Connect with us

News

Ethekon: Tutaandaa uchaguzi huru na haki, 2027

Published

on

Tume huru ya uchaguzi na mipaka nchini IEBC imewahakikishia wakenya kwamba itafanikisha uchaguzi huru na haki ifikapo mwaka wa 2027.

Kulingana na Mwenyekiti wa Tume hiyo, Erastus Ethekon, IEBC iko tayari kutekeleza majukumu yake ya kikatiba, ikiwemo usajili wa wapiga kura, kuendesha uchaguzi, pamoja na kugawaa mipaka ya maeneo ya uwakilishi.

Akizungumza mjini Mombasa tangu kuapishwa kwake kushikilia wadhfa ya Mwenyekiti wa IEBC, Ethekon alisema IEBC itaharakisha mchakato wa kuandaa chaguzi ndogo 23 kote nchini ikiwemo nafasi moja ya Seneta, nafasi 6 za ubunge na nafasi 16 za uwakilishi wadi.

Ethekon alisema nafasi hizo za viongozi ziliachwa wazi baada ya baadhi ya viongozi kupoteza maisha yao huku wengine viti vya vikasalia wazi baada ya matokeo ya chaguzi hizo kubatilishwa na Mahakama.

Wakati huo huo aliwataka wanasiasa kujiepusha na matamshi yanayoashiria uwepo wa njama za wizi wa kura katika uchaguzi mkuu ujao, akisema kauli hizo zinatia doa utendakazi wa tume ya IEBC huku akilitaka bunge la kitaifa pamoja na Wizara ya Fedha nchini kuhakikisha tume hiyo inapokea mgao wa fedha kwa wakati.

Ethekon alisisitiza kuwa tume hiyo iko imara na haitashuhudia migawanyiko kama ilivyoshuhudiwa katika vipindi vilivyopita.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Polisi wanachunguza tukio la wizi dhidi ya raia wa kigeni

Published

on

By

Maafisa wa Polisi kaunti ya Mombasa wanachunguza tukio la wizi dhidi ya mtalii wa kigeni lililotokea katika eneo la Nyali

Kulingana na ripoti ya maafisa wa polisi, mtalii huyo mwenye umri wa miaka 51 ambaye ni raia wa Marekani, anadai kulaghaiwa na kisha kushambuliwa na kundi la wanaume aliyokutana nao muda mfupi kabla ya tukio.

Ripoti hiyo imeeleza kwamba mnamo mwezi Aprili 9 mwaka huu, raia huyo wa kigeni akiwa katika mkahawa mmoja eneo la Nyali jijini Mombasa, alikutana na mwanaume aliyejitambulisha kama Alex, ambaye alimshawishi kuelekea katika nyumba ya Airbnb iliyoko karibu na mkahawa huo.

Taarifa hiyo ilifafanua zaidi kwamba alipofika katika chumba hicho, alikumbana na wanaume wengine watano waliokuwa wakimsubiri ambapo mlango ulifungwa na kisha akashambuliwa na kulazimishwa kutoa pesa na vitu vya thamani.

Wahalifu hao walitoroka na mali mbalimbali ikiwemo simu ya rununu, kompyuta mpakato (laptop), fedha taslimu pamoja na fedha za kigeni na pia walifanikiwa kutoa pesa kutoka kwenye kadi zake za benki kwa njia ya udanganyifu.

Maafisa wa polisi kutoka Bamburi kwa kushirikiana na maafisa wa upelelezi wa DCI Nyali walifika eneo la tukio na kuanza uchunguzi, ingawa hadi sasa hakuna mtu aliyekamatwa wala mali iliyopatikana.

Kesi hiyo imewekwa chini ya uchunguzi zaidi huku juhudi zikiendelea kuwabaini na kuwakamata wahusika wa tukio hilo.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

News

Polisi eneo la Likoni-Mombasa inachunguza kifo cha mwanamke

Published

on

By

Idara ya usalama eneo la Likoni kaunti ya Mombasa imesema inachunguza kifo cha mwanamke mmoja aliyefariki katika mtaa wa senti kumi.

Mkuu wa polisi wa Likoni Joseph Mutungi alisema mwanamke huyo anadaiwa kupoteza maisha wakati wakiwa nyumbani kwa mwanamme anayesemekana kuwa mchumba wake.

Taarifa za awali ziliarifu kuwa marehemu alikuwa mgonjwa na anadaiwa alifika hospitalini kusaka matibabu japo hakupata huduma na kurejea nyumbani bila kutibiwa.

Inasemekana baadaye mchumba wake alioondoka kwenda kazini na kumwacha chini ya uangalizi wa mwanamke mwengine katika ploti hiyo.

Hali yake inadaiwa kuzorota na hatimaye kuaga dunia.

Maafisa wa usalama walisema wanaendelea na uchunguzi kubaini chanzo cha kifo hicho.

Mwili wa marehemu unahifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti katika hospitali ya Coast general kwa uchunguzi zaidi.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Trending