Business
KTB imeweka mikakati ya kuwavutia wawekezaji wa kimataifa
Serikali ya kitaifa kupitia bodi ya utalii nchini (KTB) imeweka mikakati ya kuwavutia wawekezaji wa kimataifa ili kupanua soko la wageni kutoka mataifa ya nje.
Mwenyekiti wa bodi hiyo Francis Gichaba alisema kutokana na hatua hiyo, idadi ya watalii wanaozuru Pwani itaongezeka hadi zaidi ya asilimia 50 ikilinganishwa na nchi zingine zilizonawiri katika sekta ya utalii.
Akizungumza katika kongamano la uekezaji wa utalii eneo la Diani kaunti ya Kwale, Gichaba alisisitiza umuhimu wa waekezaji kuboresha maeneo ya hoteli pamoja na vivutio vingine vya kitalii.
Kwa upande wake mkurugenzi mkuu wa mamlaka ya kudhibiti utalii (TRA) Norbert Talam amesema kuwa uboreshaji wa hoteli hizo utainua viwango vya utalii nchini.
Hata hivyo Wadau wa sekta ya utalii wakiongozwa na Hasnain Nooran waliitaka serikali kuu kuongeza safari za ndege za moja kwa moja katika eneo la Pwani.
“Ikiwa Kenya itakuwa na safari za ndege za moja kwa moja kutoka mataifa ya Ulaya hadi Pwani ya Kenya basi itakuwa vizuri zaidi kuimarisha sekta ya utalii nchini kwani tumetegemea pia watalii wa kigeni”, alisema Hasnain.
Taarifa ya Mwanahabari wetu
Business
KPA yaimarisha usafirishaji wa makasha na kampeni za kimataifa
Halmashauri ya bandari nchini (KPA), imeimarisha ushirikiano wake na kampuni ya kimataifa ya usafirishaji kwa njia ya bahari, Maersk, katika juhudi za kuboresha huduma na kuongeza ufanisi wa usafirishaji wa mizigo katika eneo la Afrika Mashariki.
Makubaliano hayo yameafikiwa katika mkutano uliofanyika katika makao makuu ya KPA jijini Mombasa ambapo Mkurugenzi wa Maersk Kanda ya Afrika Mashariki, Tito Okuku, alieleza kuwa kampuni hiyo ina nia ya kupanua shughuli zake zaidi nchini na katika eneo la Afrika Mashariki kwa ujumla.
Moja ya maeneo yatakayopata kipaumbele ni kuimarisha matumizi ya Kituo cha Makontena cha ndani cha Naivasha kinachotazamwa kama kitovu muhimu katika kushughulikia usafirishaji wa mazao ya kilimo kutoka Kenya kwenda masoko ya kimataifa, huku kikitoa njia ya haraka na ya kuaminika kwa wauzaji kufikia masoko ya kimataifa.
Mkurugenzi Mkuu wa KPA, Nahodha William Ruto, alieleza kukubaliana na hatua hiyo akisema ni wakati mwafaka kwa pande zote mbili kuimarisha ushirikiano huo.
Aidha alibainisha kuwa Bandari ya Mombasa pamoja na vituo vyake vya ndani vinaendelea kushuhudia ongezeko la shehena, na akahakikishia kuwa KPA iko tayari kushughulikia mahitaji yanayoongezeka kupitia maboresho ya miundombinu na huduma.
Taarifa ya Mwanahabari wetu
Business
Wakulima wa Mananasi Magarini walilia soko
Wakulima wa matunda aina ya nanasi katika eneo bunge la Magarini kaunti ya Kilifi wanaitaka serikali kuwatafutia soko ili kuuza bidhaa zao ambazo zinaendelea kuharibika msimu huu.
Kulingana na wakulima hao hakuna soko ambapo wanaweza kuuza bidhaa hizo kwa bei nzuri hali inayofanya wakulima wengi kuuza kwa bei ya chini ili kuepuka kuharibika kwa katunda hayo.
Wakizunumza na cocofm wakulima hao walisema kuwa kwa sasa wanakadiria hasara kwani matunda ni mengi.
Wakati huo huo wakulima hao wameitaka serikali ya kaunti kujenga viwanda.
Ni kauli ambayo imeongwa mkono na wafanyibiashara wa matunda mjini Kilifi kaunti ya Kilifi ambao walisema kuwa matunda mengi msimu huu huharibika kutokana na idadi ndogo ya wateja.
“Serikali itutafutie soko pamoja na kujenga viwanda ili kusaidia wakulima na wafanyibiashara wa matunda aina ya mamanasi, kuuza matunda yao ili kuawaepushia hasara hasa wakati huu ambapo matunda ni mengi.”
Taarifa ya Pauline Mwango

