Connect with us

News

Pigo kwa serikali baada ya Mahakama kuzuia kwa mda sheria ya kudhibiti mitandao

Published

on

Mahakama kuu imesitisha kwa mda sheria tata ya kudhibiti matumizi ya mtandao ya mwaka wa 2025 pamoja na matumizi mabaya ya kompyuta, iliyofanyiwa marekebisho bungeni na kutiwa saini na Rais William Ruto kuwa sheria, Oktoba 15.

Jaji wa Mahakam kuu ya Milimani Lawrence Mugambi, alitoa agizo hilo akisema kesi hiyo ina uzito na agizo hilo limetolewa ili kupeana nafasi ya kesi hiyo iliyowasilishwa Mahakamani na Mwanamziki wa injili Reuben Kigame na Tume ya haki za binadamu nchini KHRC, itakaposikizwa na kuamuliwa.

Walalamishi wa kesi hiyo, walidai kwamba vifungu vya sheria hiyo vinakiuka haki kadhaa za kikatiba, ikiwemo uhuru wa kujieleza, haki za kikatiba, utambulisho wa kidijitali usiojulikana na hatua za kiutawala za haki.

Katika hati kiapo cha kesi hiyo, walalamishi hao pia walidai kwamba sheria hiyo ina vipengele visivyoeleweka na kupita kiasi, ambayo vinaharamisha kujieleza mitandaoni na kudhohofisha sheria ya Kenya ya kulinda data 2019.

Walalamishi hao pia walionya kwamba hatua hizo zinatishia watetezi wa haki, Wanahabari na wakosoaji wa serikali, pamoja na kudhoofisha ulinzi uliowekwa chini ya sheria ya ulinzi ya taarifa za kibinafsi ya mwaka 2019.

Viongozi wa kidini hata hivyo walimkosoa rais Ruto kwa kutia saini sheria hiyo, wakisema itakandamiza uhuru wa kujieleza, kuondoa maudhui yaliyoangaziwa kwenye mtandao hasa inayokosoa serikali pamoja na kukosoa adhabu ambayo ilitolewa na serikali ya faini ya shilingi milioni 20 ama kifungo cha miaka 10 gerezani.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Polisi wanachunguza tukio la wizi dhidi ya raia wa kigeni

Published

on

By

Maafisa wa Polisi kaunti ya Mombasa wanachunguza tukio la wizi dhidi ya mtalii wa kigeni lililotokea katika eneo la Nyali

Kulingana na ripoti ya maafisa wa polisi, mtalii huyo mwenye umri wa miaka 51 ambaye ni raia wa Marekani, anadai kulaghaiwa na kisha kushambuliwa na kundi la wanaume aliyokutana nao muda mfupi kabla ya tukio.

Ripoti hiyo imeeleza kwamba mnamo mwezi Aprili 9 mwaka huu, raia huyo wa kigeni akiwa katika mkahawa mmoja eneo la Nyali jijini Mombasa, alikutana na mwanaume aliyejitambulisha kama Alex, ambaye alimshawishi kuelekea katika nyumba ya Airbnb iliyoko karibu na mkahawa huo.

Taarifa hiyo ilifafanua zaidi kwamba alipofika katika chumba hicho, alikumbana na wanaume wengine watano waliokuwa wakimsubiri ambapo mlango ulifungwa na kisha akashambuliwa na kulazimishwa kutoa pesa na vitu vya thamani.

Wahalifu hao walitoroka na mali mbalimbali ikiwemo simu ya rununu, kompyuta mpakato (laptop), fedha taslimu pamoja na fedha za kigeni na pia walifanikiwa kutoa pesa kutoka kwenye kadi zake za benki kwa njia ya udanganyifu.

Maafisa wa polisi kutoka Bamburi kwa kushirikiana na maafisa wa upelelezi wa DCI Nyali walifika eneo la tukio na kuanza uchunguzi, ingawa hadi sasa hakuna mtu aliyekamatwa wala mali iliyopatikana.

Kesi hiyo imewekwa chini ya uchunguzi zaidi huku juhudi zikiendelea kuwabaini na kuwakamata wahusika wa tukio hilo.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

News

Polisi eneo la Likoni-Mombasa inachunguza kifo cha mwanamke

Published

on

By

Idara ya usalama eneo la Likoni kaunti ya Mombasa imesema inachunguza kifo cha mwanamke mmoja aliyefariki katika mtaa wa senti kumi.

Mkuu wa polisi wa Likoni Joseph Mutungi alisema mwanamke huyo anadaiwa kupoteza maisha wakati wakiwa nyumbani kwa mwanamme anayesemekana kuwa mchumba wake.

Taarifa za awali ziliarifu kuwa marehemu alikuwa mgonjwa na anadaiwa alifika hospitalini kusaka matibabu japo hakupata huduma na kurejea nyumbani bila kutibiwa.

Inasemekana baadaye mchumba wake alioondoka kwenda kazini na kumwacha chini ya uangalizi wa mwanamke mwengine katika ploti hiyo.

Hali yake inadaiwa kuzorota na hatimaye kuaga dunia.

Maafisa wa usalama walisema wanaendelea na uchunguzi kubaini chanzo cha kifo hicho.

Mwili wa marehemu unahifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti katika hospitali ya Coast general kwa uchunguzi zaidi.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Trending