Connect with us

News

Erastus Edung Ethekon Aapishwa Kuwa Mwenyekiti Mpya wa Tume Ya IEBC

Published

on

Wenyekiti mpya wa Tume ya uchaguzi na mipaka Erastus Ethekon pamoja na makamishena wengine sita wa Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC), wameapishwa leo Ijumaa Julai 11 katika jengo la Mahakama ya upeo.

Mwenyekiti huyo sasa atawaongoza makamishena wengine, Ann Nderitu, Moses Mukhwana, Mary Sorobit, Hassan Noor, Francis Adoul, na Fahima Abdallah kuhudumu katika time hiyo.

Awali zoezi la kuwapishwa makamishena hao, lilikuwa limesimamishwa kufuatia agizo la Mahakama kuu, iliyotaja ukiukwaji mkubwa wakati wa mchakato wa kuwateua makamishena hao.

Hata hivyo agizo hilo sasa limeondolewa na majina ya makamishena hao kuchapishwa upya katika gazeti rasmi la serikali hapo Jana Julai 10 2025.

Mnamo Julai 10 2025, Mahakama kuu ilikuwa imebatlisha uteuzi uliofanywa na Rais William Ruto wa Makamishena hao saba wa tume ya uchaguzi na mipaka (IEBC), akiwemo mwenyekiti wake Erastus Ethekon.

Hata hivyo katika uamuzi huo, Mahakama ilimpa nafasi Rais William Ruto kuhalalisha uteuzi wa makamishena hao kwa kuondolewa mbali kwa agizo hilo la awali lililozuia kuchapishwa kwa majina ya makamishena hao katika gazeti rasmi la serikali kabla ya kula kiapo.

Katika uamuzi wao siku ya Alhamisi Julai 10 2025, majaji wa Mahakama hiyo Roseline Amburili, Jaji Bahati Mwamuye na John Chigiti, walisema kwamba Rais alipasa kuheshimu maagizo hayo ya Mahakama kwani si mapendekezo tu, bali yalikuwa na msingi wa kisheria na kuapishwa kwa Makamishena hao ungekuwa kinyume Cha Sheria, na kuwatoa imani Wakenya kwa Tume hiyo.

Tume hiyo sasa inajukumu kubwa la kushughulikia masuala nyeti yaliyokuwa yamekwama tangu kuvunjwa kwa tume iliyokuwa iliongozwa na Wafula Chebukati.

Miongoni mwayo ni chaguzi ndogo katika sehemu mbali mbali za uakilishi Wadi na Ubunge likiwemo eneo Bunge la Magarini Kaunti ya Kilifi.

Pia kuna suala la kusafisha sajili ya wapiga kura pamoja na kuchunguzwa upya kwa mipaka ya maeneo ya kiwakilishi kabla ya uchaguzi mkuu ujao wa 2027.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Aisha Jumwa akihama rasmi chama cha UDA

Published

on

By

Mgombea wa kiti cha ugavana wa kaunti ya Kilifi Aisha Jumwa amekihama rasmi chama cha UDA, akisema atatangaza baadaye mwelekeo atakaochukua wa kisiasa.

Jumwa alitoa tangazo hilo katika kikao na Wanahabari kilichofanyika katika makaazi yake, eneo la Kakuyuni huko Malindi kaunti ya Kilifi leo siku ya Alhamis.

Hatua ya Jumwa ilijiri baada ya kuwepo na tetesi kwamba alikuwa na mipango ya kuhama chama hicho kutokana na sintofahamu za kisiasa ndani ya chama cha UDA kuhusu msimamo wake wa kisiasa wa kuwania nafasi ya ugavana wa Kilifi.

Jumwa alilalamika kwamba alikuwa akinyanyaswa na baadhi ya viongozi hata kutimuliwa katika Ikulu ya rais licha ya kupambana katika kampeni za rais Ruto mwaka wa 2022, akionekana kumlaumu rais Ruto kwa kutomjali tena hata baada ya kusimama na yeye kisiasa.

Kiongozi huyo alikashfu vikali kutengwa katika mikutano ya UDA licha ya kuwa mwandani wa rais Ruto na pamoja na kufanyikisha miradi ya serikali mashinani, akisema tangu atangaze mchakato wa kuwania kiti cha ugavana wa Kilifi mwaka wa 2027, amekuwa akipitia masaibu mengi.

Hii sio mara ya kwanza kwa Jumwa kukihama Chama cha UDA na kurejea kwenye chama hicho, lakini hatua aliyoichukua sasa itabadili masimamo wa kisiasa kaunti ya Kilifi.

Itakumbukwa kwamba Jumwa amekuwa mwandani wa karibu wa rais William Ruto, lakini hatua aliyoichukua huenda ikabadili msimamo wa kisiasa kaunti ya Kilifi na Pwani kwa jumla. 

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

News

Mahakama ya Kilifi yaagiza kuzuiliwa Washukiwa 7 wa mauaji

Published

on

By

Mahakama ya Kilifi imeagiza kuzuiliwa kwa siku 14 washukiwa 7 wanaotuhmiwa kuhusika katika kifo cha mwanamke mmoja aliyekuwa na umri wa miaka 65, ambaye aliuwawa kwa tuhma za uchawi katika eneo la Malomani eneo bunge la Ganze kaunti ya Kilifi.

Washukiwa hao Gilbert Karisa Changawa, Selvestar Changawa Kahindi, Elizabeth Jackson Ngala, Dhahabu Kithi Kombe, Dzendere Palu Kalama, Agness Changawa na Kadzo Ngombo Bienge watazuiliwa katika kituo cha Bamba wakati uchunguzi ukiendelea.

Kulingana na Afisa mpelelezi kutoka kitengo cha DCI ameeleza mahakama kwamba ilikuwa mnamo tarehe 27 mwezi huu ambapo walipokea tarifa kwamba dama changawa alikuwa amekatwa kichwa na kuuwawa na watu wasiojulikana usiku huo.

Afisa mpelelezi pia ameeleza kuwa washukiwa ambao ni wanafamilia,siku kabla ya tukio husika walikuwa wameandaa kikao cha kudumisha Amani baada ya kifo kilichokuwa kimetokea kwa kijana mmoja mtoto wa mmoja kati ya washukiwa aliyefariki kaunti ya Mombasa baada ya kupigwa kwa tuhma za wizi.

Kutokana na kifo cha kijana huyo wanafamilia hao walimtuhmu dama kwamba ndiye aliyekuwa amemroga kijana huyo na kusababisha kifo hicho cha gafla, ambapo usiku huo Dama aliuwawa nyumbani kwake.

Washukiwa watarudishwa mahakamani tarehe 13 mwezi Agosti mwaka huu baada ya uchunguzi kukamilika.

Taarifa ya Teclar Yeri

Continue Reading

Trending