Connect with us

News

Ofisi ya DPP yafungua kesi ya nne dhidi ya Mackenzie

Published

on

Mkurugenzi mkuu wa mashtaka ya umma, DPP, amefunga rasmi kesi ya nne na ya mwisho inayohusiana na mauaji ya halaiki ya watu katika msitu wa Shakahola, ambapo Mhubiri tata Paul Mackenzie na washtakiwa wengine 94 wanakabiliwa na mashtaka 238 ya kuua bila kukusudia.

Hatua hiyo imekuja baada ya shahidi wa 95 wa upande wa mashtaka ambaye ni mkuu wa upelelezi wa mauaji, Inspecta mkuu Raphael Wanjohi kuieleza Mahakama namna mtuhumiwa mkuu alivyodhibiti wafuasi wake hadi kusababisha vifo vya watu 429.

Akitoa ushahidi mbele ya Hakimu Mkuu Alex Ithuku, Wanjohi alisema Mackenzie na wenzake walikuwa na makubaliano ya pamoja ya kile alichokiita “mkataba wa kujiua,” wakidai kuwa walihamasisha kufunga hadi kufa kwa kisingizio cha kukutana na Yesu kabla ya mwisho wa Desemba 2020.

Aidha alieleza kuwa washtakiwa walikuwa na nia ya pamoja ya kusimamia vifo vya watoto na watu wazima kupitia mfungo wa kulazimishwa, huku wakijua wazi kuwa walikuwa wakitekeleza kitendo kisicho halali, jambo linalodhihirishwa na namna walivyoficha makaburi.

Upelelezi ulibaini kuwa Mackenzie alikuwa na kundi la ulinzi lililodhibiti mienendo ya watu na kuhakikisha mfungo huo unatekelezwa kikamilifu, huku mawasiliano ya simu yakionyesha ushirikiano wa karibu kati yake na wasaidizi wake.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Ethekon: Uchaguzi mkuu utakuwa huru, haki na uwazi

Published

on

By

Tume huru ya uchaguzi na mipaka nchini IEBC imeanza rasmi zoezi la kuwasajili wapiga kura wapya kote nchini, huku ikilenga kuwasajili wapiga kura milioni 6.2, kabla ya uchaguzi mkuu ujao. 

Mwenyekiti wa Tume hiyo Erastus Ethekon aliwahakikishia wakenya kwamba makamishna wa tume hiyo watahakikisha uchuguzi mkuu ujao unakuwa huru, haki na uwazi.

Akizungumza katika kaunti ya Kwale wakati wa kuzindua wa zoezi la usajili wa wakipiga kura kote nchini, Ethekon alisema serikali imewekeza raslimali za kutosha za kufanikisha zoezi hilo.

“Nataka kuwahakikishia wakenya kwamba tumejipanga kama IEBC na tuko na raslimali za kutosha kuhakikisha zoezi la usajili wa wapiga kura linaendeshwa vyema na uchaguzi mkuu utakuwa huru, haki na wazi ili kuhakikisha wakenya wanatekeleza jukumu lao la kidemokrasia na hatua hiyo tutafikia idadi ya wapiga kura zaidi ya milioni 27”, alisema Ethekon.

Naye Naibu Mwenyekiti wa IEBC Fahima Araphat alisema tayari maafisa wapya wa IEBC elfu 12 wameajiriwa kuhakikisha zoezi hilo liendeshwa vyema ili kusajili idadi kubwa ya wapiga kura

“Sisi tunafanya kazi yetu bila kuegemea upande wowote wa kisiasa na tuko tayari kuhakikisha anashinda uchaguzi anatangazwa mshindi kwa haki, na kama tuko na makarani elfu 12 na wote wasajili wapiga kura wapya elfu 10 kila moja tutakuwa na idadi kubwa ya wapiga kura, sasa hiyo ndio tunalenga kupata”, alisema Fahima.

Kwa upande wake Gavana wa kaunti ya Kwale Fatuma Achani, aliipongeza tume hiyo kwa zoezi hilo endelevu la wapiga kura, akisema ni hatua ya kipekee kwa jamii ambazo zimekosa fursa ya kujisajili kama wapiga kura.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

News

IEBC yasema idadi ya wanaojisajili ni ndogo mno

Published

on

By

Zoezi endelevu la usajili wa wapiga kura kote nchini limeng’oa nanga huku maafisa wa Tume huru ya uchaguzi na mipaka nchini IEBC wakilenga idadi kubwa ya vijana katika zoezi hilo.

Katika kaunti ya Kilifi eneo bunge la Kilifi Kazkazini, zoezi hilo limefanyika katika vituo vinne tofauti huku idadi ndogo ya wapiga kura ikishuhudiwa licha ya vuguvugu la TUKO KADI kuanzishwa na vijana ili kuwajisajili wapiga kura.

Akizungumza na Wanahabari wakati wa zoezi hilo, Naibu Afisa wa usajili wa wapiga kura katika eneo bunge la Kilifi Kazkazini Abdul Mohammed aliwarai vijana kujitokeza kwa wingi na kujisajili.

Mohammed pia aliwarai vijana kukoma kutumiwa vibaya na wanasiasa kwa manufaa yao binafsi, akipongeza vuguvugu lilionzishwa na vijana la TUKO KADI kama njia moja ya kuwahamasisha vijana kujisajili kama wapiga kura.

“Tumeanza zoezi hili na tunawahimiza vijana wajitokeze kwa wingi na kujisajili kama wapiga kura ili kutumia nafasi hiyo kuchagua viongozi wanawataka na wala wasikubali kutumiwa vibaya na wanasiasa”, alisema Mohammed.

Kwa upande wao baadhi ya vijana waliojisajili waliwarai vijana wenzao kujitokeza kwa wingi na kushiriki zoezi hilo ili kuchagua viongozi wanaohisi wataleta maendeleo sawa na kubuni nafasi za ajira.

Taarifa ya Elizabeth Mwende

Continue Reading

Trending