Connect with us

News

Polisi wamewakamata vijana sita Wahalifu, Kaunti ya Kilifi.

Published

on

Maafisa wa Idara ya DCI kwa ushirikiano na kitengo maalum cha Polisi wamefanikiwa kuwakamata vijana sita wanaoshukiwa kuwa wahalifu.

Katika taarifa ya Polisi, wahalifu nao wanadaiwa kwamba wamekuwa wakiwapora wananchi fedha zao wanapozuru benki mbalimbali.

Kamanda wa Polisi eneo la Kilifi Kusini Hassan Rochale amethibitisha kukamatwa kwa wahalifu hao, akisema maafisa wa polisi wako makini kuhakikisha wahalifu wote wanakabiliwa kisheria.

Maafisa wa polisi wamesema wakati wa makabiliano na wahalifu hao, mhalifu mmoja alipigwa risasi na kujeruhiwa mkono huku magari mawili yenye nambari bandia za usajali pamoja na vifaa nyingine hatari vilivyotumika kwa uhalifu vikinaswa na maafisa wa polisi.

Aidha wamesema wahalifu hao wamekuwa wakiwahangaisha wakaazi wa kaunti za Kilifi na Mombasa, na kwamba wamekamatwa katika eneo la Kadzengo kwenye barabara kuu ya Mombasa – Malindi wakielekea maeneo ya Mtwapa kutoka Kilifi.

Wahalifu hao ni pamoja na Erick Wachira, Ali Said Nassir, Fredrick Kalugo Konde, Nicholas Mungaro Kitumba, Fred Mwajira, na Edwin Kyalo Mulandi.

Wahalifu hao wanazuiliwa katika kituo cha polisi cha Kijipwa kaunti ya Kilifi wakisubiri kufikishwa Mahakamani.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Polisi wanachunguza tukio la wizi dhidi ya raia wa kigeni

Published

on

By

Maafisa wa Polisi kaunti ya Mombasa wanachunguza tukio la wizi dhidi ya mtalii wa kigeni lililotokea katika eneo la Nyali

Kulingana na ripoti ya maafisa wa polisi, mtalii huyo mwenye umri wa miaka 51 ambaye ni raia wa Marekani, anadai kulaghaiwa na kisha kushambuliwa na kundi la wanaume aliyokutana nao muda mfupi kabla ya tukio.

Ripoti hiyo imeeleza kwamba mnamo mwezi Aprili 9 mwaka huu, raia huyo wa kigeni akiwa katika mkahawa mmoja eneo la Nyali jijini Mombasa, alikutana na mwanaume aliyejitambulisha kama Alex, ambaye alimshawishi kuelekea katika nyumba ya Airbnb iliyoko karibu na mkahawa huo.

Taarifa hiyo ilifafanua zaidi kwamba alipofika katika chumba hicho, alikumbana na wanaume wengine watano waliokuwa wakimsubiri ambapo mlango ulifungwa na kisha akashambuliwa na kulazimishwa kutoa pesa na vitu vya thamani.

Wahalifu hao walitoroka na mali mbalimbali ikiwemo simu ya rununu, kompyuta mpakato (laptop), fedha taslimu pamoja na fedha za kigeni na pia walifanikiwa kutoa pesa kutoka kwenye kadi zake za benki kwa njia ya udanganyifu.

Maafisa wa polisi kutoka Bamburi kwa kushirikiana na maafisa wa upelelezi wa DCI Nyali walifika eneo la tukio na kuanza uchunguzi, ingawa hadi sasa hakuna mtu aliyekamatwa wala mali iliyopatikana.

Kesi hiyo imewekwa chini ya uchunguzi zaidi huku juhudi zikiendelea kuwabaini na kuwakamata wahusika wa tukio hilo.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

News

Polisi eneo la Likoni-Mombasa inachunguza kifo cha mwanamke

Published

on

By

Idara ya usalama eneo la Likoni kaunti ya Mombasa imesema inachunguza kifo cha mwanamke mmoja aliyefariki katika mtaa wa senti kumi.

Mkuu wa polisi wa Likoni Joseph Mutungi alisema mwanamke huyo anadaiwa kupoteza maisha wakati wakiwa nyumbani kwa mwanamme anayesemekana kuwa mchumba wake.

Taarifa za awali ziliarifu kuwa marehemu alikuwa mgonjwa na anadaiwa alifika hospitalini kusaka matibabu japo hakupata huduma na kurejea nyumbani bila kutibiwa.

Inasemekana baadaye mchumba wake alioondoka kwenda kazini na kumwacha chini ya uangalizi wa mwanamke mwengine katika ploti hiyo.

Hali yake inadaiwa kuzorota na hatimaye kuaga dunia.

Maafisa wa usalama walisema wanaendelea na uchunguzi kubaini chanzo cha kifo hicho.

Mwili wa marehemu unahifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti katika hospitali ya Coast general kwa uchunguzi zaidi.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Trending