Connect with us

News

Idara ya Usalama Yalaumiwa kwa Kukosa Kuhamia Mfumo wa Kidijitali

Published

on

Idara ya Usalama nchini imelaumiwa kwa kushindwa kuzihamisha huduma zake hadi katika mfumo wa kidijitali hali ambayo imerudisha nyuma juhudi za kutafuta usaidizi wa kiusalama.

Kulingana na Wanaharakati wa kijamii, licha ya taifa kupiga hatua katika kuhakikisha haki inapatikana kwa washukiwa na wale wanaofika Mahakamani bado idara hiyo imesalia nyuma kiteknolojia.

Wanaharakati hao wakiongozwa na Victor Kaudo, wamelaumu mfumo wa zamani unaotumika na maafisa wa usalama katika kunakili na kuweka rekodi za kesi mbalimbali zinazowasilishwa katika vituo vya polisi, wakidai kwamba mfumo huo unachelewesha kesi Mahakamani.

“The next Place ambayo tunahitaji zaidi iende digital ni National Police service ili zile faili pale ziwe zinafanywa haraka haraka ndio tukienda pale katika Gender base tuache kuwa frastrated and alot of paper work. Wakifanya kazi zote kuwa katika mtandao tutakuwa tunafanya kazi zetu kwa urahisi”, alisema Kaudo.

Hata hivyo mwaka wa 2019, Idara ya usalama nchini ilianzisha mchakato wa kuweka rekodi za kesi wanazopokea katika mfumo wa kidijitali lakini mpango huo ilikosa kufaulu na kuwarejesha katika mfumo wa zamani wa kutumia vitabu kunakili kesi.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Polisi wanachunguza tukio la wizi dhidi ya raia wa kigeni

Published

on

By

Maafisa wa Polisi kaunti ya Mombasa wanachunguza tukio la wizi dhidi ya mtalii wa kigeni lililotokea katika eneo la Nyali

Kulingana na ripoti ya maafisa wa polisi, mtalii huyo mwenye umri wa miaka 51 ambaye ni raia wa Marekani, anadai kulaghaiwa na kisha kushambuliwa na kundi la wanaume aliyokutana nao muda mfupi kabla ya tukio.

Ripoti hiyo imeeleza kwamba mnamo mwezi Aprili 9 mwaka huu, raia huyo wa kigeni akiwa katika mkahawa mmoja eneo la Nyali jijini Mombasa, alikutana na mwanaume aliyejitambulisha kama Alex, ambaye alimshawishi kuelekea katika nyumba ya Airbnb iliyoko karibu na mkahawa huo.

Taarifa hiyo ilifafanua zaidi kwamba alipofika katika chumba hicho, alikumbana na wanaume wengine watano waliokuwa wakimsubiri ambapo mlango ulifungwa na kisha akashambuliwa na kulazimishwa kutoa pesa na vitu vya thamani.

Wahalifu hao walitoroka na mali mbalimbali ikiwemo simu ya rununu, kompyuta mpakato (laptop), fedha taslimu pamoja na fedha za kigeni na pia walifanikiwa kutoa pesa kutoka kwenye kadi zake za benki kwa njia ya udanganyifu.

Maafisa wa polisi kutoka Bamburi kwa kushirikiana na maafisa wa upelelezi wa DCI Nyali walifika eneo la tukio na kuanza uchunguzi, ingawa hadi sasa hakuna mtu aliyekamatwa wala mali iliyopatikana.

Kesi hiyo imewekwa chini ya uchunguzi zaidi huku juhudi zikiendelea kuwabaini na kuwakamata wahusika wa tukio hilo.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

News

Polisi eneo la Likoni-Mombasa inachunguza kifo cha mwanamke

Published

on

By

Idara ya usalama eneo la Likoni kaunti ya Mombasa imesema inachunguza kifo cha mwanamke mmoja aliyefariki katika mtaa wa senti kumi.

Mkuu wa polisi wa Likoni Joseph Mutungi alisema mwanamke huyo anadaiwa kupoteza maisha wakati wakiwa nyumbani kwa mwanamme anayesemekana kuwa mchumba wake.

Taarifa za awali ziliarifu kuwa marehemu alikuwa mgonjwa na anadaiwa alifika hospitalini kusaka matibabu japo hakupata huduma na kurejea nyumbani bila kutibiwa.

Inasemekana baadaye mchumba wake alioondoka kwenda kazini na kumwacha chini ya uangalizi wa mwanamke mwengine katika ploti hiyo.

Hali yake inadaiwa kuzorota na hatimaye kuaga dunia.

Maafisa wa usalama walisema wanaendelea na uchunguzi kubaini chanzo cha kifo hicho.

Mwili wa marehemu unahifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti katika hospitali ya Coast general kwa uchunguzi zaidi.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Trending