Connect with us

News

Serikali kuongeza mshahara wa maafisa wa polisi kwa asilimia 40

Published

on

Katibu katika Wizara ya usalama wa ndani Raymond Omollo ametangaza nyongeza ya asilimia 40 kwa mishahara ya maafisa wa polisi ambayo itaanza kutekelezwa mwezi Julai mwaka huu.

Omollo ambaye anaongoza Kamati maalum ya kuangazia mishahara na marupurupu ya maafisa wa polisi nchini, alisema pendekezo lililowasilishwa kwa hazina ya kitaifa, afisa wa kiwango cha chini kabisa wa polisi atapokea shilingi 57, 700 kutoka shilingi 38,975.

Pendekezo hilo pia linataka afisa wa chini kabisa wa idara ya magereza kupokea kiwango cha shilingi 57,700 huku Afisa wa polisi aliyefuzu kutoka chuo cha Kiganjo akipendekezwa kupokea mshahara wa shilingi 29,296 kutoka shilingi 20,390.

Hata hivyo afisi wa kiwango cha chini kabisa kutoka Shirika la huduma kwa vijana wa taifa NYS atapokea mshahara wa shilingi elfu 26 huku afisa wa NYS wajuu zaidi akipokea mshahara wa shilingi elfu 37.

Pendekezo hilo pia limeafikia kwamba maafisa wa polisi wa ngazi ya juu zaidi watalipwa kati ya shilingi 301,548 na shilingi 584,903 ikiwa ni nyongeza ya asilimia ya juu zaidi.

Wakati huo huo Inspekta Jenerali wa Polisi nchini Douglas Kenja amesema hatua hiyo inalenga kuhakikisha maafisa wa polisi wanatekeleza majukumu yao vyema huku Afisa mkuu mtendaji wa Tume ya maadili na kupambana na ufisadi nchini EACC Abdi Ahmed Mohamud akiwarai maafisa wa polisi kujiepusha na ufisadi.

Taraifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Ethekon: Uchaguzi mkuu utakuwa huru, haki na uwazi

Published

on

By

Tume huru ya uchaguzi na mipaka nchini IEBC imeanza rasmi zoezi la kuwasajili wapiga kura wapya kote nchini, huku ikilenga kuwasajili wapiga kura milioni 6.2, kabla ya uchaguzi mkuu ujao. 

Mwenyekiti wa Tume hiyo Erastus Ethekon aliwahakikishia wakenya kwamba makamishna wa tume hiyo watahakikisha uchuguzi mkuu ujao unakuwa huru, haki na uwazi.

Akizungumza katika kaunti ya Kwale wakati wa kuzindua wa zoezi la usajili wa wakipiga kura kote nchini, Ethekon alisema serikali imewekeza raslimali za kutosha za kufanikisha zoezi hilo.

“Nataka kuwahakikishia wakenya kwamba tumejipanga kama IEBC na tuko na raslimali za kutosha kuhakikisha zoezi la usajili wa wapiga kura linaendeshwa vyema na uchaguzi mkuu utakuwa huru, haki na wazi ili kuhakikisha wakenya wanatekeleza jukumu lao la kidemokrasia na hatua hiyo tutafikia idadi ya wapiga kura zaidi ya milioni 27”, alisema Ethekon.

Naye Naibu Mwenyekiti wa IEBC Fahima Araphat alisema tayari maafisa wapya wa IEBC elfu 12 wameajiriwa kuhakikisha zoezi hilo liendeshwa vyema ili kusajili idadi kubwa ya wapiga kura

“Sisi tunafanya kazi yetu bila kuegemea upande wowote wa kisiasa na tuko tayari kuhakikisha anashinda uchaguzi anatangazwa mshindi kwa haki, na kama tuko na makarani elfu 12 na wote wasajili wapiga kura wapya elfu 10 kila moja tutakuwa na idadi kubwa ya wapiga kura, sasa hiyo ndio tunalenga kupata”, alisema Fahima.

Kwa upande wake Gavana wa kaunti ya Kwale Fatuma Achani, aliipongeza tume hiyo kwa zoezi hilo endelevu la wapiga kura, akisema ni hatua ya kipekee kwa jamii ambazo zimekosa fursa ya kujisajili kama wapiga kura.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

News

IEBC yasema idadi ya wanaojisajili ni ndogo mno

Published

on

By

Zoezi endelevu la usajili wa wapiga kura kote nchini limeng’oa nanga huku maafisa wa Tume huru ya uchaguzi na mipaka nchini IEBC wakilenga idadi kubwa ya vijana katika zoezi hilo.

Katika kaunti ya Kilifi eneo bunge la Kilifi Kazkazini, zoezi hilo limefanyika katika vituo vinne tofauti huku idadi ndogo ya wapiga kura ikishuhudiwa licha ya vuguvugu la TUKO KADI kuanzishwa na vijana ili kuwajisajili wapiga kura.

Akizungumza na Wanahabari wakati wa zoezi hilo, Naibu Afisa wa usajili wa wapiga kura katika eneo bunge la Kilifi Kazkazini Abdul Mohammed aliwarai vijana kujitokeza kwa wingi na kujisajili.

Mohammed pia aliwarai vijana kukoma kutumiwa vibaya na wanasiasa kwa manufaa yao binafsi, akipongeza vuguvugu lilionzishwa na vijana la TUKO KADI kama njia moja ya kuwahamasisha vijana kujisajili kama wapiga kura.

“Tumeanza zoezi hili na tunawahimiza vijana wajitokeze kwa wingi na kujisajili kama wapiga kura ili kutumia nafasi hiyo kuchagua viongozi wanawataka na wala wasikubali kutumiwa vibaya na wanasiasa”, alisema Mohammed.

Kwa upande wao baadhi ya vijana waliojisajili waliwarai vijana wenzao kujitokeza kwa wingi na kushiriki zoezi hilo ili kuchagua viongozi wanaohisi wataleta maendeleo sawa na kubuni nafasi za ajira.

Taarifa ya Elizabeth Mwende

Continue Reading

Trending