Connect with us

Business

CBK: Bei za bidhaa za chakula zaendelea kupanda

Published

on

Utafiti wa hivi karibuni uliofanywa na Benki Kuu ya Kenya (CBK) katika sekta ya Kilimo umebainisha kuwa kuna ongezeko la bei ya bidhaa muhimu za chakula, ikiwemo Mahindi, Sukari, na Mafuta ya kupikia.

Ripoti hiyo ilionyesha kuwa mabadiliko haya ya bei yanachochewa na sababu mbalimbali za kitaifa na kimataifa, zenye athari kubwa kwa walaji wa kawaida na sekta ya biashara kwa ujumla.

Kwa mujibu wa CBK, bei ya Mahindi imekuwa ikiongezeka tangu wiki za mwisho za mwezi Mei.

Hali hii imepelekea ongezeko la bei ya paketi ya kilo 2 ya unga wa Mahindi kwa wastani wa shilingi 6, hatua ambayo wasagaji wa unga wa Mahindi wameitaja kuwa imesababishwa na uhaba wa Mahindi sokoni.

Kukabiliana na changamoto hiyo, Wizara ya Kilimo nchini imeingilia kati kwa kusambaza magunia laki mbili ya Mahindi kwa wasagaji mbalimbali kote nchini, ili kusaidia kudhibiti bei na kuhakikisha upatikanaji wa unga kwa wananchi kwa gharama nafuu zaidi.

Wakati huo huo, bei ya sukari na mafuta ya kupikia pia inatarajiwa kuendelea kupanda.

Ongezeko hili linahusishwa na mabadiliko ya bei katika masoko ya kimataifa, hasa kutokana na kupungua kwa uzalishaji katika baadhi ya nchi zinazouza bidhaa hizo kwa wingi, pamoja na gharama za usafirishaji zinazoendelea kuongezeka.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Business

Bei za mafuta kuongezeka katikati ya mwezi aprili

Published

on

By

Kenya sasa inakabiliwa na hatari ya kupanda kwa bei za mafuta, huku mgogoro unaoendelea mashariki ya Kati ukianza kuathiri bei nchini.

Serikali sasa imeonya kuwa kufikia katikati ya mwezi Aprili, bei za mafuta huenda zikapanda ikionya kuwa ongezeko la bei ya mafuta kwa sasa haliwezi kuepukika kufuatia kupanda kwa bei za mafuta kimataifa.

Waziri wa hazina kuu ya kitaifa John Mbadi aliwahakikishia wakenya kuwa hakuna cha kuhofia kwani wameweka mikakati kupunguza athari zake.

Ili kupunguza athari za bei za mafuta kuongezeka, serikali ilisema itatumia shilingi bilioni 17 kutoka mfuko wa ada ya uwekezaji wa mafuta kusaidia kudhibiti bei kwa mda wa miezi 3 ijayo.

Kwa sasa serikali inasema kuna akiba ya kutosha ya mafuta na shehena zaidi zinatarajiwa nchini hivi karibuni.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

Business

KPA yaimarisha usafirishaji wa makasha na kampeni za kimataifa

Published

on

By

Halmashauri ya bandari nchini (KPA), imeimarisha ushirikiano wake na kampuni ya kimataifa ya usafirishaji kwa njia ya bahari, Maersk, katika juhudi za kuboresha huduma na kuongeza ufanisi wa usafirishaji wa mizigo katika eneo la Afrika Mashariki.

Makubaliano hayo yameafikiwa katika mkutano uliofanyika katika makao makuu ya KPA jijini Mombasa ambapo Mkurugenzi wa Maersk Kanda ya Afrika Mashariki, Tito Okuku, alieleza kuwa kampuni hiyo ina nia ya kupanua shughuli zake zaidi nchini na katika eneo la Afrika Mashariki kwa ujumla.

Moja ya maeneo yatakayopata kipaumbele ni kuimarisha matumizi ya Kituo cha Makontena cha ndani cha Naivasha kinachotazamwa kama kitovu muhimu katika kushughulikia usafirishaji wa mazao ya kilimo kutoka Kenya kwenda masoko ya kimataifa, huku kikitoa njia ya haraka na ya kuaminika kwa wauzaji kufikia masoko ya kimataifa.

Mkurugenzi Mkuu wa KPA, Nahodha William Ruto, alieleza kukubaliana na hatua hiyo akisema ni wakati mwafaka kwa pande zote mbili kuimarisha ushirikiano huo.

Aidha alibainisha kuwa Bandari ya Mombasa pamoja na vituo vyake vya ndani vinaendelea kushuhudia ongezeko la shehena, na akahakikishia kuwa KPA iko tayari kushughulikia mahitaji yanayoongezeka kupitia maboresho ya miundombinu na huduma.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Trending