Sports
Tiketi za Stars Hazikuuzwa Zote
Rais wa FKF Hussein Mohamed amesema kwamba shirikisho hilo lilipata shilingi milioni 6.9 na wala si milioni 9.1 kama ilivyoripotiwa mechi ya Harambee stars dhidi ya Gabon Jumapili.
Kwenye hotuba kwa wanahabari Hussein ameweka wazi kwamba tiketi zote za mchuoano huo hazikuazwa (Sold out) kinyume na ilivyoripotiwa.
“Nataka niweke wazi kwamba kati ya tiketi 22,900 ambazo tulipewa na wahusika wa idadi ya mashabiki kuingia uwanja wa Nyayo ni tiketi 17,500 pekee ambazo ziliuzwa kwa mashabiki ila uwanja ulijaa hadi pomoni ,ukweli ni kwamba Kuna tiketi hazikuuzwa zote ukiwa na maana mashabiki wengine waliingia kinyume.
” Vyombo vya habari viliripoti kuuzwa kwa tiketi zote siku mbili kabla ya mchuoano huku pia shirikisho Hilo likithibitisha Hilo ila Rais huyo amekanusha kauli hiyo ya awali.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

