Connect with us

News

Musyoka, Akosoa Kuvamiwa kwa Gachagua Kasarani

Published

on

Kinara wa Chama cha Wiper Kalonzo Musyoka amekosoa uvamizi uliofanywa na kundi la vijana wakati wa ibada ya Jumapili katika Kanisa la PCEA Kasarani jijiji Nairobi.

Kalonzo amesema uvamizi huo ulitatiza shughuli za ibada Kanisani na huenda vijana hao walikuwa na malengo ya kumdhuru aliyekuwa Naibu Rais Rigathi Gachagua.

Kalonzo ametaja kitendo hicho kama cha aibu kwa taifa hili ambalo linatambulika na ulimwengu kama taifa lenye kuenzi amani na usalama, uwiano na ushirikiano wa kijamii.

Kiongozi huyo wa Wiper amedai kuchukizwa na jinsi vijana wanavyoweza kusababisha vurugu katika sehemu za ibada, akisema tabia hiyo inafaa kukomeshwa kote nchini.

Katika tukio hilo la siku ya Jumapili, Gachagua amemkashfu Rais William Ruto na Gavana wa Nairobi Johnson Sakaja akidai kwamba wanahusika moja kwa moja na shambulio hilo hali ambayo ilizua taharuki Kanisani.

Akizungumza baada ya maafisa wake wa kibinafsi na wale wa usalama kuingilia kati swala hilo, Gachagua amedai kushangazwa na baadhi ya maafisa wa polisi kutothubutu kusaidia kuimarisha usalama wakati wa tukio.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Polisi wanachunguza tukio la wizi dhidi ya raia wa kigeni

Published

on

By

Maafisa wa Polisi kaunti ya Mombasa wanachunguza tukio la wizi dhidi ya mtalii wa kigeni lililotokea katika eneo la Nyali

Kulingana na ripoti ya maafisa wa polisi, mtalii huyo mwenye umri wa miaka 51 ambaye ni raia wa Marekani, anadai kulaghaiwa na kisha kushambuliwa na kundi la wanaume aliyokutana nao muda mfupi kabla ya tukio.

Ripoti hiyo imeeleza kwamba mnamo mwezi Aprili 9 mwaka huu, raia huyo wa kigeni akiwa katika mkahawa mmoja eneo la Nyali jijini Mombasa, alikutana na mwanaume aliyejitambulisha kama Alex, ambaye alimshawishi kuelekea katika nyumba ya Airbnb iliyoko karibu na mkahawa huo.

Taarifa hiyo ilifafanua zaidi kwamba alipofika katika chumba hicho, alikumbana na wanaume wengine watano waliokuwa wakimsubiri ambapo mlango ulifungwa na kisha akashambuliwa na kulazimishwa kutoa pesa na vitu vya thamani.

Wahalifu hao walitoroka na mali mbalimbali ikiwemo simu ya rununu, kompyuta mpakato (laptop), fedha taslimu pamoja na fedha za kigeni na pia walifanikiwa kutoa pesa kutoka kwenye kadi zake za benki kwa njia ya udanganyifu.

Maafisa wa polisi kutoka Bamburi kwa kushirikiana na maafisa wa upelelezi wa DCI Nyali walifika eneo la tukio na kuanza uchunguzi, ingawa hadi sasa hakuna mtu aliyekamatwa wala mali iliyopatikana.

Kesi hiyo imewekwa chini ya uchunguzi zaidi huku juhudi zikiendelea kuwabaini na kuwakamata wahusika wa tukio hilo.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

News

Polisi eneo la Likoni-Mombasa inachunguza kifo cha mwanamke

Published

on

By

Idara ya usalama eneo la Likoni kaunti ya Mombasa imesema inachunguza kifo cha mwanamke mmoja aliyefariki katika mtaa wa senti kumi.

Mkuu wa polisi wa Likoni Joseph Mutungi alisema mwanamke huyo anadaiwa kupoteza maisha wakati wakiwa nyumbani kwa mwanamme anayesemekana kuwa mchumba wake.

Taarifa za awali ziliarifu kuwa marehemu alikuwa mgonjwa na anadaiwa alifika hospitalini kusaka matibabu japo hakupata huduma na kurejea nyumbani bila kutibiwa.

Inasemekana baadaye mchumba wake alioondoka kwenda kazini na kumwacha chini ya uangalizi wa mwanamke mwengine katika ploti hiyo.

Hali yake inadaiwa kuzorota na hatimaye kuaga dunia.

Maafisa wa usalama walisema wanaendelea na uchunguzi kubaini chanzo cha kifo hicho.

Mwili wa marehemu unahifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti katika hospitali ya Coast general kwa uchunguzi zaidi.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Trending