Connect with us

News

Pigo kwa serikali baada ya Mahakama kuzuia kwa mda sheria ya kudhibiti mitandao

Published

on

Mahakama kuu imesitisha kwa mda sheria tata ya kudhibiti matumizi ya mtandao ya mwaka wa 2025 pamoja na matumizi mabaya ya kompyuta, iliyofanyiwa marekebisho bungeni na kutiwa saini na Rais William Ruto kuwa sheria, Oktoba 15.

Jaji wa Mahakam kuu ya Milimani Lawrence Mugambi, alitoa agizo hilo akisema kesi hiyo ina uzito na agizo hilo limetolewa ili kupeana nafasi ya kesi hiyo iliyowasilishwa Mahakamani na Mwanamziki wa injili Reuben Kigame na Tume ya haki za binadamu nchini KHRC, itakaposikizwa na kuamuliwa.

Walalamishi wa kesi hiyo, walidai kwamba vifungu vya sheria hiyo vinakiuka haki kadhaa za kikatiba, ikiwemo uhuru wa kujieleza, haki za kikatiba, utambulisho wa kidijitali usiojulikana na hatua za kiutawala za haki.

Katika hati kiapo cha kesi hiyo, walalamishi hao pia walidai kwamba sheria hiyo ina vipengele visivyoeleweka na kupita kiasi, ambayo vinaharamisha kujieleza mitandaoni na kudhohofisha sheria ya Kenya ya kulinda data 2019.

Walalamishi hao pia walionya kwamba hatua hizo zinatishia watetezi wa haki, Wanahabari na wakosoaji wa serikali, pamoja na kudhoofisha ulinzi uliowekwa chini ya sheria ya ulinzi ya taarifa za kibinafsi ya mwaka 2019.

Viongozi wa kidini hata hivyo walimkosoa rais Ruto kwa kutia saini sheria hiyo, wakisema itakandamiza uhuru wa kujieleza, kuondoa maudhui yaliyoangaziwa kwenye mtandao hasa inayokosoa serikali pamoja na kukosoa adhabu ambayo ilitolewa na serikali ya faini ya shilingi milioni 20 ama kifungo cha miaka 10 gerezani.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending