Sports
Fikirini Jacobs- Benni Mccarthy Ni Sahihi Harambee Stars
Katibu katika Wizara Kuu ya Kitaifa Inayosimamia Maswala ya Vijana na Uchumi Bunifu Fikirini Jacobs amesifia hatua ya Shirikisho la soka nchini FKF na serikali kupitia kwa Wizara ya Michezo kumteua Benni Mccarthy kuwa kocha mkuu wa timu ya soka wanaume Harambee Stars.
Kwa mujibu wa Katibu huyo hatua hiyo ni ishara tosha ya kufufuka kwa mchezo huo nchini baada ya ukimya wa muda mrefu kwenye timu hiyo.
“Nichukue Fursa Hii kuwapongeza Wizara ya Michezo ambapo yuko mwenzangu Elijah Mwangi sitaki nizungumz mengi lakini hata hatua ya Taifa La Kenya kumchukua Benni Mccarthy aliyekua kocha Manchester United kuwa kocha wa Harambee Stars ni hatua ya kufufua timu hiyo pamoja na The Lost Glory ,kwa sababu kihistoria mimi ni mtu nimekaa na watu wengi akiwemo mzee wetu The RT HON.Raila Amollo Odinga na aliwahi kuniambia hapa kenya mpira ulikua mkubwa mno kuliko magharibi na hata Afrika Kusini.”
Katibu huyo aliyasema hayo katika fainali ya mashindano ya kaunti ya shule za Upili katika shule ya Upili ya kilifi towship.
Entertainment
Arsenal Ikishinda Kombe Nitampa Main Man Rio Gari na Dadangu – Shuga Boy
Mjadala mkali umeibuka katika kipindi cha COCO Asubuhi baada ya Shuga Boy, shabiki wa Manchester United, kuweka dau zito na la kushangaza dhidi ya Main Man Rio ambaye ni shabiki wa Arsenal.
Akizungumza kwenye kipindi cha COCO Asubuhi, kinachoendeshwa na Tatu Sure—inayojumuisha Shuga Boy mwenyewe, Main Man Rio na Solomon Zully—Shuga Boy alifunguka, akidai kuwa Arsenal hawana uwezo wa kubeba hata kombe moja msimu huu licha ya matarajio makubwa kutoka kwa mashabiki wao.
Kwa mujibu wa Shuga Boy, mashabiki wa Arsenal wamekuwa wakijipa matumaini makubwa ya kutwaa hadi vikombe vinne, lakini hali halisi uwanjani haioneshi dalili hizo. Alienda mbali zaidi na kuweka dau la kipekee kwa Main Man Rio, ambaye ni shabiki mkubwa wa Arsenal.
“Nilimwambia Main Man Rio, wakibeba kombe nitampa gari yangu. Sasa naongeza dau—wakishinda kikombe msimu huu, nitampa gari yangu pamoja na dadangu,” alisema Shuga Boy kwa msisitizo, kauli iliyozua kicheko na mjadala mkali studio.
Kauli hiyo imekuja katika kipindi ambacho Arsenal wamekuwa wakionyesha ushindani mkubwa chini ya kocha Mikel Arteta, wakijijenga kama moja ya timu zinazowania ubingwa wa Premier League. Licha ya maendeleo hayo, ukosefu wa vikombe katika misimu mingi bado unawapa wapinzani wao nafasi ya kuwabeza.
Kwa upande mwingine, Manchester United nao wanapitia kipindi cha mabadiliko, wakijaribu kurejea kwenye ubora wao wa zamani waliouonyesha enzi za Sir Alex Ferguson. Licha ya changamoto, bado wana historia nzito ya mafanikio, jambo linalowapa mashabiki wao kujiamini wanapojadili soka la Uingereza.
Usiku wa leo, macho ya mashabiki yataelekezwa kwenye mchezo wa ligi kati ya Manchester United dhidi ya Leeds United—mchezo unaotarajiwa kuwa na ushindani mkali, huku Shuga Boy akitumaini timu yake itapata ushindi na kuendeleza presha kwa wapinzani wao.
Wakati mabishano yakiendelea mitandaoni na kwenye studio za redio, swali kubwa linabaki: Je, Arsenal wataweza kuwanyamazisha wakosoaji wao kwa kubeba angalau kombe moja msimu huu, au kauli ya Shuga Boy itageuka kuwa unabii?

