Connect with us

News

KESSHA: Huenda shule za upili zikafungwa kufuatia ukosefu wa fedha

Published

on

Katibu Mkuu wa Muungano wa walimu wakuu wa shule za upili nchini KESSHA Abdinoor Haji
ameonya kuhusu uwezekano wa shule kufungwa mapema iwapo pesa za kugharimia masomo hazitatolewa haraka.

Haji alisema ukosefu wa fedha hizo umeathiri shughuli mbalimbali shuleni kote nchini.

Haji alisema ucheleweshwaji wa kutolewa kwa fedha hizo umesababisha viwango vya elimu kudorora na ndio chanzo kikuu cha upatikanaji wa alama za E katika mitihani ya kitaifa ya KCSE kwa muda wa miaka mitatu iliyopita.

“Shule za kutwa ndizo ziliathiriwa zaidi kwa sababu zinategemea pakubwa fedha hizo za serikali. Ukosefu wa fedha hizo umedumaza uwezo wa kufanikisha upatikanaji wa elimu bora,” alisema Haji.

Aidha, alisema kutokana na ukosefu wa fedha, shule nyingi zimeshindwa kuwalipa wasambazaji bidhaa huku baadhi ya shule zikilazimika kuwaachisha kazi walimu walioajiriwa na bodi za usimamizi wa shule.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa KESSHA Willy Kuria alisema shule za upili zinaidai serikali kuu shillingi bilioni 17 za muhula wa kwanza na wa pili.

Kuria alisema ikiwa Wizara ya Elimu nchini itakosa kulipa malimbikizi hayo ya madeni, shule zitalazimika kufungwa mapema kwa sababu ya ukosefu wa pesa za kuwaweka wanafunzi shuleni.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Polisi wanachunguza tukio la wizi dhidi ya raia wa kigeni

Published

on

By

Maafisa wa Polisi kaunti ya Mombasa wanachunguza tukio la wizi dhidi ya mtalii wa kigeni lililotokea katika eneo la Nyali

Kulingana na ripoti ya maafisa wa polisi, mtalii huyo mwenye umri wa miaka 51 ambaye ni raia wa Marekani, anadai kulaghaiwa na kisha kushambuliwa na kundi la wanaume aliyokutana nao muda mfupi kabla ya tukio.

Ripoti hiyo imeeleza kwamba mnamo mwezi Aprili 9 mwaka huu, raia huyo wa kigeni akiwa katika mkahawa mmoja eneo la Nyali jijini Mombasa, alikutana na mwanaume aliyejitambulisha kama Alex, ambaye alimshawishi kuelekea katika nyumba ya Airbnb iliyoko karibu na mkahawa huo.

Taarifa hiyo ilifafanua zaidi kwamba alipofika katika chumba hicho, alikumbana na wanaume wengine watano waliokuwa wakimsubiri ambapo mlango ulifungwa na kisha akashambuliwa na kulazimishwa kutoa pesa na vitu vya thamani.

Wahalifu hao walitoroka na mali mbalimbali ikiwemo simu ya rununu, kompyuta mpakato (laptop), fedha taslimu pamoja na fedha za kigeni na pia walifanikiwa kutoa pesa kutoka kwenye kadi zake za benki kwa njia ya udanganyifu.

Maafisa wa polisi kutoka Bamburi kwa kushirikiana na maafisa wa upelelezi wa DCI Nyali walifika eneo la tukio na kuanza uchunguzi, ingawa hadi sasa hakuna mtu aliyekamatwa wala mali iliyopatikana.

Kesi hiyo imewekwa chini ya uchunguzi zaidi huku juhudi zikiendelea kuwabaini na kuwakamata wahusika wa tukio hilo.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

News

Polisi eneo la Likoni-Mombasa inachunguza kifo cha mwanamke

Published

on

By

Idara ya usalama eneo la Likoni kaunti ya Mombasa imesema inachunguza kifo cha mwanamke mmoja aliyefariki katika mtaa wa senti kumi.

Mkuu wa polisi wa Likoni Joseph Mutungi alisema mwanamke huyo anadaiwa kupoteza maisha wakati wakiwa nyumbani kwa mwanamme anayesemekana kuwa mchumba wake.

Taarifa za awali ziliarifu kuwa marehemu alikuwa mgonjwa na anadaiwa alifika hospitalini kusaka matibabu japo hakupata huduma na kurejea nyumbani bila kutibiwa.

Inasemekana baadaye mchumba wake alioondoka kwenda kazini na kumwacha chini ya uangalizi wa mwanamke mwengine katika ploti hiyo.

Hali yake inadaiwa kuzorota na hatimaye kuaga dunia.

Maafisa wa usalama walisema wanaendelea na uchunguzi kubaini chanzo cha kifo hicho.

Mwili wa marehemu unahifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti katika hospitali ya Coast general kwa uchunguzi zaidi.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Trending