Connect with us

Business

Bei ya mafuta ya Petroli, Dizeli na Taa yapanda

Published

on

Huenda wakenya wakagharamika zaidi katika kumudu gharama ya maisha kutokana na ongezeko la bei ya mafuta ya Petroli, Dizeli na Taa mtawalia.

Hii ni kutokana na bei mpya iliyotolewa na Mamlaka ya kudhibiti Kawi na mafuta ya Petroli nchini EPRA kwani bei ya mafuta ya Petroli imeongezeka kwa shilingi 8.99, mafuta ya Dizeli kwa shilingi 8.67 na mafuta ya taa kwa shilingi 9.55 kwa lita.

Kulingana na EPRA, bei hiyo mpya itatumika kwa kipindi cha mwezi mmoja hadi Agosti 14, ambapo bei ya mafuta ya Petroli katika jiji la Nairobi itauzwa kwa shilingi 186.31, Diseli kwa shilingi 171.58 na mafuta ya taa kwa shilingi 156.58.

Katika jiji la Mombasa bei hiyo mpya ya mafuta itauzwa kwa shilingi 183.02, mafuta ya Dizeli yatauzwa kwa shilingi 168.30 na mafuta ya taa yatauzwa kwa shilingi 153.29 kwa lita katika kipindi cha siku 30.

Hata hivyo katika kaunti ya Kilifi bei hiyo ya mafuta iko tafauti kwa sasa mafuta ya Petroli yatauzwa kwa shilingi 183.88, mafuta ya Dizeli yakiuzwa kwa shilingi 169.16 na matufa ya taa yatauzwa kwa shilingi 153.29 kwa lita.

Kulingana na taarifa kutoka EPRA, bei hiyo mpya mafuta imetoka na kupanda kwa bei ya mali ghafi kwa asilimia 6.45 ambayo ni Dola za Marekani 590.24 kwa “Cubic metre” kwenye mafuta ya Petroli mwezi Mei mwaka huu.

Mkurugenzi mkuu wa Mamlaka hiyo Daniel Bargoria alisema japo bei hiyo huenda ikashuka iwapo soko huru la mafuta litapunguza bei ya mali ghafi ambayo imechangiwa na mizozo ya kivita katika mataifa yanayopigana ambayo na yamekuwa yanazalisha mafuta.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Business

Wafanyibiashara wa mitumba eneo la Diani wafunga biashara zao

Published

on

By

Wafanyibiashara wa mitumba katika soko la Diani, kaunti ya Kwale, wamelazimika kufunga biashara zao kutokana na kudorora kwa shughuli za kibiashara katika kipindi hiki cha msimu wa watalii wachache na mvua zinazoendelea kushuhudiwa katika eneo hilo.

Wafanyabiashara hao wanasema idadi ya wanunuzi imepungua kwa kiasi kikubwa, hali iliyosababisha nguo nyingi kukosa soko.

Kulingana na wafanyibiashara hao wanategemea zaidi watalii wa ndani na nje  na kutokana na msimu huu kuwa uko uko chini wateja wamepungua hali inayofanya maisha kuwa mgumu.

Wanasema  wamelazimika kutupa baadhi ya nguo kwani  zimesalia sokoni kwa  muda mrefu hadi zingingine kuharibika, jambo ambalo limepelekea kupata hasara kubwa.

Aidha, wameongeza kuwa bei ya nguo za mitumba imeendelea kupanda ambapo wananunua ngunia moja kwa shilingi elfu 40 huku mauzo yakizidi kushuka.

“ Biashara imedorora sai kwani hakuna wateja ikizingatiwa kuwa tunategemea sana watalii na sasa hakuna wageni hata imetulazimu kutupa nguo kwani ngigi zimeharibika baada ya kukaa kwa mda mrefu bila kununuliwa”.

Taarifa ya Pauline Mwango

Continue Reading

Business

Mamlaka ya AFA yahimiza upanzi wa mkorosho

Published

on

By

Mamlaka ya Kilimo na Chakula nchini AFA, imekuwa mstari wa mbele kuhakikisha taifa linaboresha mazao yake na kuchangia uzalishaji wa chakula nchini.

Hatua hii imechangia zaidi na mikakati endelevu ya kuwawezesha wakulima kufahamu mipango endelevu ya uimarishaji wa Kilimo cha sasa na kwa kuzingatia utumiaji wa mifumo bora ya kilimo.

Mamlaka hiyo ambapo inaendeleza kampeni ya kuhamisha wakulima kuhusu umuhimu wa kilimo cha Korosho imesisitiza haja ya ujumuishaji wa wakulima, wawekezaji na wadau mbalimbali ili kupiga jeki sekta ya Kilimo huku ikiahidi kuendeleza hamasa kwa jamii za kaunti za Pwani kuhusu kilimo cha korosho na utafutaji wa soko huru.

Katika Kongamano la kitaifa lililoandaliwa katika kaunti ya Kwale, Mamlaka hiyo iliwapa wakulima kutoka kaunti sita za Pwani miche ya mikorosho elfu mia moja katika juhudi za kukuza kilimo cha zao hilo nchini.

Katibu katika Idara ya Kilimo nchini Paul Kiprono, alisema mpango huo unalenga kuwawezesha wakulima kuongeza uzalishaji wa korosho na kuchangia ukuaji wa uchumi wa taifa.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa kongamano hilo, Kiprono alitoa wito kwa serikali za kaunti pamoja na wadau wa sekta ya kilimo kushirikiana kwa karibu ili kuboresha kilimo cha korosho.

“Kenya ilikuwa ikiongoza katika zao la mkorosho katika miaka ya 1990 lakini kutokana na changamoto za kibiashara zao hilo lilishuka katika masoko ya kimataifa kutokana na ukosefu wa kuwekezaji kwa wakulima lakini sasa tumeanza kupiga hatua kwani tunazalisha zaidi ya tan elfu 9 za korosho”, alisema Rono.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa AFA, Cornelly Serem, alisema mamlaka hiyo imejizatiti kuboresha kilimo cha korosho kupitia utoaji wa miche bora na mafunzo kwa wakulima ili kuongeza tija.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Trending