Sports
Rashford Kujiunga na Barcelona Kuimarisha Safu ya Ushambuliaji
Mchezaji nyota wa Manchester United, Marcus Rashford, sasa yupo sokoni na anapatikana kwa vilabu vyote kwa ada ya uhamisho ya takriban pauni milioni 40.
Tetesi zinasema kwamba, klabu ya Barcelona bado inaendelea kumfuatilia mshambuliaji huyo, ikiwa ni mwendelezo wa nia waliyoonyesha tangu mwezi Januari mwaka huu.
Hapo awali, dili hilo halikukamilika kutokana na kutokuwepo kwa uuzwaji wa mchezaji mwingine ambaye angewezesha uhamisho huo.
Hivi karibuni, mwandishi wa soka Toni Juanmartí (@tjuanmarti) ameripoti kuwa wawakilishi wa Rashford wamekutana tena na viongozi wa Barcelona kwa mazungumzo zaidi kuhusu uwezekano wa uhamisho huo.
Rashford ametajwa kuwa miongoni mwa wachezaji wanne waliopo kwenye orodha ya Barcelona, wanaochunguzwa kwa ajili ya kuimarisha kikosi hicho msimu ujao.
Ingawa bado hakuna uthibitisho rasmi kuhusu mafanikio ya mazungumzo hayo, uwezekano wa Rashford kujiunga na Barcelona bado upo wazi.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

