Connect with us

News

Papa Francis Ameaga Dunia akiwa na Umri wa Miaka 88

Published

on

Kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani Papa Francis ameaga dunia akiwa na umri wa miaka 88.

Uongozi wa Kanisa Katoliki umethibitisha kifo chake na kusema kwamba Papa Francis ameaga dunia asubuhi siku ya Jumatatu ya Pasaka Aprili 21 katika makaazi yake katika Casa Santa Marta, Vatican.

Kadinali Kevin Farrell, Camerlengo Vatican amesema Kanisa Katoliki liko na huzuni kubwa kwa kumpoteza kiongozi huyo.

Kadinali Farrell amesisitiza umuhimu wa waumuni wa Kanisa Katoliki kuzingatia mafunzo ya Papa Francis ya utumishi kwa ajili ya Kanisa na kuthamini maisha ya utume.

Kadinali Farrell amehimiza ulimwengu kuzingatia uamunifu, ujasiri na upendo hasa kwa ajili ya maskini na wale waliotengwa jinsi Papa Francis alivyokuwa akihimiza ulimwengu.

Papa Francis alionekana mara ya mwisho akiwasalimia waumini wa Kanisa Katoliki wakati wa Ibada ya Misa ya Jumapili ya Pasaka katika Kanisa la St Peters Square mjini Rome na kuwahimiza waumini kuthamini ufufuko wa Yesu Kristu wakati wanapoadhimisha Pasaka.

Papa Franics hata hivyo alikuwa akiugua ugonjwa wa amonia ya mapafu na kulazwa kwa zaidi ya wiki tatu hospitalini na baadaye akarejea katika makaazi yake baada ya kupata nafuu kabla ya kuaga dunia siku ya Juamtatu, Aprili 21.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending