Connect with us

News

Siasa za migawanyiko za tawala kampeni za uchaguzi mdogo Magarini

Published

on

Viongozi wa chama cha ODM wamekita kambi katika eneo bunge la Magarini kaunti ya Kilifi kwa ajili ya kumpigia debe Harrison Garama Kombe anayewania kiti cha ubunge kwenye uchaguzi mdogo ulioratibiwa kufanyika Novemba 27, 2025.

Viongozi hao waliendesha kampeni zao eneo la Garashi kisha kukamilisha na Marafa wakiwaahidi wakaazi wa Magarini kunufaika kimaendeleo iwapo watamchagua Kombe wakati wa uchaguzi huo.

Wakiongozwa na mwenyekiti wa kitaifa wa chama cha ODM Gladys Wanga ambaye pia ni gavana wa kaunti ya Homabay na naibu kinara wa chama hicho Abdhulswamad Sharrif Nassir, viongozi hao walielekeza lawama kwa viongozi wa upinzani, wakisema wanaendeleza siasa za ukabila na migawanyiko.

Viongozi hao walisema chama cha ODM kinaendeleza sera za mwanzilishi wake hayati Raila Odinga za kuunganisha wakenya pamoja, wakisistiza kutoruhusu viongozi wa upinzani kupata tope chama hicho.

Hata hivyo semi za viongozi hao zilionekana kumlenga moja kwa moja kinara wa chama cha DCP Rigathi Gachagua.

Kwa upande wake seneta wa kaunti ya Kilifi Stewart Madzayo, alimtaka rais William Ruto kuhakikisha anatekeleza maagizo ya ajenda 10 walizoafikiana na hayati Raila Odinga, wakati wa kutiwa saini mkataba wa serikali jumuishi, wakisema wataendelea kusalia ndani ya serikali kwa manufaa ya mwananchi.

Gavana wa kaunti ya Kilifi Gideon Mung’aro akimpigia debe Harrison Kombe(Picha kwa hisani)

Vile vile viongozi hao waliwarai wakaazi wa Magarini kumuunga mkono mgombea wao Harrison Kombe wakati wa uchaguzi huo mdogo, wakisema hatua hiyo itamwezesha kukamilisha miradi ya maendelea aliyokuwa ameianzisha.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending