Connect with us

News

Kenya, Ufaransa kukabili mabadiliko ya tabia nchi.

Published

on

Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron amesisitiza ushirikiano kati ya ufaransa na Kenya katika kutetea ajenda ya kimataifa inayojumuisha maendeleo endelevu na hatua za kukabili mabadiliko ya tabia nchi, kabla ya mkutano mwengine utakaohusisha bara afrika na Ufaransa jijini Nairobi mwaka ujao.

Akizungumza kutoka Seville katika kongamano la ngazi ya juu kuhusu ushirikiano wa kimataifa, Rais Macron alisisitiza maono yake ya pamoja na Rais William Ruto akisema hakuna nchi inapaswa kulazimishwa kuchagua kati ya maendeleo ya kiuchumi na ulinzi wa mazingira.

“Pamoja na Rais William Ruto, tunashiriki ahadi moja: kwamba hakuna nchi inapaswa kuchagua kati ya maendeleo na kulinda sayari,” Macron alisema. “Haya ndiyo matamanio tunayoleta leo Seville na washirika wetu, kama sehemu ya mkataba wa mafanikio, watu na sayari uliozinduliwa miaka miwili iliyopita huko Paris.”

Viongozi hao wawili wanatarajiwa kuendeleza ajenda hii katika kongamano la Afrika na Ufaransa 2026, ambalo litasimamiwa na Kenya na Ufaransa jijini Nairobi.

Mkutano huo unatazamiwa kuangazia ushirikiano wa kibunifu unaoshughulikia malengo ya maendeleo endelevu ya afrika sambamba na kukuza ukuaji wa uchumi jumuishi.

Rais Macron pia alisema kuwa Kenya na Ufaransa zinashirikiana kikamilifu katika miradi muhimu ya nchi mbili kama vile mpito wa nishati, miundombinu endelevu ya uchukuzi na maendeleo ya kilimo.

Alisema miradi hii, inaonyesha aina ya ushirikiano wa kimantiki unaohitajika ili kufikia maendeleo yanayostahimili hali ya hewa.

Mbali na ushirikiano wa kiuchumi na kimazingira, marais hao wawili walisisitiza dhamira yao ya pamoja ya kukuza amani na usalama kote barani Afrika, hasa katika eneo la Maziwa Makuu, Sudan na Somalia.

“Tulisisitiza dhamira yetu ya pamoja ya amani na usalama katika eneo la Maziwa Makuu, Sudan, na Somalia,” Rais Macron alibainisha, akisisitiza jukumu la Ufaransa na Kenya kusaidia utulivu wa kikanda kupitia ushirikiano wa kidiplomasia na usaidizi wa maendeleo.

Tarifa ya Joseph Jira

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Polisi wanachunguza tukio la wizi dhidi ya raia wa kigeni

Published

on

By

Maafisa wa Polisi kaunti ya Mombasa wanachunguza tukio la wizi dhidi ya mtalii wa kigeni lililotokea katika eneo la Nyali

Kulingana na ripoti ya maafisa wa polisi, mtalii huyo mwenye umri wa miaka 51 ambaye ni raia wa Marekani, anadai kulaghaiwa na kisha kushambuliwa na kundi la wanaume aliyokutana nao muda mfupi kabla ya tukio.

Ripoti hiyo imeeleza kwamba mnamo mwezi Aprili 9 mwaka huu, raia huyo wa kigeni akiwa katika mkahawa mmoja eneo la Nyali jijini Mombasa, alikutana na mwanaume aliyejitambulisha kama Alex, ambaye alimshawishi kuelekea katika nyumba ya Airbnb iliyoko karibu na mkahawa huo.

Taarifa hiyo ilifafanua zaidi kwamba alipofika katika chumba hicho, alikumbana na wanaume wengine watano waliokuwa wakimsubiri ambapo mlango ulifungwa na kisha akashambuliwa na kulazimishwa kutoa pesa na vitu vya thamani.

Wahalifu hao walitoroka na mali mbalimbali ikiwemo simu ya rununu, kompyuta mpakato (laptop), fedha taslimu pamoja na fedha za kigeni na pia walifanikiwa kutoa pesa kutoka kwenye kadi zake za benki kwa njia ya udanganyifu.

Maafisa wa polisi kutoka Bamburi kwa kushirikiana na maafisa wa upelelezi wa DCI Nyali walifika eneo la tukio na kuanza uchunguzi, ingawa hadi sasa hakuna mtu aliyekamatwa wala mali iliyopatikana.

Kesi hiyo imewekwa chini ya uchunguzi zaidi huku juhudi zikiendelea kuwabaini na kuwakamata wahusika wa tukio hilo.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

News

Polisi eneo la Likoni-Mombasa inachunguza kifo cha mwanamke

Published

on

By

Idara ya usalama eneo la Likoni kaunti ya Mombasa imesema inachunguza kifo cha mwanamke mmoja aliyefariki katika mtaa wa senti kumi.

Mkuu wa polisi wa Likoni Joseph Mutungi alisema mwanamke huyo anadaiwa kupoteza maisha wakati wakiwa nyumbani kwa mwanamme anayesemekana kuwa mchumba wake.

Taarifa za awali ziliarifu kuwa marehemu alikuwa mgonjwa na anadaiwa alifika hospitalini kusaka matibabu japo hakupata huduma na kurejea nyumbani bila kutibiwa.

Inasemekana baadaye mchumba wake alioondoka kwenda kazini na kumwacha chini ya uangalizi wa mwanamke mwengine katika ploti hiyo.

Hali yake inadaiwa kuzorota na hatimaye kuaga dunia.

Maafisa wa usalama walisema wanaendelea na uchunguzi kubaini chanzo cha kifo hicho.

Mwili wa marehemu unahifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti katika hospitali ya Coast general kwa uchunguzi zaidi.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Trending