Sports
Rais Awahidi Basi Mpya Mabingwa Wa Ligi Kuu Police
Rais William Samoei Ruto ameahidi kununulia basi jipya Mabingwa wapya wa ligi kuu FKF PL Kenya Police kwa kazi kuntu waliofanya msimu huu.
Rais alitoa ahadi hiyo wakati wa kikao cha chakula cha asubuhi baada ya mwaliko ikuluni mapema leo ambapo aliweza kupongeza timu hiyo akiahidi pia atatembea nao msimu ujao katika juhudi zao za kueteta ligi hiyo ya taifa.
“Kama wachezaji na wanaspoti nichukua fursa hii kuwahukuru kwa kazi nzuri tutazidi kuwashika mkono nimeambiwa mnahitaji basi nzuri ,Nitawatafutia Basi nzuri kwa majukumu ya usafiri.”
Kwa upande wake Waziri wa Michezo Salim Mvurya amefichua kwamba hivi karibuni Wizara yake litazindua taji la Rais marufu kama Presidents Cup ambalo litaanza mashinani hadi kwneye taifa na kuanzishwa na rais mwenyewe.
Entertainment
Arsenal Ikishinda Kombe Nitampa Main Man Rio Gari na Dadangu – Shuga Boy
Mjadala mkali umeibuka katika kipindi cha COCO Asubuhi baada ya Shuga Boy, shabiki wa Manchester United, kuweka dau zito na la kushangaza dhidi ya Main Man Rio ambaye ni shabiki wa Arsenal.
Akizungumza kwenye kipindi cha COCO Asubuhi, kinachoendeshwa na Tatu Sure—inayojumuisha Shuga Boy mwenyewe, Main Man Rio na Solomon Zully—Shuga Boy alifunguka, akidai kuwa Arsenal hawana uwezo wa kubeba hata kombe moja msimu huu licha ya matarajio makubwa kutoka kwa mashabiki wao.
Kwa mujibu wa Shuga Boy, mashabiki wa Arsenal wamekuwa wakijipa matumaini makubwa ya kutwaa hadi vikombe vinne, lakini hali halisi uwanjani haioneshi dalili hizo. Alienda mbali zaidi na kuweka dau la kipekee kwa Main Man Rio, ambaye ni shabiki mkubwa wa Arsenal.
“Nilimwambia Main Man Rio, wakibeba kombe nitampa gari yangu. Sasa naongeza dau—wakishinda kikombe msimu huu, nitampa gari yangu pamoja na dadangu,” alisema Shuga Boy kwa msisitizo, kauli iliyozua kicheko na mjadala mkali studio.
Kauli hiyo imekuja katika kipindi ambacho Arsenal wamekuwa wakionyesha ushindani mkubwa chini ya kocha Mikel Arteta, wakijijenga kama moja ya timu zinazowania ubingwa wa Premier League. Licha ya maendeleo hayo, ukosefu wa vikombe katika misimu mingi bado unawapa wapinzani wao nafasi ya kuwabeza.
Kwa upande mwingine, Manchester United nao wanapitia kipindi cha mabadiliko, wakijaribu kurejea kwenye ubora wao wa zamani waliouonyesha enzi za Sir Alex Ferguson. Licha ya changamoto, bado wana historia nzito ya mafanikio, jambo linalowapa mashabiki wao kujiamini wanapojadili soka la Uingereza.
Usiku wa leo, macho ya mashabiki yataelekezwa kwenye mchezo wa ligi kati ya Manchester United dhidi ya Leeds United—mchezo unaotarajiwa kuwa na ushindani mkali, huku Shuga Boy akitumaini timu yake itapata ushindi na kuendeleza presha kwa wapinzani wao.
Wakati mabishano yakiendelea mitandaoni na kwenye studio za redio, swali kubwa linabaki: Je, Arsenal wataweza kuwanyamazisha wakosoaji wao kwa kubeba angalau kombe moja msimu huu, au kauli ya Shuga Boy itageuka kuwa unabii?

