Connect with us

News

Mahakama ya Kilifi yaagiza kukamatwa kwa washukiwa watatu wa mauaji

Published

on

Mahakama ya Kilifi imeagiza kukamatwa kwa washukiwa watatu akiwemo Wakili Devison Liano Kazungu, ambaye amekuwa akihudumu bila vibali halali pamoja Karani wake Hersi Mathius Kahindi na Lawrence Menza Gona ili wafikishwe Mahakamani.

Hii ni baada ya mshukiwa Charo Kazungu Baya kufikishwa Mahakamani pekee huku wenzake wakiwa mafichoni kufuatia kesi ya mauaji ya Silvia Panganin ambaye ni rais wa Uswizi.

Hakimu wa Mahakama hiyo Charles Obulutsa alitoa agizo hilo baada ya Afisi wa polisi anayechunguza kesi hiyo Felix Odwiya kuiambia Mahakama kwamba uchunguzi wa kesi hiyo bado unaendelea.

Mawakili wa washukiwa walimtea mteja wao na kuwasilisha ombi la kutaka aachiliwe kwa dhamana ombi ambalo limepingwa vikali na upande wa mashtaka ukiongozwa na Ridhwan Mohammed.

Katika kesi hiyo mshukiwa Charo Kazungu Baya alibainika kwamba mnamo mwezi Juni mwaka 2024 katika Ofisi za usajili wa ardhi mjini Kilifi alijisajili kama mmiliki wa kipande cha ardhi nambari gede/dabaso 454 yenye thamani ya shilingi milioni 26, mali ya marehemu Silvia Panganin, akisema alikuwa ameachiwa kama urithi.

Mshukiwa Baya anakabiliwa na shtaka lengine la kuchukua na kujisajili kama mmiliki wa gari aina ya Toyota Wagon nambari ya usajili KBU 076N mali ya Luigi Paganin yenye thamani ya shilingi laki tano na elfu hamsini, akisema aliuziwa na bibi yake marehemu Silvia Vera Panganin.

Kesi hiyo itaendelea mnamo tarehe 6 mwezi Machi mwaka huu ambapo Mahakama itatoa uamuzi wa ombi la kuachiliwa kwa mshukiwa kwa dhamana au la.

Taarifa ya Teclar Yeri

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending