Connect with us

News

Boniface Mwangi akamatwa na maafisa wa DCI

Published

on

Mwanaharakati wa kutetea haki za kibinadamu nchini Boniface Mwangi amekamatwa na maafisa wa idara ya upelelezi wa jinai nchini DCI. 

Kulingana na Mkewe Boniface, Hellen Njeri Mwangi, Mumewe amekamatwa nyumbani wako katika eneo la Lukenya kaunti ya Machokos na maafisa waliojitambulisha kwamba wanatoka katika Idara ya DCI.

Hellen alisema Boniface amepelekwa katika makao makuu ya idara ya DCI jijini Nairobi huku sababu za kukamatwa kwa Boniface zikihusisha na masuala ya ugaidi.

Kulingana na Wakili wa Boniface, James Kamau alisema maafisa wa DCI walivamia makaazi ya mteja wake wakiwa wamejihami kwa silaha na kumtia nguvuni.

Hatua hii imejiri baada ya Boniface na Mwanaharakati kutoka Uganda Agather Utuhaire mnamo siku ya Ijumaa Julai 18, 2025 kuwasilisha kesi katika Mahakama ya Afrika Mashariki na kulishtaki taifa la Tanzania kwa madai kwamba maafisa wa serikali ya Tanzania walikiuka haki zao za kibinadamu.

Kwenye mashtaka hayo, Wanaharakati hao walidai kutekwa nyara na watu wasiojulikana wakiwa jijini Dar er Salam pamoja na vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia na kutupwa nje ya mpaka wa Tanzania, Uganda na Kenya, mtawalia.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Polisi wanachunguza tukio la wizi dhidi ya raia wa kigeni

Published

on

By

Maafisa wa Polisi kaunti ya Mombasa wanachunguza tukio la wizi dhidi ya mtalii wa kigeni lililotokea katika eneo la Nyali

Kulingana na ripoti ya maafisa wa polisi, mtalii huyo mwenye umri wa miaka 51 ambaye ni raia wa Marekani, anadai kulaghaiwa na kisha kushambuliwa na kundi la wanaume aliyokutana nao muda mfupi kabla ya tukio.

Ripoti hiyo imeeleza kwamba mnamo mwezi Aprili 9 mwaka huu, raia huyo wa kigeni akiwa katika mkahawa mmoja eneo la Nyali jijini Mombasa, alikutana na mwanaume aliyejitambulisha kama Alex, ambaye alimshawishi kuelekea katika nyumba ya Airbnb iliyoko karibu na mkahawa huo.

Taarifa hiyo ilifafanua zaidi kwamba alipofika katika chumba hicho, alikumbana na wanaume wengine watano waliokuwa wakimsubiri ambapo mlango ulifungwa na kisha akashambuliwa na kulazimishwa kutoa pesa na vitu vya thamani.

Wahalifu hao walitoroka na mali mbalimbali ikiwemo simu ya rununu, kompyuta mpakato (laptop), fedha taslimu pamoja na fedha za kigeni na pia walifanikiwa kutoa pesa kutoka kwenye kadi zake za benki kwa njia ya udanganyifu.

Maafisa wa polisi kutoka Bamburi kwa kushirikiana na maafisa wa upelelezi wa DCI Nyali walifika eneo la tukio na kuanza uchunguzi, ingawa hadi sasa hakuna mtu aliyekamatwa wala mali iliyopatikana.

Kesi hiyo imewekwa chini ya uchunguzi zaidi huku juhudi zikiendelea kuwabaini na kuwakamata wahusika wa tukio hilo.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

News

Polisi eneo la Likoni-Mombasa inachunguza kifo cha mwanamke

Published

on

By

Idara ya usalama eneo la Likoni kaunti ya Mombasa imesema inachunguza kifo cha mwanamke mmoja aliyefariki katika mtaa wa senti kumi.

Mkuu wa polisi wa Likoni Joseph Mutungi alisema mwanamke huyo anadaiwa kupoteza maisha wakati wakiwa nyumbani kwa mwanamme anayesemekana kuwa mchumba wake.

Taarifa za awali ziliarifu kuwa marehemu alikuwa mgonjwa na anadaiwa alifika hospitalini kusaka matibabu japo hakupata huduma na kurejea nyumbani bila kutibiwa.

Inasemekana baadaye mchumba wake alioondoka kwenda kazini na kumwacha chini ya uangalizi wa mwanamke mwengine katika ploti hiyo.

Hali yake inadaiwa kuzorota na hatimaye kuaga dunia.

Maafisa wa usalama walisema wanaendelea na uchunguzi kubaini chanzo cha kifo hicho.

Mwili wa marehemu unahifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti katika hospitali ya Coast general kwa uchunguzi zaidi.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Trending