasa limeondolewa na majina ya makamishena hao kuchapishwa upya katika gazeti rasmi la serikali hapo Jana Julai 10 2025.

Mnamo Julai 10 2025, Mahakama kuu ilikuwa imebatlisha uteuzi uliofanywa na Rais William Ruto wa Makamishena hao saba wa tume ya uchaguzi na mipaka (IEBC), akiwemo mwenyekiti wake Erastus Ethekon.

Hata hivyo katika uamuzi huo, Mahakama ilimpa nafasi Rais William Ruto kuhalalisha uteuzi wa makamishena hao kwa kuondolewa mbali kwa agizo hilo la awali lililozuia kuchapishwa kwa majina ya makamishena hao katika gazeti rasmi la serikali kabla ya kula kiapo.

Katika uamuzi wao siku ya Alhamisi Julai 10 2025, majaji wa Mahakama hiyo Roseline Amburili, Jaji Bahati Mwamuye na John Chigiti, walisema kwamba Rais alipasa kuheshimu maagizo hayo ya Mahakama kwani si mapendekezo tu, bali yalikuwa na msingi wa kisheria na kuapishwa kwa Makamishena hao ungekuwa kinyume Cha Sheria, na kuwatoa imani Wakenya kwa Tume hiyo.

Tume hiyo sasa inajukumu kubwa la kushughulikia masuala nyeti yaliyokuwa yamekwama tangu kuvunjwa kwa tume iliyokuwa iliongozwa na Wafula Chebukati.

Miongoni mwayo ni chaguzi ndogo katika sehemu mbali mbali za uakilishi Wadi na Ubunge likiwemo eneo Bunge la Magarini Kaunti ya Kilifi.

Pia kuna suala la kusafisha sajili ya wapiga kura pamoja na kuchunguzwa upya kwa mipaka ya maeneo ya kiwakilishi kabla ya uchaguzi mkuu ujao wa 2027.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Ethekon: Uchaguzi mkuu utakuwa huru, haki na uwazi

Published

on

By

Tume huru ya uchaguzi na mipaka nchini IEBC imeanza rasmi zoezi la kuwasajili wapiga kura wapya kote nchini, huku ikilenga kuwasajili wapiga kura milioni 6.2, kabla ya uchaguzi mkuu ujao. 

Mwenyekiti wa Tume hiyo Erastus Ethekon aliwahakikishia wakenya kwamba makamishna wa tume hiyo watahakikisha uchuguzi mkuu ujao unakuwa huru, haki na uwazi.

Akizungumza katika kaunti ya Kwale wakati wa kuzindua wa zoezi la usajili wa wakipiga kura kote nchini, Ethekon alisema serikali imewekeza raslimali za kutosha za kufanikisha zoezi hilo.

“Nataka kuwahakikishia wakenya kwamba tumejipanga kama IEBC na tuko na raslimali za kutosha kuhakikisha zoezi la usajili wa wapiga kura linaendeshwa vyema na uchaguzi mkuu utakuwa huru, haki na wazi ili kuhakikisha wakenya wanatekeleza jukumu lao la kidemokrasia na hatua hiyo tutafikia idadi ya wapiga kura zaidi ya milioni 27”, alisema Ethekon.

Naye Naibu Mwenyekiti wa IEBC Fahima Araphat alisema tayari maafisa wapya wa IEBC elfu 12 wameajiriwa kuhakikisha zoezi hilo liendeshwa vyema ili kusajili idadi kubwa ya wapiga kura

“Sisi tunafanya kazi yetu bila kuegemea upande wowote wa kisiasa na tuko tayari kuhakikisha anashinda uchaguzi anatangazwa mshindi kwa haki, na kama tuko na makarani elfu 12 na wote wasajili wapiga kura wapya elfu 10 kila moja tutakuwa na idadi kubwa ya wapiga kura, sasa hiyo ndio tunalenga kupata”, alisema Fahima.

Kwa upande wake Gavana wa kaunti ya Kwale Fatuma Achani, aliipongeza tume hiyo kwa zoezi hilo endelevu la wapiga kura, akisema ni hatua ya kipekee kwa jamii ambazo zimekosa fursa ya kujisajili kama wapiga kura.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

News

IEBC yasema idadi ya wanaojisajili ni ndogo mno

Published

on

By

Zoezi endelevu la usajili wa wapiga kura kote nchini limeng’oa nanga huku maafisa wa Tume huru ya uchaguzi na mipaka nchini IEBC wakilenga idadi kubwa ya vijana katika zoezi hilo.

Katika kaunti ya Kilifi eneo bunge la Kilifi Kazkazini, zoezi hilo limefanyika katika vituo vinne tofauti huku idadi ndogo ya wapiga kura ikishuhudiwa licha ya vuguvugu la TUKO KADI kuanzishwa na vijana ili kuwajisajili wapiga kura.

Akizungumza na Wanahabari wakati wa zoezi hilo, Naibu Afisa wa usajili wa wapiga kura katika eneo bunge la Kilifi Kazkazini Abdul Mohammed aliwarai vijana kujitokeza kwa wingi na kujisajili.

Mohammed pia aliwarai vijana kukoma kutumiwa vibaya na wanasiasa kwa manufaa yao binafsi, akipongeza vuguvugu lilionzishwa na vijana la TUKO KADI kama njia moja ya kuwahamasisha vijana kujisajili kama wapiga kura.

“Tumeanza zoezi hili na tunawahimiza vijana wajitokeze kwa wingi na kujisajili kama wapiga kura ili kutumia nafasi hiyo kuchagua viongozi wanawataka na wala wasikubali kutumiwa vibaya na wanasiasa”, alisema Mohammed.

Kwa upande wao baadhi ya vijana waliojisajili waliwarai vijana wenzao kujitokeza kwa wingi na kushiriki zoezi hilo ili kuchagua viongozi wanaohisi wataleta maendeleo sawa na kubuni nafasi za ajira.

Taarifa ya Elizabeth Mwende

Continue Reading

Trending