Connect with us

News

Mahakama ya Kilifi yaagiza kukamatwa kwa washukiwa watatu wa mauaji

Published

on

Mahakama ya Kilifi imeagiza kukamatwa kwa washukiwa watatu akiwemo Wakili Devison Liano Kazungu, ambaye amekuwa akihudumu bila vibali halali pamoja Karani wake Hersi Mathius Kahindi na Lawrence Menza Gona ili wafikishwe Mahakamani.

Hii ni baada ya mshukiwa Charo Kazungu Baya kufikishwa Mahakamani pekee huku wenzake wakiwa mafichoni kufuatia kesi ya mauaji ya Silvia Panganin ambaye ni rais wa Uswizi.

Hakimu wa Mahakama hiyo Charles Obulutsa alitoa agizo hilo baada ya Afisi wa polisi anayechunguza kesi hiyo Felix Odwiya kuiambia Mahakama kwamba uchunguzi wa kesi hiyo bado unaendelea.

Mawakili wa washukiwa walimtea mteja wao na kuwasilisha ombi la kutaka aachiliwe kwa dhamana ombi ambalo limepingwa vikali na upande wa mashtaka ukiongozwa na Ridhwan Mohammed.

Katika kesi hiyo mshukiwa Charo Kazungu Baya alibainika kwamba mnamo mwezi Juni mwaka 2024 katika Ofisi za usajili wa ardhi mjini Kilifi alijisajili kama mmiliki wa kipande cha ardhi nambari gede/dabaso 454 yenye thamani ya shilingi milioni 26, mali ya marehemu Silvia Panganin, akisema alikuwa ameachiwa kama urithi.

Mshukiwa Baya anakabiliwa na shtaka lengine la kuchukua na kujisajili kama mmiliki wa gari aina ya Toyota Wagon nambari ya usajili KBU 076N mali ya Luigi Paganin yenye thamani ya shilingi laki tano na elfu hamsini, akisema aliuziwa na bibi yake marehemu Silvia Vera Panganin.

Kesi hiyo itaendelea mnamo tarehe 6 mwezi Machi mwaka huu ambapo Mahakama itatoa uamuzi wa ombi la kuachiliwa kwa mshukiwa kwa dhamana au la.

Taarifa ya Teclar Yeri

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Ethekon: Uchaguzi mkuu utakuwa huru, haki na uwazi

Published

on

By

Tume huru ya uchaguzi na mipaka nchini IEBC imeanza rasmi zoezi la kuwasajili wapiga kura wapya kote nchini, huku ikilenga kuwasajili wapiga kura milioni 6.2, kabla ya uchaguzi mkuu ujao. 

Mwenyekiti wa Tume hiyo Erastus Ethekon aliwahakikishia wakenya kwamba makamishna wa tume hiyo watahakikisha uchuguzi mkuu ujao unakuwa huru, haki na uwazi.

Akizungumza katika kaunti ya Kwale wakati wa kuzindua wa zoezi la usajili wa wakipiga kura kote nchini, Ethekon alisema serikali imewekeza raslimali za kutosha za kufanikisha zoezi hilo.

“Nataka kuwahakikishia wakenya kwamba tumejipanga kama IEBC na tuko na raslimali za kutosha kuhakikisha zoezi la usajili wa wapiga kura linaendeshwa vyema na uchaguzi mkuu utakuwa huru, haki na wazi ili kuhakikisha wakenya wanatekeleza jukumu lao la kidemokrasia na hatua hiyo tutafikia idadi ya wapiga kura zaidi ya milioni 27”, alisema Ethekon.

Naye Naibu Mwenyekiti wa IEBC Fahima Araphat alisema tayari maafisa wapya wa IEBC elfu 12 wameajiriwa kuhakikisha zoezi hilo liendeshwa vyema ili kusajili idadi kubwa ya wapiga kura

“Sisi tunafanya kazi yetu bila kuegemea upande wowote wa kisiasa na tuko tayari kuhakikisha anashinda uchaguzi anatangazwa mshindi kwa haki, na kama tuko na makarani elfu 12 na wote wasajili wapiga kura wapya elfu 10 kila moja tutakuwa na idadi kubwa ya wapiga kura, sasa hiyo ndio tunalenga kupata”, alisema Fahima.

Kwa upande wake Gavana wa kaunti ya Kwale Fatuma Achani, aliipongeza tume hiyo kwa zoezi hilo endelevu la wapiga kura, akisema ni hatua ya kipekee kwa jamii ambazo zimekosa fursa ya kujisajili kama wapiga kura.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

News

IEBC yasema idadi ya wanaojisajili ni ndogo mno

Published

on

By

Zoezi endelevu la usajili wa wapiga kura kote nchini limeng’oa nanga huku maafisa wa Tume huru ya uchaguzi na mipaka nchini IEBC wakilenga idadi kubwa ya vijana katika zoezi hilo.

Katika kaunti ya Kilifi eneo bunge la Kilifi Kazkazini, zoezi hilo limefanyika katika vituo vinne tofauti huku idadi ndogo ya wapiga kura ikishuhudiwa licha ya vuguvugu la TUKO KADI kuanzishwa na vijana ili kuwajisajili wapiga kura.

Akizungumza na Wanahabari wakati wa zoezi hilo, Naibu Afisa wa usajili wa wapiga kura katika eneo bunge la Kilifi Kazkazini Abdul Mohammed aliwarai vijana kujitokeza kwa wingi na kujisajili.

Mohammed pia aliwarai vijana kukoma kutumiwa vibaya na wanasiasa kwa manufaa yao binafsi, akipongeza vuguvugu lilionzishwa na vijana la TUKO KADI kama njia moja ya kuwahamasisha vijana kujisajili kama wapiga kura.

“Tumeanza zoezi hili na tunawahimiza vijana wajitokeze kwa wingi na kujisajili kama wapiga kura ili kutumia nafasi hiyo kuchagua viongozi wanawataka na wala wasikubali kutumiwa vibaya na wanasiasa”, alisema Mohammed.

Kwa upande wao baadhi ya vijana waliojisajili waliwarai vijana wenzao kujitokeza kwa wingi na kushiriki zoezi hilo ili kuchagua viongozi wanaohisi wataleta maendeleo sawa na kubuni nafasi za ajira.

Taarifa ya Elizabeth Mwende

Continue Reading

Trending