Connect with us

News

Siasa za migawanyiko za tawala kampeni za uchaguzi mdogo Magarini

Published

on

Viongozi wa chama cha ODM wamekita kambi katika eneo bunge la Magarini kaunti ya Kilifi kwa ajili ya kumpigia debe Harrison Garama Kombe anayewania kiti cha ubunge kwenye uchaguzi mdogo ulioratibiwa kufanyika Novemba 27, 2025.

Viongozi hao waliendesha kampeni zao eneo la Garashi kisha kukamilisha na Marafa wakiwaahidi wakaazi wa Magarini kunufaika kimaendeleo iwapo watamchagua Kombe wakati wa uchaguzi huo.

Wakiongozwa na mwenyekiti wa kitaifa wa chama cha ODM Gladys Wanga ambaye pia ni gavana wa kaunti ya Homabay na naibu kinara wa chama hicho Abdhulswamad Sharrif Nassir, viongozi hao walielekeza lawama kwa viongozi wa upinzani, wakisema wanaendeleza siasa za ukabila na migawanyiko.

Viongozi hao walisema chama cha ODM kinaendeleza sera za mwanzilishi wake hayati Raila Odinga za kuunganisha wakenya pamoja, wakisistiza kutoruhusu viongozi wa upinzani kupata tope chama hicho.

Hata hivyo semi za viongozi hao zilionekana kumlenga moja kwa moja kinara wa chama cha DCP Rigathi Gachagua.

Kwa upande wake seneta wa kaunti ya Kilifi Stewart Madzayo, alimtaka rais William Ruto kuhakikisha anatekeleza maagizo ya ajenda 10 walizoafikiana na hayati Raila Odinga, wakati wa kutiwa saini mkataba wa serikali jumuishi, wakisema wataendelea kusalia ndani ya serikali kwa manufaa ya mwananchi.

Gavana wa kaunti ya Kilifi Gideon Mung’aro akimpigia debe Harrison Kombe(Picha kwa hisani)

Vile vile viongozi hao waliwarai wakaazi wa Magarini kumuunga mkono mgombea wao Harrison Kombe wakati wa uchaguzi huo mdogo, wakisema hatua hiyo itamwezesha kukamilisha miradi ya maendelea aliyokuwa ameianzisha.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Polisi wanachunguza tukio la wizi dhidi ya raia wa kigeni

Published

on

By

Maafisa wa Polisi kaunti ya Mombasa wanachunguza tukio la wizi dhidi ya mtalii wa kigeni lililotokea katika eneo la Nyali

Kulingana na ripoti ya maafisa wa polisi, mtalii huyo mwenye umri wa miaka 51 ambaye ni raia wa Marekani, anadai kulaghaiwa na kisha kushambuliwa na kundi la wanaume aliyokutana nao muda mfupi kabla ya tukio.

Ripoti hiyo imeeleza kwamba mnamo mwezi Aprili 9 mwaka huu, raia huyo wa kigeni akiwa katika mkahawa mmoja eneo la Nyali jijini Mombasa, alikutana na mwanaume aliyejitambulisha kama Alex, ambaye alimshawishi kuelekea katika nyumba ya Airbnb iliyoko karibu na mkahawa huo.

Taarifa hiyo ilifafanua zaidi kwamba alipofika katika chumba hicho, alikumbana na wanaume wengine watano waliokuwa wakimsubiri ambapo mlango ulifungwa na kisha akashambuliwa na kulazimishwa kutoa pesa na vitu vya thamani.

Wahalifu hao walitoroka na mali mbalimbali ikiwemo simu ya rununu, kompyuta mpakato (laptop), fedha taslimu pamoja na fedha za kigeni na pia walifanikiwa kutoa pesa kutoka kwenye kadi zake za benki kwa njia ya udanganyifu.

Maafisa wa polisi kutoka Bamburi kwa kushirikiana na maafisa wa upelelezi wa DCI Nyali walifika eneo la tukio na kuanza uchunguzi, ingawa hadi sasa hakuna mtu aliyekamatwa wala mali iliyopatikana.

Kesi hiyo imewekwa chini ya uchunguzi zaidi huku juhudi zikiendelea kuwabaini na kuwakamata wahusika wa tukio hilo.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

News

Polisi eneo la Likoni-Mombasa inachunguza kifo cha mwanamke

Published

on

By

Idara ya usalama eneo la Likoni kaunti ya Mombasa imesema inachunguza kifo cha mwanamke mmoja aliyefariki katika mtaa wa senti kumi.

Mkuu wa polisi wa Likoni Joseph Mutungi alisema mwanamke huyo anadaiwa kupoteza maisha wakati wakiwa nyumbani kwa mwanamme anayesemekana kuwa mchumba wake.

Taarifa za awali ziliarifu kuwa marehemu alikuwa mgonjwa na anadaiwa alifika hospitalini kusaka matibabu japo hakupata huduma na kurejea nyumbani bila kutibiwa.

Inasemekana baadaye mchumba wake alioondoka kwenda kazini na kumwacha chini ya uangalizi wa mwanamke mwengine katika ploti hiyo.

Hali yake inadaiwa kuzorota na hatimaye kuaga dunia.

Maafisa wa usalama walisema wanaendelea na uchunguzi kubaini chanzo cha kifo hicho.

Mwili wa marehemu unahifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti katika hospitali ya Coast general kwa uchunguzi zaidi.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Trending