Connect with us

News

Papa Francis Ameaga Dunia akiwa na Umri wa Miaka 88

Published

on

Kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani Papa Francis ameaga dunia akiwa na umri wa miaka 88.

Uongozi wa Kanisa Katoliki umethibitisha kifo chake na kusema kwamba Papa Francis ameaga dunia asubuhi siku ya Jumatatu ya Pasaka Aprili 21 katika makaazi yake katika Casa Santa Marta, Vatican.

Kadinali Kevin Farrell, Camerlengo Vatican amesema Kanisa Katoliki liko na huzuni kubwa kwa kumpoteza kiongozi huyo.

Kadinali Farrell amesisitiza umuhimu wa waumuni wa Kanisa Katoliki kuzingatia mafunzo ya Papa Francis ya utumishi kwa ajili ya Kanisa na kuthamini maisha ya utume.

Kadinali Farrell amehimiza ulimwengu kuzingatia uamunifu, ujasiri na upendo hasa kwa ajili ya maskini na wale waliotengwa jinsi Papa Francis alivyokuwa akihimiza ulimwengu.

Papa Francis alionekana mara ya mwisho akiwasalimia waumini wa Kanisa Katoliki wakati wa Ibada ya Misa ya Jumapili ya Pasaka katika Kanisa la St Peters Square mjini Rome na kuwahimiza waumini kuthamini ufufuko wa Yesu Kristu wakati wanapoadhimisha Pasaka.

Papa Franics hata hivyo alikuwa akiugua ugonjwa wa amonia ya mapafu na kulazwa kwa zaidi ya wiki tatu hospitalini na baadaye akarejea katika makaazi yake baada ya kupata nafuu kabla ya kuaga dunia siku ya Juamtatu, Aprili 21.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Polisi wanachunguza tukio la wizi dhidi ya raia wa kigeni

Published

on

By

Maafisa wa Polisi kaunti ya Mombasa wanachunguza tukio la wizi dhidi ya mtalii wa kigeni lililotokea katika eneo la Nyali

Kulingana na ripoti ya maafisa wa polisi, mtalii huyo mwenye umri wa miaka 51 ambaye ni raia wa Marekani, anadai kulaghaiwa na kisha kushambuliwa na kundi la wanaume aliyokutana nao muda mfupi kabla ya tukio.

Ripoti hiyo imeeleza kwamba mnamo mwezi Aprili 9 mwaka huu, raia huyo wa kigeni akiwa katika mkahawa mmoja eneo la Nyali jijini Mombasa, alikutana na mwanaume aliyejitambulisha kama Alex, ambaye alimshawishi kuelekea katika nyumba ya Airbnb iliyoko karibu na mkahawa huo.

Taarifa hiyo ilifafanua zaidi kwamba alipofika katika chumba hicho, alikumbana na wanaume wengine watano waliokuwa wakimsubiri ambapo mlango ulifungwa na kisha akashambuliwa na kulazimishwa kutoa pesa na vitu vya thamani.

Wahalifu hao walitoroka na mali mbalimbali ikiwemo simu ya rununu, kompyuta mpakato (laptop), fedha taslimu pamoja na fedha za kigeni na pia walifanikiwa kutoa pesa kutoka kwenye kadi zake za benki kwa njia ya udanganyifu.

Maafisa wa polisi kutoka Bamburi kwa kushirikiana na maafisa wa upelelezi wa DCI Nyali walifika eneo la tukio na kuanza uchunguzi, ingawa hadi sasa hakuna mtu aliyekamatwa wala mali iliyopatikana.

Kesi hiyo imewekwa chini ya uchunguzi zaidi huku juhudi zikiendelea kuwabaini na kuwakamata wahusika wa tukio hilo.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

News

Polisi eneo la Likoni-Mombasa inachunguza kifo cha mwanamke

Published

on

By

Idara ya usalama eneo la Likoni kaunti ya Mombasa imesema inachunguza kifo cha mwanamke mmoja aliyefariki katika mtaa wa senti kumi.

Mkuu wa polisi wa Likoni Joseph Mutungi alisema mwanamke huyo anadaiwa kupoteza maisha wakati wakiwa nyumbani kwa mwanamme anayesemekana kuwa mchumba wake.

Taarifa za awali ziliarifu kuwa marehemu alikuwa mgonjwa na anadaiwa alifika hospitalini kusaka matibabu japo hakupata huduma na kurejea nyumbani bila kutibiwa.

Inasemekana baadaye mchumba wake alioondoka kwenda kazini na kumwacha chini ya uangalizi wa mwanamke mwengine katika ploti hiyo.

Hali yake inadaiwa kuzorota na hatimaye kuaga dunia.

Maafisa wa usalama walisema wanaendelea na uchunguzi kubaini chanzo cha kifo hicho.

Mwili wa marehemu unahifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti katika hospitali ya Coast general kwa uchunguzi zaidi.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Trending