Connect with us

Business

Kanda ya Pwani kuimarika kupitia Kilimo cha kisasa

Published

on

Kanda ya Pwani inatarajiwa kuimarika zaidi kupitia Kilimo cha kisasa kinachotekelezwa kupitia mfumo wa teknolojia.

Hii ni kupitia mikakati inayoendelezwa na Agitech Seedlings kuhakikisha Wakulima na Wenyeji wa Kanda ya Pwani wanakumbatia Kilimo cha kisasa kama maeneo mengine nchini.

Akizungumza na Coco FM katika maonyesho ya Kilimo cha kisasa na uzinduzi wa tawi jipya la Agitech Seedling katika eneo la Kwa Ndomo mjini Malindi kaunti ya Kilifi, Mkurugenzi wa Agitech Seedlings Peter Karanja Ndung’u alieleza sababu za kuanzisha Kilimo hicho cha kisasa katika ukanda wa Pwani.

Karanja pia alisema wanapania kuhakikisha wenyeji wa Pwani wanahamasishwa ipasavyo na hata kuonyeshwa namna ya kufanya Kilimo hicho hapa pwani.

“Kupitia hamasa ambazo tunatoa kwa wakulima na wenyeji wa Pwani kwa jumla tunatarajia kuwa Kilimo kitaanza kuimarika na kuondoa dhana ambayo imekuwepo kwamba eneo la Pwani linatambulika pekee kwa masuala ya uvuvi’’, alisema Karanja.

Vilevile, Karanja alisema kuna haja ya Wakulima kutunza ardhi zao kwa kuhakikisha zina rutuba ya kutosha ili kuzalisha chakula kwa wingi na bora.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Business

Biashara ya Mananasi yakabiliwa na changamoto Kilifi

Published

on

By

Wafanyibiashara kuuza matunda aina ya Nanasi kaunti ya Kilifi wanasema biashara ya matunda hayo inazidi kudorora msimu huu ikilinganishwa na msimu uliopita.

Kulingana na wafanyibiashara hao, matunda ya Mananasi hayapatikana kwa urahisi sokoni kutokana na mabadiliko ya hali ya angani licha ya biashara ya matunda hayo kuwa na thamani kubwa katika soko la Pwani na taifa.

Wakiongozwa na Japhet Khambi, wafanyibiashara hao walisema kwa sasa wanategemea matunda hayo kutoka nje ya nchi hasa taifa la Uganda ambapo uagizaji wa matunda hayo umekuwa ghali mno.

Katika suala la usafirishaji wa bidhaa hiyo katika soko la kaunti ya Kilifi kutoka taifa hilo jirani la Afrika Mashariki, wafanyibiashara hao walisema ghamara ya usafiri uko juu mno hali ilichangia bei ya bidhaa hizo kuongezeka mara dufu.

“Hii mambo ya gharama ya usafirishaji na uhaba wa matunda hayo bei ya bidhaa hiyo imepanda kwa kiwango kikubwa, alieleza Khambi.

Wafanyibiashara wa matunda ya Mananasi walisema Nanasi ambalo lilikuwa Linanunuliwa kwa shilingi 100 sasa tunda hilo limepanda bei na kuuzwa kwa shilingi 250.

“ Tulikuwa tunanunua Mananasi kutoka eneo la Chakama katika eneo bunge la Magarini kaunti ya Kilifi kwa bei nafuu lakini kwa sasa hayapatikani na kutulazimu kuangiza matunda kutoka Uganda.”, alisema Khambi.

Taarifa ya Pauline Mwango

Continue Reading

Business

Bei za mafuta kuongezeka katikati ya mwezi aprili

Published

on

By

Kenya sasa inakabiliwa na hatari ya kupanda kwa bei za mafuta, huku mgogoro unaoendelea mashariki ya Kati ukianza kuathiri bei nchini.

Serikali sasa imeonya kuwa kufikia katikati ya mwezi Aprili, bei za mafuta huenda zikapanda ikionya kuwa ongezeko la bei ya mafuta kwa sasa haliwezi kuepukika kufuatia kupanda kwa bei za mafuta kimataifa.

Waziri wa hazina kuu ya kitaifa John Mbadi aliwahakikishia wakenya kuwa hakuna cha kuhofia kwani wameweka mikakati kupunguza athari zake.

Ili kupunguza athari za bei za mafuta kuongezeka, serikali ilisema itatumia shilingi bilioni 17 kutoka mfuko wa ada ya uwekezaji wa mafuta kusaidia kudhibiti bei kwa mda wa miezi 3 ijayo.

Kwa sasa serikali inasema kuna akiba ya kutosha ya mafuta na shehena zaidi zinatarajiwa nchini hivi karibuni.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

Trending