News
Serikali kuongeza mshahara wa maafisa wa polisi kwa asilimia 40
Katibu katika Wizara ya usalama wa ndani Raymond Omollo ametangaza nyongeza ya asilimia 40 kwa mishahara ya maafisa wa polisi ambayo itaanza kutekelezwa mwezi Julai mwaka huu.
Omollo ambaye anaongoza Kamati maalum ya kuangazia mishahara na marupurupu ya maafisa wa polisi nchini, alisema pendekezo lililowasilishwa kwa hazina ya kitaifa, afisa wa kiwango cha chini kabisa wa polisi atapokea shilingi 57, 700 kutoka shilingi 38,975.
Pendekezo hilo pia linataka afisa wa chini kabisa wa idara ya magereza kupokea kiwango cha shilingi 57,700 huku Afisa wa polisi aliyefuzu kutoka chuo cha Kiganjo akipendekezwa kupokea mshahara wa shilingi 29,296 kutoka shilingi 20,390.
Hata hivyo afisi wa kiwango cha chini kabisa kutoka Shirika la huduma kwa vijana wa taifa NYS atapokea mshahara wa shilingi elfu 26 huku afisa wa NYS wajuu zaidi akipokea mshahara wa shilingi elfu 37.
Pendekezo hilo pia limeafikia kwamba maafisa wa polisi wa ngazi ya juu zaidi watalipwa kati ya shilingi 301,548 na shilingi 584,903 ikiwa ni nyongeza ya asilimia ya juu zaidi.
Wakati huo huo Inspekta Jenerali wa Polisi nchini Douglas Kenja amesema hatua hiyo inalenga kuhakikisha maafisa wa polisi wanatekeleza majukumu yao vyema huku Afisa mkuu mtendaji wa Tume ya maadili na kupambana na ufisadi nchini EACC Abdi Ahmed Mohamud akiwarai maafisa wa polisi kujiepusha na ufisadi.
Taraifa ya Mwahoka Mtsumi
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

