Connect with us

News

Siasa za migawanyiko za tawala kampeni za uchaguzi mdogo Magarini

Published

on

Viongozi wa chama cha ODM wamekita kambi katika eneo bunge la Magarini kaunti ya Kilifi kwa ajili ya kumpigia debe Harrison Garama Kombe anayewania kiti cha ubunge kwenye uchaguzi mdogo ulioratibiwa kufanyika Novemba 27, 2025.

Viongozi hao waliendesha kampeni zao eneo la Garashi kisha kukamilisha na Marafa wakiwaahidi wakaazi wa Magarini kunufaika kimaendeleo iwapo watamchagua Kombe wakati wa uchaguzi huo.

Wakiongozwa na mwenyekiti wa kitaifa wa chama cha ODM Gladys Wanga ambaye pia ni gavana wa kaunti ya Homabay na naibu kinara wa chama hicho Abdhulswamad Sharrif Nassir, viongozi hao walielekeza lawama kwa viongozi wa upinzani, wakisema wanaendeleza siasa za ukabila na migawanyiko.

Viongozi hao walisema chama cha ODM kinaendeleza sera za mwanzilishi wake hayati Raila Odinga za kuunganisha wakenya pamoja, wakisistiza kutoruhusu viongozi wa upinzani kupata tope chama hicho.

Hata hivyo semi za viongozi hao zilionekana kumlenga moja kwa moja kinara wa chama cha DCP Rigathi Gachagua.

Kwa upande wake seneta wa kaunti ya Kilifi Stewart Madzayo, alimtaka rais William Ruto kuhakikisha anatekeleza maagizo ya ajenda 10 walizoafikiana na hayati Raila Odinga, wakati wa kutiwa saini mkataba wa serikali jumuishi, wakisema wataendelea kusalia ndani ya serikali kwa manufaa ya mwananchi.

Gavana wa kaunti ya Kilifi Gideon Mung’aro akimpigia debe Harrison Kombe(Picha kwa hisani)

Vile vile viongozi hao waliwarai wakaazi wa Magarini kumuunga mkono mgombea wao Harrison Kombe wakati wa uchaguzi huo mdogo, wakisema hatua hiyo itamwezesha kukamilisha miradi ya maendelea aliyokuwa ameianzisha.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Rais Ruto atia saini kuwa sheria mswada wa hazina ya taifa ya uwekezaji wa mali

Published

on

By

Rais William Ruto ametia saini kuwa sheria mswada wa hazina ya kitaifa ya uwekezaji wa mali (Sovereign Wealth Fund), hatua inayotajwa kuwa muhimu katika juhudi za Kenya za kuimarisha usimamizi wa fedha za umma, kulinda utajiri wa taifa na kuchochea ukuaji wa uchumi wa muda mrefu.

Utiaji huo wa saini ulifanyika katika Ikulu ya Nairobi na unaweka msingi wa kisheria wa kuanzishwa na kusimamiwa kwa mfuko wa taifa wa uwekezaji wa mali na kwamba unatarajiwa kuiwezesha nchi kuhifadhi rasilimali za umma zinazobaki baada ya matumizi ya kawaida, kufadhili uwekezaji wa kimkakati na kuimarisha uwezo wa uchumi kukabiliana na misukosuko ya kifedha siku zijazo.

Sheria hiyo mpya inaleta mfumo rasmi wa usimamizi wa utajiri wa taifa kwa kutenga akiba kwa ajili ya vizazi vijavyo, kuimarisha uthabiti wa uchumi na kufadhili uwekezaji katika miundombinu ya kimkakati ili kuongeza uimara wa kifedha nchini pamoja na kuhimiza matumizi yenye uwajibikaji ya rasilimali za umma.

Mfuko huo utatumika kuwekeza mapato ya ziada yanayotokana na rasilimali za asili na mali nyingine za umma, kwa lengo la kuhakikisha manufaa yake yanawanufaisha wananchi wa sasa na vizazi vijavyo.

Aidha, mfuko huo unakusudia kupunguza athari za changamoto za kiuchumi kwa kutoa kinga ya kifedha wakati wa misukosuko ya uchumi.

Sheria hiyo ni sehemu ya ajenda pana ya serikali ya mageuzi ya uchumi inayolenga kuimarisha usimamizi wa fedha za umma, kuongeza uwazi na kuendeleza maendeleo endelevu.

Pia, sheria hiyo imeweka mfumo wa uongozi na usimamizi wa mfuko huo, ukiwemo utaratibu wa kuhakikisha uwajibikaji, uwazi na usimamizi madhubuti katika uwekezaji na matumizi ya rasilimali za umma.

Maafisa wa serikali wameeleza kuwa Mfuko wa Taifa wa Uwekezaji wa Mali utakuwa na mchango mkubwa katika kufadhili miradi ya maendeleo yenye kipaumbele nchini huku ukihifadhi utajiri wa taifa kwa manufaa ya vizazi vijavyo.

Kupitishwa kwa sheria hiyo kunaiweka Kenya miongoni mwa mataifa yanayoongezeka duniani ambayo yameanzisha mifuko ya taifa ya uwekezaji wa mali kwa lengo la kulinda mali za taifa, kuimarisha uthabiti wa uchumi na kufadhili malengo ya maendeleo ya muda mrefu.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

News

IEBC yakosolewa dhidi ya masharti mapya iliyotoa kwa wanasiasa

Published

on

By

Kiongozi wa vijana katika Chama cha Wiper kaunti ya Kwale Nyawa Masai ameikosoa Tume huru ya uchaguzi na mipaka nchini IEBC kutokana na masharti mapya iliyotoa dhidi ya wanasaisa kabla ya uchaguzi mkuu ujao.

Nyawa ameitaka Tume hiyo kuzingatia kanuni zake na taratibu za kuandaa uchaguzi na wala sio kila uchao kutoa masharti ambayo yanakinzana na majukumu ya Tume, akisema kuna taasisi zengine za umma zinafaa kuwajibika.

Akizungumza katika mkutano wa kisiasa katika eneo la Mwereni gatuzi dogo la Lungalunga kaunti ya Kwale, Nyawa aliesisitiza haja ya wanasiasa kupewa nafasi ya kuzungumza na wananchi sawa na kueleza sera zao bila ya vizuizi.

Kiongozi huyo wa vijana ambaye alitangaza nia yake ya kuwania kiti cha uwakilishi wadi ya Mwereni wakati wa uchaguzi ujao, amesema taifa la Kenya linazingatia demokrasia na kwamba kila taasisi inafaa kutekeleza majukumu yake.

“Katika uwaja wa siasa IEBC inakuzi moja tu kama msimamizi na kama msimamizi anaanza kutengeza sheria hapo ndipo anakosea, hii Kneya ni nchi ya demokrasia kwa hivyo IEBC isilete sheria nyingi na kufuatilia wanasiasa kuhusu pesa watatumia kwa kampeni, hiyo sio jukumu lake kuna taasisi inaitwa EACC”, alisema Nyawa.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Trending